Check out the new design

Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili - Ali Muhsin Al-Barwani. * - Übersetzungen

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Al-Balad   Vers:

Al-Balad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Naapa kwa Mji huu! [1]
[1] Naapa kiapo cha mkazo kwa mji wa Makka, mji mtakatifu;
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Nawe unaukaa Mji huu. [2]
[2] Na wewe unaishi katika mji huu, unauzidisha utukufu wake na cheo chake.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa. [3]
[3] Na naapa kwa mzazi na anacho kizaa, na kwa hao wawili ndio jinsi inahifadhika na maendeleo yanabakia.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu. [4]
[4] Hakika Sisi tumemuumba mtu katika mashaka na taabu tangu mwanzo wake mpaka kumalizika mambo yake.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza? [5]
[5] Je! Anadhani mtu aliye umbwa katika mashaka haya kuwa hapana awezae kumdhalilisha?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali. [6]
[6] Anasema: Nimetumia katika kupambana na Muhammad s.a.w. na kuupinga wito wake mali mengi ukiyakusanya pamoja.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona? [7]
[7] Ati anadhani kwamba mambo yake hayo yamefichikana, hayajui yeyote hata huyo aliye muumba?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili? [8]
[8] Kwani Sisi hatukumuumba na macho mawili ya kutazamia,?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
Na ulimi, na midomo miwili? [9]
[9] Na ulimi na midomo miwili ili aweze kutamka na kusema sawa?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
Na tukambainishia zote njia mbili? [10]
[10] Na tukamwonyesha njia ya kheri na ya shari, na tukamtengenezea aweze kuchagua mojawapo?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani. [11]
[11] Basi huyo hakunafiika kwa tuliyo mtengenezea, wala hakuivuka njia ya milimani inayo mzuia asifikie uwokovu, nayo ni choyo wa nafsi yake.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani? [12]
[12] Na kitu gani kitakufunza nini huko kujitoma kwenye njia ya milimani?
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
فَكُّ رَقَبَةٍ
Kumkomboa mtumwa; [13]
[13] Kumkomboa mtu kutokana na utumwa,
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kumlisha siku ya njaa [14]
[14] Au kumlisha siku ya njaa
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
Yatima aliye jamaa, [15]
[15] Yatima aliye jamaa wa kumliwaza kwa ujamaa na ufakiri.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
Au masikini aliye vumbini. [16]
[16] Au masikini mwingi wa haja na kufakirika.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana. [17]
[17] Tena awe pamoja na hayo miongoni mwa wenye Imani wanao usiana na wenzao kwa subira na kuoneana huruma.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani. [18]
[18] Hao wanao sifika kwa sifa hizi, ndio watu wa kheri, wa mkono wa kulia.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni. [19]
[19] Na walio zikataa dalili tulizo zisimamisha kuthibitisha Haki kutoka na Kitabu na hoja zake, hao ndio wapotovu watu waovu walio kosa kheri na watapata adhabu.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande. [20]
[20] Juu yao utakuwa Moto ulio bebeana na milango yake ikafungwa.
Arabische Interpretationen von dem heiligen Quran:
 
Übersetzung der Bedeutungen Surah / Kapitel: Al-Balad
Suren/ Kapiteln Liste Nummer der Seite
 
Übersetzung der Bedeutungen von dem heiligen Quran - Die Übersetzung in Swahili - Ali Muhsin Al-Barwani. - Übersetzungen

Übersetzung von Ali Muhsin Al-Barwani.

Schließen