Check out the new design

Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Câu: (10) Chương: Al-Hadid
وَمَا لَكُمۡ أَلَّا تُنفِقُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَلِلَّهِ مِيرَٰثُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ لَا يَسۡتَوِي مِنكُم مَّنۡ أَنفَقَ مِن قَبۡلِ ٱلۡفَتۡحِ وَقَٰتَلَۚ أُوْلَٰٓئِكَ أَعۡظَمُ دَرَجَةٗ مِّنَ ٱلَّذِينَ أَنفَقُواْ مِنۢ بَعۡدُ وَقَٰتَلُواْۚ وَكُلّٗا وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلۡحُسۡنَىٰۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ
Na ni kitu gani kinachowazuia nyinyi kutoa katika njia ya Mwenyezi Mungu? Hakika ni kwamba Mwenyezi Mungu Ndiye Mwenye urithi wa mbingu na ardhi, Anavirithi vyote vilivyomo humo, na hatasalia yoyote kuwa ni mwenye kumiliki chochote humo. Hawalingani kimalipo na thawabu wale waliotoa kabla ya ufunguzi wa Makkah na wakapigana na wakanushaji na wasiokuwa wao, kwani wao wana daraja kubwa zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko wale waliotoa katika njia ya Mwenyezi Mungu baada ya ufunguzi na wakapigana na wakanushaji, na kila mojawapo ya makundi mawili haya Mwenyezi Mungu Ameliahidi Pepo. Na Mwenyezi Mungu ni Mtambuzi wa matendo yenu, hakuna chchote katika hayo kinachofichamana Kwake, na Atawalipa nyinyi kwa hayo.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (10) Chương: Al-Hadid
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - 斯瓦西里语翻译 - 阿卜杜拉·穆罕默德和纳索尔·胡麦斯 - Mục lục các bản dịch

阿卜杜拉·穆罕默德·艾布·比克尔和谢赫纳索尔·胡麦斯翻译

Đóng lại