Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani * - Mục lục các bản dịch

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ý nghĩa nội dung Câu: (19) Chương: Chương Yunus
وَمَا كَانَ ٱلنَّاسُ إِلَّآ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ فَٱخۡتَلَفُواْۚ وَلَوۡلَا كَلِمَةٞ سَبَقَتۡ مِن رَّبِّكَ لَقُضِيَ بَيۡنَهُمۡ فِيمَا فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ
Wala watu hawakuwa ila Umma mmoja tu. Kisha wakakhitalifiana. Na lau kuwa si neno lililo kwisha tangulia kutokana na Mola wako Mlezi, hapana shaka hukumu ingeli kwisha katwa baina yao katika hayo wanayo khitalifiana.
Watu kwa maumbile yao hawakuwa ila ni Umma mmoja tu. Kisha tukawapelekea Mitume wawaongoze na wawaongoe kwa mujibu wa Ufunuo wa Mwenyezi Mungu Mtukufu. Ikawa tabia ya kibinaadamu iliyo pelekea kheri na shari ndiyo sababu ya kuwa na nguvu zaidi shari katika baadhi yao. Juu yao hao matamanio na nyendo za Shetani zikatawala, na kwa hivyo wakakhitalifiana. Na lau kuwa hukumu ya Mola wako Mlezi haikutangulia ya kuwapa muhula makafiri kwa ajili yako, Ewe Nabii, na kuakhirisha maangamizo yao mpaka siku maalumu iliyo ahidiwa, Mwenyezi Mungu angeli wapelekea upesi maangamizo na adhabu, kwa sababu ya mfarakano waliyo uingia, kama zilivyo ingia kaumu zilizo kwisha pita.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (19) Chương: Chương Yunus
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili do 'Ali Muhsin Al-Barwani dịch thuật

Đóng lại