Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis * - Índice de traducciones


Traducción de significados Capítulo: Sura Al-Fajr   Versículo:

Surat Al-Fajr

وَٱلۡفَجۡرِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa wakati wa alfajiri
Las Exégesis Árabes:
وَلَيَالٍ عَشۡرٖ
na masiku kumi ya kwanza ya Mfungotatu na kwa kile kilichoyafanya yawe matukufu,
Las Exégesis Árabes:
وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ
kwa kila idadi igawanyikayo na isiyogawanyika,
Las Exégesis Árabes:
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ
kwa usiku upitapo na giza lake.
Las Exégesis Árabes:
هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ
Kwani hakuna katika kiapo kiliyotajwa chenye kukinaisha kwa mwenye akili?
Las Exégesis Árabes:
أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ
Huoni, ewe Mtume, vipi Mola wako
Las Exégesis Árabes:
إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ
Alivyoiangamiza kaumu ya Ād'. kabila la Irama lenye nguvu na majengo yaliyoinuliwa juu ya vipia,
Las Exégesis Árabes:
ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ
ambalo hakukuumbwa mfano wake katika miji, kwa ukubwa wa miili na wingi wa nguvu?
Las Exégesis Árabes:
وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ
Na vipi Alivyowafanya Thamūd, kaumu ya Ṣāliḥ, ambao waliweza kuchonga jabali na kufanya nyumba ndani yake?
Las Exégesis Árabes:
وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ
Na vipi Alivyomfanya Firauni, mfalme wa Misri, aliyekuwa na askari waliouhami ufalme wake na kuutilia nguvu.
Las Exégesis Árabes:
ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ
Hawa ndio waliokitumia nguvu na kudhulumu mijini.
Las Exégesis Árabes:
فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ
Wakaeneza humo, kwa dhuluma zao, uharibifu.
Las Exégesis Árabes:
فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ
Mwenyezi Mungu Akawamiminia adhabu kali.
Las Exégesis Árabes:
إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ
Hakika Mola wako,ewe Mtume, Anamwangalia mwenye kumuasi kwa kumpa muhula kidogo, kisha Humpatiliza kwa uwezo na ushindi..
Las Exégesis Árabes:
فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ
Huyu binadamu, Mola wake Anapompa mtihani wa neema, Anapomkunjulia riziki yake na kumpa maisha mazuri, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye ana cheo kwa Mola wake na huwa akisema :»Mola wangu Amenitukuza.»
Las Exégesis Árabes:
وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ
Na Anapomuonja na Akambania riziki yake, huwa akidhani kuwa hayo ni kwa kuwa yeye amefanywa mnyonge na Mwenyezi Mungu na huwa akisema: «Mola wangu Amenifanya mnyonge.».
Las Exégesis Árabes:
كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ
Hali ya mambo si kama anavyodhania binadamu huyu, kwani mtu hutukuzwa kwa kumtii Mwenyzi Mungu na hufanywa mnyonge kwa kumuasi Mwenyezi Mungu. Na nyinyi hamwakirimu mayatima na kuwatendea wema.
Las Exégesis Árabes:
وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hamhimizani kulisha maskini.
Las Exégesis Árabes:
وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا
Na mnakula haki za watu, katika kurithi, kwa pupa.
Las Exégesis Árabes:
وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا
Na mnapenda mali kupita kiasi.
Las Exégesis Árabes:
كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا
Basi hali zenu zisiwe namna hiyo. Kumbukeni pindi ardhi itakapotikiswa na kuvunjwavunjwa.
Las Exégesis Árabes:
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا
Na Akaja Mola wako kutoa uamuzi kwa waja Wake hali Malaika wamepiga safu.
Las Exégesis Árabes:
وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ
Na ukaletwa, Siku Hiyo kubwa, moto wa Jahanamu. Hiyo ndiyo Siku kafiri atakumbuka na kutubia. Kutamfalia nini sasa kukumbuka kwake na kutubia, na yeye katika ulimwengu alikuwa ameyapuuza hayo, na wakati wake umekwisha kupita?
Las Exégesis Árabes:
يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي
Atakuwa akisema: ‘Laiti mimi nilitanguliza ulimwenguni amali zenye kunifaa katika maisha yangu ya Akhera’.
Las Exégesis Árabes:
فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ
Katika Siku Hiyo ngumu yenye vituko, hakuna atakaye kuweza kuadhibu kama adhabu ya Mwenyezi Mungu kwa anayemuasi.
Las Exégesis Árabes:
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ
Na hakuna atakaye kuweza kufunga kama kifungo Chake wala kufikia hadi yake.
Las Exégesis Árabes:
يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ
Ewe nafsi iliyotulia kwa kumtaja Mwenyezi Mungu, kumwamini Yeye na kuamini starehe ya Pepo Aliyowaandalia waumini!
Las Exégesis Árabes:
ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ
Rudi kwa Mola wako hali ya kuridhika na takrima ya Mwenyezi Mungu kwako na hali ya kuwa Mwenyezi Mungu Ameridhika na wewe.
Las Exégesis Árabes:
فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي
Ingia miongoni mwa waja wa Mwenyezi Mungu walio wema
Las Exégesis Árabes:
وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي
na ingia kwenye Pepo yangu.
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Capítulo: Sura Al-Fajr
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al idioma swahili- Abdullah Mohamad y Naser Jamis - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por el Dr. Abdalla Mohamed Abubakar y Nassor Khamis

Cerrar