Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Câu: (57) Chương: Chương Al-Zukhruf
۞ وَلَمَّا ضُرِبَ ٱبۡنُ مَرۡيَمَ مَثَلًا إِذَا قَوۡمُكَ مِنۡهُ يَصِدُّونَ
Na washirikina walipopiga mfano wa Īsā mwana wa Maryam walipomjadili Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kumhoji kuwa Wanaswara wanamuabudu, unawakuta watu wako wanainua sauti zao na kupiga kelele kwa furaha na kuterema. Napo ni pale neno la Mwenyezi Mungu Aliyetukuka lilipoteremka (Nyinyi na vile mnavyoviabudu badala ya Mwenyezi Mungu ni kuni za Moto, nyinyi nyote ndani ya Moto huo mtaingia). Na washirikina wakasema, «Tumeridhika kwa waungu wetu wawe na cheo cha Īsā, Mwenyezi Mungu Akateremsha neno lake (Hakika wale ambao ilitangulia kutoka kwetu kuwa wao ni wema, hao ni wenye kuepushwa nao huo Moto). Yule anayetupwa Motoni, miongoni mwa waungu wa makafiri, ni yule aliyeridhika kuabudiwa na wao.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (57) Chương: Chương Al-Zukhruf
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại