クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany * - 対訳の目次

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

対訳 章: 町章   節:

Surat Al-Balad

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Naapa kwa Mji huu!
Naapa kiapo cha mkazo kwa mji wa Makka, mji mtakatifu;
アラビア語 クルアーン注釈:
وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ
Nawe unaukaa Mji huu.
Na wewe unaishi katika mji huu, unauzidisha utukufu wake na cheo chake.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
Na naapa kwa mzazi na anacho kizaa, na kwa hao wawili ndio jinsi inahifadhika na maendeleo yanabakia.
アラビア語 クルアーン注釈:
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
Hakika Sisi tumemuumba mtu katika mashaka na taabu tangu mwanzo wake mpaka kumalizika mambo yake.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
Je! Anadhani mtu aliye umbwa katika mashaka haya kuwa hapana awezae kumdhalilisha?
アラビア語 クルアーン注釈:
يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
Anasema: Nimetumia katika kupambana na Muhammad s.a.w. na kuupinga wito wake mali mengi ukiyakusanya pamoja.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
Ati anadhani kwamba mambo yake hayo yamefichikana, hayajui yeyote hata huyo aliye muumba?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ
Kwani hatukumpa macho mawili?
Kwani Sisi hatukumuumba na macho mawili ya kutazamia,?
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ
Na ulimi, na midomo miwili?
Na ulimi na midomo miwili ili aweze kutamka na kusema sawa?
アラビア語 クルアーン注釈:
وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
Na tukambainishia zote njia mbili?
Na tukamwonyesha njia ya kheri na ya shari, na tukamtengenezea aweze kuchagua mojawapo?
アラビア語 クルアーン注釈:
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
Basi huyo hakunafiika kwa tuliyo mtengenezea, wala hakuivuka njia ya milimani inayo mzuia asifikie uwokovu, nayo ni choyo wa nafsi yake.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
Na kitu gani kitakufunza nini huko kujitoma kwenye njia ya milimani?
アラビア語 クルアーン注釈:
فَكُّ رَقَبَةٍ
Kumkomboa mtumwa;
Kumkomboa mtu kutokana na utumwa,
アラビア語 クルアーン注釈:
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kumlisha siku ya njaa
Au kumlisha siku ya njaa
アラビア語 クルアーン注釈:
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
Yatima aliye jamaa,
Yatima aliye jamaa wa kumliwaza kwa ujamaa na ufakiri.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
Au masikini aliye vumbini.
Au masikini mwingi wa haja na kufakirika.
アラビア語 クルアーン注釈:
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
Tena awe pamoja na hayo miongoni mwa wenye Imani wanao usiana na wenzao kwa subira na kuoneana huruma.
アラビア語 クルアーン注釈:
أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
Hao wanao sifika kwa sifa hizi, ndio watu wa kheri, wa mkono wa kulia.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
Na walio zikataa dalili tulizo zisimamisha kuthibitisha Haki kutoka na Kitabu na hoja zake, hao ndio wapotovu watu waovu walio kosa kheri na watapata adhabu.
アラビア語 クルアーン注釈:
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
Juu yao utakuwa Moto ulio bebeana na milango yake ikafungwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 町章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Ali Muhsen Alberwany

閉じる