Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Câu: (10) Chương: Chương Al-Tahrim
ضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلٗا لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱمۡرَأَتَ نُوحٖ وَٱمۡرَأَتَ لُوطٖۖ كَانَتَا تَحۡتَ عَبۡدَيۡنِ مِنۡ عِبَادِنَا صَٰلِحَيۡنِ فَخَانَتَاهُمَا فَلَمۡ يُغۡنِيَا عَنۡهُمَا مِنَ ٱللَّهِ شَيۡـٔٗا وَقِيلَ ٱدۡخُلَا ٱلنَّارَ مَعَ ٱلدَّٰخِلِينَ
Mwenyezi Mungu Anapiga mfano wa hali ya makafiri- katika kutangamana kwao na Waislamu, kuwa karibu na wao na kutangamana nao na kwamba hilo halitawanufaisha kwa kuwa wamemkufuru Mwenyezi Mungu- kuwa ni kama hali ya mke wa Nabii wa Mwenyezi Mungu, Nūḥ, na mke wa Nabii wa Mwenyezi mungu, Lūṭ, kwa kuwa wote wawili walikuwa chini ya hifadhi ya ndoa ya waja wawili wema miongoni mwa waja wetu, ukapatikana kutoka kwao kuwafanyia uhaini wa kidini, kwani wote wawili walikuwa makafiri. Mitume wawili hawa hawakuweza kuwatetea wake zao na adhabu ya Mwenyezi Mungu, na wakaambiwa wake wawili hao, «Ingieni Motoni pamoja na wenye kuingia huko.» Katika kupiga mfano huu pana dalili ya kwamba kuwa karibu na Manabii na watu wema hakufai kitu iwapo mtu mwenyewe ana matendo mabaya.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (10) Chương: Chương Al-Tahrim
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại