Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Câu: (10) Chương: Chương Al-Mumtahinah
يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا جَآءَكُمُ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتُ مُهَٰجِرَٰتٖ فَٱمۡتَحِنُوهُنَّۖ ٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِإِيمَٰنِهِنَّۖ فَإِنۡ عَلِمۡتُمُوهُنَّ مُؤۡمِنَٰتٖ فَلَا تَرۡجِعُوهُنَّ إِلَى ٱلۡكُفَّارِۖ لَا هُنَّ حِلّٞ لَّهُمۡ وَلَا هُمۡ يَحِلُّونَ لَهُنَّۖ وَءَاتُوهُم مَّآ أَنفَقُواْۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ أَن تَنكِحُوهُنَّ إِذَآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّۚ وَلَا تُمۡسِكُواْ بِعِصَمِ ٱلۡكَوَافِرِ وَسۡـَٔلُواْ مَآ أَنفَقۡتُمۡ وَلۡيَسۡـَٔلُواْ مَآ أَنفَقُواْۚ ذَٰلِكُمۡ حُكۡمُ ٱللَّهِ يَحۡكُمُ بَيۡنَكُمۡۖ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٞ
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkafuata Sheria Zake kivitendo! Wakiwajia nyinyi wanawake Waumini wakiwa wamehama kutoka nchi ya ukafiri kuja kwenye nchi ya Uislamu, wafanyieni mtihani, ili mjue ukweli wa Imani yao, Mwenyezi Mungu Ndiye Mjuzi zaidi wa Imani yao. Mkiwajua kuwa ni Waumini kulingana na alama na ushahidi uliowafunukia, basi msiwarudishe kwa waume wao makafiri. Kwani wanawake Waumini si halali waolewe na makafiri, na makafiri si halali wawaoe wanawake Waumini. Nawapeni waume wa wale wanawake waliosilimu mahari waliotoa kuwapa hao wanawake. Na si dhambi kwenu kuwaoa mkiwapa mahari yao. Na msishikilie kuendelea na ndoa za wake wenu waliokufuru. Na takeni kwa washirikina mrudishiwe mahari mliotoa kuwapa wanawake wenu walioritadi na wakaungana na hao washirikina. Na wao watake kurudishiwa mahari waliotoa kwa wanawake wao waliosilimu na wakaungana na nyinyi. Hukumu hii iliyotajwa katika aya ni hukumu ya Mwenyezi Mungu Anahukumu baina yenu, basi msiende kinyume nayo. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, hakuna kitu chochote kinachofichamana Kwake, ni Mwingi wa hekima katika maneno Yake na vitendo Vyake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (10) Chương: Chương Al-Mumtahinah
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại