Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني * - Sadržaj prijevodā

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Prijevod značenja Sura: Sura el-Karia   Ajet:

Surat Al-Qari'ah

ٱلۡقَارِعَةُ
Inayo gonga!
AL-QAARIA'H, Inayo gonga, ni Kiyama, ambacho kinaanza kwa mpulizo wa mwanzo wa barugumu, na kinaishia itapo katwa hukumu baina ya watu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Nini Inayo gonga?
Kitu gani kilicho cha ajabu zaidi katika ukuu wake, na khatari zake na kitisho chake!
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Na nini kitacho kujuilisha nini Inayo gonga?
Na kitu gani kitacho kujuulisha hali ya AL-QAARIA'H katika kitisho chake juu ya nafsi za watu?
Tefsiri na arapskom jeziku:
يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo walio tawanyika;
Siku hiyo watu watakuwa kama vipepeo kwa wingi na kuhangaika kulia na kushoto, madhaifu na wanyonge!
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
Na milima itakuwa kama sufi iliyo tiwa rangi na kuchambuliwa kwa kutapanyika vipande mbali mbali na kupeperuka katika anga huku na huku.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
Ama yule ambaye mizani yake itakuwa nzito, mema yake yakapindukia kuliko maovu yake,
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza.
Basi huyo atakuwa na maisha yatayo mridhisha mwenyewe, na nafsi yake itue.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
Na ama ambaye mizani yake itakuwa nyepesi, na maovu yake yakazidi kuliko mema yake,
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
Basi makaazi yake yatakuwa Jahannamu.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
Na nini cha kukujuulisha ni nini Hawiya?
Tefsiri na arapskom jeziku:
نَارٌ حَامِيَةُۢ
Ni Moto mkali!
Moto ulio mkali, hapana moto unao fikilia ukali wake, hata ukichochewa vipi na kutiwa kuni gani!
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: Sura el-Karia
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - علي محسن البرواني - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها علي محسن البرواني.

Zatvaranje