《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 章: 印菲塔尔   段:

Surat Al-Infitar

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ
Mbingu itapo chanika!
Itakapo pasuka mbingu,
阿拉伯语经注:
وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ
Na nyota zitapo tawanyika!
Na nyota zitakapo pukutika na kutawanyika,
阿拉伯语经注:
وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ
Na bahari zitakapo pasuliwa!
Na bahari zikafurika na kuingiliana kwa kuondoka viziwizi baina yao,
阿拉伯语经注:
وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ
Na makaburi yatapo fukuliwa!
Na makaburi yakafunuliwa na wakatoka maiti walio kuwamo,
阿拉伯语经注:
عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
Hapo basi kila nafsi itajua nini kheri au shari iliyo tanguliza na iliyo chelewesha.
阿拉伯语经注:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
Ewe mwanaadamu! Kitu gani kilicho kukhadaa wewe na Mola wako Mlezi Mtukufu hata ukafanya jeuri ya kwenda kumuasi? (Ni dhaahiri kuwa Sayyid Abdulla bin Ali bin Nassir aliye tunga utenzi wa Kiswahili maarufu uitwao Al Inkishaf aliiwaza Aya hii alipo tunga ubeti huu: Moyo wangu nini huzundukani Likughurielo hela ni nni? Hunelezi nami kalibaini Liwapo na sura nisikataye )
阿拉伯语经注:
ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha!
Mungu wako huyo ndiye aliye kuumba nawe hukuwa chochote, akakuumba na viungo vya kukuletea manufaa, akakufanya umenyooka kwa umbo sawa sawa.
阿拉伯语经注:
فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
Akakujenga na akakuleta katika sura yoyote aliyo itaka.
阿拉伯语经注:
كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
Hamwachi? Bali nyinyi mnakadhibisha malipo ya Siku ya Kiyama!
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
Na hakika wapo juu yenu Malaika walinzi, ambao ni waheshimiwa kwetu,
阿拉伯语经注:
كِرَامٗا كَٰتِبِينَ
Waandishi wenye hishima,
Wanasajili vitendo vyenu vyote mvitendavyo, vya kheri na shari.
阿拉伯语经注:
يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ
Wanayajua mnayo yatenda.
Wanayajua mnayo yafanya ya kheri na ya shari
阿拉伯语经注:
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
Hakika wale walio ni wa kweli katika Imani yao wapo katika neema kubwa.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
Na hakika walio iacha amri ya Mwenyezi bila ya shaka watakuwa katika Moto unao unguza,
阿拉伯语经注:
يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Wataingia humo Siku ya Malipo.
Wataingia humo Siku ya Malipo.
阿拉伯语经注:
وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ
Na hawatoacha kuwamo humo.
Na wala hawatatoka katika Jahannamu!
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
Na nini kitakujuvya ni nini hiyo Siku ya Malipo, na mambo yake yamepindukia ujuzi wako na fikra zako?
阿拉伯语经注:
ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
Tena ni nini kitacho kujuvya ni nini hiyo Siku ya Malipo kwa vitisho vyake na shida zake?
阿拉伯语经注:
يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
Siku ambayo nafsi haitakuwa na mamlaka yoyote juu ya nafsi ya kuifaa au kuidhuru; na amri yote siku hiyo itakuwa ni ya Mwenyezi Mungu peke yake!
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 印菲塔尔
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭