Check out the new design

Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Chương: Al-Dukhan   Câu:
وَأَن لَّا تَعۡلُواْ عَلَى ٱللَّهِۖ إِنِّيٓ ءَاتِيكُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu kwa kuwakanusha Mitume Wake, kwani mimi ni mwenye kuwajia na hoja waziwazi ya ukweli wa utume wangu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَإِنِّي عُذۡتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمۡ أَن تَرۡجُمُونِ
Na mimi nimejihami kwa Mwenyezi Mungu msipate kuniua kwa kunipiga mawe.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَإِن لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ لِي فَٱعۡتَزِلُونِ
Na iwapo hamniamini kwa haya niliokuja nayo, basi niacheni nifuate njia yangu na muache kuniudhi.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنَّ هَٰٓؤُلَآءِ قَوۡمٞ مُّجۡرِمُونَ
Hapo Mūsā akamuomba Mola wake, Fir’awn na watu wake walipomkanusha, akisema, «Hakika hawa ni watu wenye kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kumkanusha.”
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَأَسۡرِ بِعِبَادِي لَيۡلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Basi enda na waja wangu waliokuamini, wakakusadiki na wakakufuata, ewe Mūsā, katika kipindi cha usiku, kwani nyinyi mtafuatwa na Fir’awn na askari wake. Na nyinyi mtaokolewa, na Fir’awn askari wake watazama.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱتۡرُكِ ٱلۡبَحۡرَ رَهۡوًاۖ إِنَّهُمۡ جُندٞ مُّغۡرَقُونَ
Na iache bahari hali ilivyo utakapopita, ikiwa imetulia haina mchafuko. Hakika Fir’awn na askari wake ni wenye kuzamishwa humo baharini.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَمۡ تَرَكُواْ مِن جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Ni vingapi alivyoviacha Fir’awn na watu wake, baada ya kuangamia kwao na kuzamishwa baharini na Mwenyezi Mungu, miongoni mwa mabustani na mashamba yaliyostawi, chemchemi za maji yenye kupita,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَزُرُوعٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ
Namazao na majumba mazuri na maisha
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَنَعۡمَةٖ كَانُواْ فِيهَا فَٰكِهِينَ
waliokuwa nayo ya neema na anasa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا قَوۡمًا ءَاخَرِينَ
Mfano wa mateso hayo ndivyo Mwenyezi Mungu Anavyowatesa wenye kukanusha na kubadilisha neema za Mwenyezi Mungu kwa kuzikanusha. Na tuliwarithisha neema hizo, baada ya Fir’awn na watu wake, watu wengine waliokuja baada yao wakashika nafasi yao miongoni mwa Wana wa Isrāīl.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَمَا بَكَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلسَّمَآءُ وَٱلۡأَرۡضُ وَمَا كَانُواْ مُنظَرِينَ
Mbingu na ardhi hazikulia kwa kumsikitikia Fir’awn na watu wake, na hawakuwa ni wenye kucheleshewa adhabu iliyowashukia.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَلَقَدۡ نَجَّيۡنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ مِنَ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡمُهِينِ
Kwa hakika, tuliwaokoa Wana wa Isrāīl kutokana na adhabu yenye kuwafanya wanyonge kwa kuuawa watoto wao wa kiume na kutumishwa wanawake wao.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
مِن فِرۡعَوۡنَۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيٗا مِّنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ
Kutokana na Fir’awn. Hakika yeye alikuwa mjeuri, miongoni mwa washirikina, aliyepita mpaka katika kujigamba na kuwafanyia kiburi waja wa Mwenyezi Mungu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَلَقَدِ ٱخۡتَرۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ عِلۡمٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na kwa hakika, tuliwachagua Wana wa Isrāīl, kwa kuwajua kwetu, juu ya walimwengu wa zama zao.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَءَاتَيۡنَٰهُم مِّنَ ٱلۡأٓيَٰتِ مَا فِيهِ بَلَٰٓؤٞاْ مُّبِينٌ
Tukawapatia miujiza, kupitia kwa Mūsā, ambayo ilikuwa ni mtihani na maonjo kwao ya raha na shida.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ
Hakika hawa washirikina wa watu wako, ewe Mtume, wanasema,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنۡ هِيَ إِلَّا مَوۡتَتُنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُنشَرِينَ
”Hakuna kifo chochote ila kile kifo chetu tutakachokufia , nacho ndicho kifo cha mwanzo na cha mwisho, na sisi baada ya kufa kwetu hatutakuwa ni wenye kufufuliwa tuhesabiwe na tulipwe mema au tuteswe.”
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَأۡتُواْ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ
Na wanasema pia, «Basi tuletee, ewe Muhammad: wewe na walio pamoja na wewe, wazazi wetu waliokufa, iwapo nyinyi ni wakweli kwamba Mwenyezi Mungu Atawafufua walio makaburini wakiwa hai.”
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَهُمۡ خَيۡرٌ أَمۡ قَوۡمُ تُبَّعٖ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ أَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ مُجۡرِمِينَ
Je, hawa washirikina ni bora au watu wa Tubba’ wa Himyar na wale waliokuwa kabla yao miongoni mwa ummah waliomkanusha Mola wao? Tuliwaangamiza kwa uhalifu wao na kukanusha kwao. Hawa washirikina si bora kuliko hao ili tuwasamehe na tusiwaangamize, na hali wao wanamkanusha Mwenyezi Mungu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا لَٰعِبِينَ
Na hatukuumba mbingu na ardhi na vilivyoko baina yake kwa mchezo.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
مَا خَلَقۡنَٰهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Hatukuviumba hivyo viwili isipokuwa kwa haki ambayo ndiyo mpango wa Mwenyezi Mungu katika kuumba Kwake na kupelekesha mambo Kwake. Lakini wengi wa hawa washirikina hawalijui hilo, na kwa hivyo hawavitii akilini vitu viwili hivyo, kwa kuwa wao hawatarajii kupata malipo mema wala hawaogopi mateso.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Al-Dukhan
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 - Mục lục các bản dịch

阿卜杜拉·穆罕默德·艾布·比克尔和谢赫纳索尔·胡麦斯翻译

Đóng lại