Check out the new design

《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 盖拉姆   段:
إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyowajaribu wale wenye shamba, walipoapa kwamba watayavuna mazao yake itakapokuwa asubuhi.
阿拉伯语经注:
وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
阿拉伯语经注:
فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
阿拉伯语经注:
فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ
Likawa kama usiku wa giza.
阿拉伯语经注:
فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ
Asubuhi wakaitana.
阿拉伯语经注:
أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
阿拉伯语经注:
فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana.
阿拉伯语经注:
أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
阿拉伯语经注:
وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
阿拉伯语经注:
فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ
Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!
阿拉伯语经注:
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali tumenyimwa!
阿拉伯语经注:
قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
阿拉伯语经注:
قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
阿拉伯语经注:
فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
阿拉伯语经注:
قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
阿拉伯语经注:
عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lililo bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
阿拉伯语经注:
كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangelijua!
阿拉伯语经注:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Hakika wacha Mungu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
阿拉伯语经注:
أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
阿拉伯语经注:
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Mna nini? Mnahukumu vipi?
阿拉伯语经注:
أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
阿拉伯语经注:
إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Kuwa mtapata humo mnayoyapenda?
阿拉伯语经注:
أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayojihukumia?
阿拉伯语经注:
سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
阿拉伯语经注:
أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
阿拉伯语经注:
يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ
Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 盖拉姆
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 - 译解目录

由拉瓦德翻译中心团队与拉布瓦 الدعوة协会和伊斯兰内容服务协会合作翻译。

关闭