Check out the new design

《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 穆勒萨拉提   段:

Al-Mursalat

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا
Ninaapa kwa zinazotumwa kwa upole!
阿拉伯语经注:
فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا
Na zinazovuma kwa kasi!
阿拉伯语经注:
وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا
Na zikaeneza maeneo yote!
阿拉伯语经注:
فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا
Na zinazofarikisha zikatawanya!
阿拉伯语经注:
فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا
Na zinazopeleka mawaidha!
阿拉伯语经注:
عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا
Kuwa udhuru au kuonya.
阿拉伯语经注:
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ
Hakika mnayoahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
阿拉伯语经注:
فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ
Wakati nyota zitakapofutwa.
阿拉伯语经注:
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ
Na mbingu zitakapopasuliwa.
阿拉伯语经注:
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ
Na milima itakapopeperushwa.
阿拉伯语经注:
وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao.
阿拉伯语经注:
لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
阿拉伯语经注:
لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ
Kwa siku ya kupambanua!
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ
Na nini kitakachokujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao, siku hiyo hao wanaokanusha!
阿拉伯语经注:
أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Kwani hatukuwaangamiza waliotangulia?
阿拉伯语经注:
ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ
Kisha tukawafuatilizia waliofuatia?
阿拉伯语经注:
كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!
阿拉伯语经注:
أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
阿拉伯语经注:
فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
阿拉伯语经注:
إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ
Mpaka muda maalumu?
阿拉伯语经注:
فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!
阿拉伯语经注:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya.
阿拉伯语经注:
أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا
Walio hai na maiti?
阿拉伯语经注:
وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!
阿拉伯语经注:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Nendeni kwenye adhabu mliyokuwa mkiikanusha!
阿拉伯语经注:
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
阿拉伯语经注:
لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.
阿拉伯语经注:
إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!
阿拉伯语经注:
كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!
阿拉伯语经注:
هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu.
阿拉伯语经注:
وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao waliokanusha!
阿拉伯语经注:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na waliotangulia.
阿拉伯语经注:
فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ
Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao waliokanusha!
阿拉伯语经注:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ
Hakika wacha Mungu watakuwa katika vivuli na chemchemI.
阿拉伯语经注:
وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ
Na matunda wanayoyapenda.
阿拉伯语经注:
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyokuwa mkiyatenda.
阿拉伯语经注:
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hakika ndio kama hivyo tunavyowalipa watendao mema.
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!
阿拉伯语经注:
كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!
阿拉伯语经注:
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
阿拉伯语经注:
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ
Ole wao siku hiyo hao wanaokanusha!
阿拉伯语经注:
فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 穆勒萨拉提
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 - 译解目录

由拉瓦德翻译中心团队与拉布瓦 الدعوة协会和伊斯兰内容服务协会合作翻译。

关闭