የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ * - የትርጉሞች ማዉጫ


የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል ጋሺያህ   አንቀጽ:

Surat Al-Ghashiyah

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ
Je, ilikujia,ewe Mtume, habari ya Kiyama chenye vituko venye kuwaenea watu?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ
Nyuso za Makafiri, Siku hiyo, zitakuwa zimenyongeka kwa adhabu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ
Zishughulishie, zimechoka na kutaabika.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ
Zinachomwa kwa Moto wenye kuwaka kwa ukali.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ
Zitanyweshwa maji ya chemchemi yenye moto sana.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ
Watu wa Motoni hawatakuwa na chakula isipokuwa kinachotoka kwenye mti wa miba ilioshikana na chini. Ni kibaya sana chakula hiko na ni kichafu mno.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ
Hakimnoneshi mwenye kukila, awapo amekonda, wala hakimuondolei njaa, awapo na njaa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ
Nyuso za Waumini, siku ya Kiyama, zitakuwa kwenye neema.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ
Kwa kuwa zilijishughulisha ulimwenguni kumtii Mwenyezi Mungu na kuridhika na Akhera.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ
Zitakuwa kwenye Pepo ya daraja ya juu.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ
Hutasikia humo hata neno moja la upuuzi.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ
Ndani yake kuna chemchemi yenye kuteremka maji yake.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ
Ndani yake mna vitanda vilioangatika,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ
na vikombe vilivyotayarishwa kwa wenye kunywa,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ
na mito iliyopangwa, mmoja baada ya mwingine,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ
na mazulia mengi yaliyotandikwa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ
Kwani, hawa makafiri wenye kukanusha, hawaangalii ngamia namna walivyoumbwa kiajabu?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ
Na mbingu namna zlizoinuliwa juu kwa namna ya kupendeza?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ
Na milima namna iliyoimarishwa ukapatikana uthabiti na utulivu wa ardhi?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ
Na ardhi namna ilivyotandikwa na kutayarishwa?
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ
Basi wawaidhie, ewe Mtume, wale wenye kupa nyongo yale uliyotumilizwa kwayo wala usihuzunike kwa kupa mgongo kwao.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ
Kwani wewe ni muwaidhiaji kwao, na si juu yako kuwalazimisha kuamini..
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ
Lakini yule mwenye kuyapa mgongo makumbusho na mawaidha na akawa mkakamavu kwenye ukafiri wake,
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ
Mwenyezi Mungu Atamuadhibu adhabu kali Motoni.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ
Hakika wao watarudi kwetu baada ya kufa.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم
Kisha ni juu yetu kuwalipa kwa waliyoyafanya.
የአረብኛ ቁርኣን ማብራሪያ:
 
የይዘት ትርጉም ምዕራፍ: ሱረቱ አል ጋሺያህ
የምዕራፎች ማውጫ የገፅ ቁጥር
 
የቅዱስ ቁርዓን ይዘት ትርጉም - የ እስዋሂሊ ቋንቋ ትርጉም - በአብደላህ ሙሀመድ ናስር ከሚስ - የትርጉሞች ማዉጫ

የተከበረው ቁርአን ስዋሂሊኛ መልዕክተ ትርጉም - በዶ/ር ሙሐመድ ዓብደሏህ አቡ በክር እና ሸይኽ ናሲር ኸሚስ

መዝጋት