《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 * - 译解目录


含义的翻译 段: (37) 章: 艾哈拉布
وَإِذۡ تَقُولُ لِلَّذِيٓ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ وَأَنۡعَمۡتَ عَلَيۡهِ أَمۡسِكۡ عَلَيۡكَ زَوۡجَكَ وَٱتَّقِ ٱللَّهَ وَتُخۡفِي فِي نَفۡسِكَ مَا ٱللَّهُ مُبۡدِيهِ وَتَخۡشَى ٱلنَّاسَ وَٱللَّهُ أَحَقُّ أَن تَخۡشَىٰهُۖ فَلَمَّا قَضَىٰ زَيۡدٞ مِّنۡهَا وَطَرٗا زَوَّجۡنَٰكَهَا لِكَيۡ لَا يَكُونَ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ حَرَجٞ فِيٓ أَزۡوَٰجِ أَدۡعِيَآئِهِمۡ إِذَا قَضَوۡاْ مِنۡهُنَّ وَطَرٗاۚ وَكَانَ أَمۡرُ ٱللَّهِ مَفۡعُولٗا
Na pindi unaposema, ewe Nabii, kumwambia yule ambaye Mwenyezi Mungu Amemneemesha kwa Uislamu, naye ni Zayd bin Harithah ambaye Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na wewe ukamneemesha kwa kumuacha huru, «Baki na mke wako, Zaynab binti Jahsh, na usimuache! na muogope Mwenyezi Mungu , ewe Zayd!» na huku unaficha, ewe Nabii, katika nafsi yako kile Alichokuletea wahyi nacho Mwenyezi Mungu cha Zayd kumuacha Zaynab na kuwa wewe utamuoa. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ni Mwenye kudhihirisha ulichokificha, na unaogopa wasije wanafiki wakasema kwamba Muhammad amemuoa mtalaka wa mwanawe wa kubandika, na Mwenyezi Mungu Anastahiki zaidi umuogope. Basi Zayd alipomaliza haja yake kwa Zaynab na akamuacha kisha eda lake likamalizika, tulikuoza wewe, ili uwe ni kiigizo katika kubatilisha mila ya uharamishaji wa kuoa mke wa mwana wa kubandika baada ya kuachwa, wala haitakuwa kosa na dhambi kwa Wamini kuwaoa wake za wale watoto wao wa kubandika baada kuwaacha iwapo wamemaliza haja yao kwao. Na kwa hakika amri ya Mwenyezi Mungu ni yenye kufanyika, hakuna mwenye kuiwekea pingamizi wala kuizuia. Ada ya kujibandika mtoto ilikuwako zama za kijinga (kabla ya Uislamu) kisha ikabatilishwa kwa neno lake Mwenyezi Mungu, «Waiteni wao kwa kuwanasibisha na baba zao..».
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 段: (37) 章: 艾哈拉布
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 阿布杜拉·穆罕默德和纳赛尔·海米斯。 - 译解目录

古兰经斯瓦希里文译解,阿布杜拉·穆罕默德·艾布·拜克尔博士和谢赫纳赛尔·哈米斯翻译。

关闭