Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman * - Translations’ Index


Translation of the meanings Surah: Al-Fajr   Ayah:

Surat Al-Fajr

وَٱلۡفَجۡرِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa alfajiri
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَيَالٍ عَشۡرٖ
na masiku kumi ya kwanza ya Mfungotatu na kwa kile kilichoyafanya yawe matukufu,
Arabic explanations of the Qur’an:
وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ
kwa kila idadi igawanyikayo na isiyogawanyika,
Arabic explanations of the Qur’an:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ
kwa usiku upitapo na giza lake.
Arabic explanations of the Qur’an:
هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ
Kwani hakuna katika kiapo kiliyotajwa chenye kukinaisha kwa mwenye akili?
Arabic explanations of the Qur’an:
أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Huoni, ewe Mtume, vipi Mola wako
Arabic explanations of the Qur’an:
إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ
Alivyoiangamiza kaumu ya Ād'. kabila la Irama lenye nguvu na majengo yaliyoinuliwa juu ya vipia,
Arabic explanations of the Qur’an:
ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ
ambalo hakukuumbwa mfano wake katika miji, kwa ukubwa wa miili na wingi wa nguvu?
Arabic explanations of the Qur’an:
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ
Na vipi Alivyowafanya Thamūd, kaumu ya Ṣāliḥ, ambao waliweza kuchonga jabali na kufanya nyumba ndani yake?
Arabic explanations of the Qur’an:
وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ
Na vipi Alivyomfanya Firauni, mfalme wa Misri, aliyekuwa na askari waliouhami ufalme wake na kuutilia nguvu.
Arabic explanations of the Qur’an:
ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ
Hawa ndio waliokitumia nguvu na kudhulumu mijini.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ
Wakaeneza humo, kwa dhuluma zao, uharibifu.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ
Mwenyezi Mungu Akawamiminia adhabu kali.
Arabic explanations of the Qur’an:
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ
Hakika Mola wako,ewe Mtume, Anamwangalia mwenye kumuasi kwa kumpa muhula kidogo, kisha Humpatiliza kwa uwezo na ushindi..
Arabic explanations of the Qur’an:
فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ
Huyu binadamu, Mola wake Anapompa mtihani wa neema, Anapomkunjulia riziki yake na kumpa maisha mazuri, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye ana cheo kwa Mola wake na huwa akisema :»Mola wangu Amenitukuza.»
Arabic explanations of the Qur’an:
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ
Na Anapomuonja na Akambania riziki yake, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye amefanywa mnyonge na Mwenyezi Mungu na huwa akisema: «Mola wangu Amenifanya mnyonge.».
Arabic explanations of the Qur’an:
كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ
Hali ya mambo si kama anavyodhania binadamu huyu, kwani mtu hutukuzwa kwa kumtii Mwenyzi Mungu na hufanywa mnyonge kwa kumuasi Mwenyezi Mungu. Na nyinyi hamwakirimu mayatima na kuwatendea wema.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hamhimizani kulisha maskini.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا
Na mnakula haki za watu, katika kurithi, kwa pupa.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا
Na mnapenda mali kupita kiasi.
Arabic explanations of the Qur’an:
كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا
Basi hali zenu zisiwe namna hiyo. Kumbukeni pindi ardhi itakapotikiswa na kuvunjwavunjwa.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا
Na Akaja Mola wako kutoa uamuzi kwa waja Wake hali Malaika wamepiga safu.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ
Na ukaletwa, Siku Hiyo kubwa, moto wa Jahanamu. Hiyo ndiyo Siku kafiri atakumbuka na kutubia. Kutamfalia nini sasa kukumbuka kwake na kutubia, na yeye katika ulimwengu alikuwa ameyapuuza hayo, na wakati wake umekwisha kupita?
Arabic explanations of the Qur’an:
يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي
Atakuwa akisema: ‘Laiti mimi nilitanguliza ulimwenguni amali zenye kunifaa katika maisha yangu ya Akhera’.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ
Katika Siku Hiyo ngumu yenye vituko, hakuna atakaye kuweza kuadhibu kama adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa anayemuasi.
Arabic explanations of the Qur’an:
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ
Na hakuna atakaye kuweza kufunga kama kifungo Chake wala kufikia hadi yake.
Arabic explanations of the Qur’an:
يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ
Ewe nafsi iliyotulia kwa kumtaja Mwenyezi Mungu, kumwamini Yeye na kuamini starehe ya Pepo Aliyowaandalia waumini!
Arabic explanations of the Qur’an:
ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ
Rudi kwa Mola wako hali ya kuridhika na takrima ya Mwenyezi Mungu kwako na hali ya kuwa Mwenyezi Mungu Ameridhika na wewe.
Arabic explanations of the Qur’an:
فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي
Ingia miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu walio wema
Arabic explanations of the Qur’an:
وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي
na ingia kwenye Pepo yangu.
Arabic explanations of the Qur’an:
 
Translation of the meanings Surah: Al-Fajr
Surahs’ Index Page Number
 
Translation of the Meanings of the Noble Qur'an - Swahili translation - Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis Abdurahman - Translations’ Index

Translation of the Quran meanings into Swahili by Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

close