Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Ayah: (37) Surah: Al-Ahzāb
وَإِذۡ تَقُولُ لِلَّذِيٓ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ وَأَنۡعَمۡتَ عَلَيۡهِ أَمۡسِكۡ عَلَيۡكَ زَوۡجَكَ وَٱتَّقِ ٱللَّهَ وَتُخۡفِي فِي نَفۡسِكَ مَا ٱللَّهُ مُبۡدِيهِ وَتَخۡشَى ٱلنَّاسَ وَٱللَّهُ أَحَقُّ أَن تَخۡشَىٰهُۖ فَلَمَّا قَضَىٰ زَيۡدٞ مِّنۡهَا وَطَرٗا زَوَّجۡنَٰكَهَا لِكَيۡ لَا يَكُونَ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ حَرَجٞ فِيٓ أَزۡوَٰجِ أَدۡعِيَآئِهِمۡ إِذَا قَضَوۡاْ مِنۡهُنَّ وَطَرٗاۚ وَكَانَ أَمۡرُ ٱللَّهِ مَفۡعُولٗا
Na pindi unaposema, ewe Nabii, kumwambia yule ambaye Mwenyezi Mungu Amemneemesha kwa Uislamu, naye ni Zayd bin Harithah ambaye Mtume , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na wewe ukamneemesha kwa kumuacha huru, «Baki na mke wako, Zaynab binti Jahsh, na usimuache! na muogope Mwenyezi Mungu , ewe Zayd!» na huku unaficha, ewe Nabii, katika nafsi yako kile Alichokuletea wahyi nacho Mwenyezi Mungu cha Zayd kumuacha Zaynab na kuwa wewe utamuoa. Na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ni Mwenye kudhihirisha ulichokificha, na unaogopa wasije wanafiki wakasema kwamba Muhammad amemuoa mtalaka wa mwanawe wa kubandika, na Mwenyezi Mungu Anastahiki zaidi umuogope. Basi Zayd alipomaliza haja yake kwa Zaynab na akamuacha kisha eda lake likamalizika, tulikuoza wewe, ili uwe ni kiigizo katika kubatilisha mila ya uharamishaji wa kuoa mke wa mwana wa kubandika baada ya kuachwa, wala haitakuwa kosa na dhambi kwa Wamini kuwaoa wake za wale watoto wao wa kubandika baada kuwaacha iwapo wamemaliza haja yao kwao. Na kwa hakika amri ya Mwenyezi Mungu ni yenye kufanyika, hakuna mwenye kuiwekea pingamizi wala kuizuia. Ada ya kujibandika mtoto ilikuwako zama za kijinga (kabla ya Uislamu) kisha ikabatilishwa kwa neno lake Mwenyezi Mungu, «Waiteni wao kwa kuwanasibisha na baba zao..».
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Ayah: (37) Surah: Al-Ahzāb
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis - Indise ng mga Salin

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an sa Wikang Swahili. Isinalin ito nina Doktor Abdullah Muhammad Abu Bakr at Shaykh Nasir Khamis. Inilathala ito ng King Fahd Glorious Quran Printing Complex sa Madinah Munawwarah, imprenta ng taong 1435 H.

Isara