Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany * - Índice de traducciones

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Traducción de significados Capítulo: Sura Al-Qaari'a   Versículo:

Surat Al-Qari'ah

ٱلۡقَارِعَةُ
Inayo gonga!
AL-QAARIA'H, Inayo gonga, ni Kiyama, ambacho kinaanza kwa mpulizo wa mwanzo wa barugumu, na kinaishia itapo katwa hukumu baina ya watu.
Las Exégesis Árabes:
مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Nini Inayo gonga?
Kitu gani kilicho cha ajabu zaidi katika ukuu wake, na khatari zake na kitisho chake!
Las Exégesis Árabes:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
Na kitu gani kitacho kujuulisha hali ya AL-QAARIA'H katika kitisho chake juu ya nafsi za watu?
Las Exégesis Árabes:
يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
Siku hiyo watu watakuwa kama vipepeo kwa wingi na kuhangaika kulia na kushoto, madhaifu na wanyonge!
Las Exégesis Árabes:
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
Na milima itakuwa kama sufi iliyo tiwa rangi na kuchambuliwa kwa kutapanyika vipande mbali mbali na kupeperuka katika anga huku na huku.
Las Exégesis Árabes:
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
Ama yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, mema yake yakapindukia kuliko maovu yake,
Las Exégesis Árabes:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
Basi huyo atakuwa na maisha yatayo mridhisha mwenyewe, na nafsi yake itue.
Las Exégesis Árabes:
وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
Na ama ambaye mizani yake itakuwa nyepesi, na maovu yake yakazidi kuliko mema yake,
Las Exégesis Árabes:
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
Basi makaazi yake yatakuwa Jahannamu.
Las Exégesis Árabes:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
Na nini cha kukujuulisha ni nini Hawiya?
Las Exégesis Árabes:
نَارٌ حَامِيَةُۢ
Ni Moto mkali!
Moto ulio mkali, hapana moto unao fikilia ukali wake, hata ukichochewa vipi na kutiwa kuni gani!
Las Exégesis Árabes:
 
Traducción de significados Capítulo: Sura Al-Qaari'a
Índice de Capítulos Número de página
 
Traducción de los significados del Sagrado Corán - Traducción al suajili - Ali Muhsen Alberwany - Índice de traducciones

Traducción del significado del Noble Corán al suajili por Ali Muhsen Alberwany

Cerrar