ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی * - لیست ترجمه ها

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

ترجمهٔ معانی سوره: سوره شرح   آیه:

Surat Ash-Sharh

أَلَمۡ نَشۡرَحۡ لَكَ صَدۡرَكَ
Hatukukunjulia kifua chako?
Hakika tumekukunjulia kifua chako kwa kuwa tulitia ndani yake Uwongofu na Imani.
تفسیرهای عربی:
وَوَضَعۡنَا عَنكَ وِزۡرَكَ
Na tukakuondolea mzigo wako!
Na tumekupunguzia mizigo iliyo kuwa mizito juu ya mgongo wako, kwa kukuunga mkono na kukusahilishia mambo yako,
تفسیرهای عربی:
ٱلَّذِيٓ أَنقَضَ ظَهۡرَكَ
Ulio vunja mgongo wako?
Ambayo yalikuwa ni mazito juu ya mgongo wako.
تفسیرهای عربی:
وَرَفَعۡنَا لَكَ ذِكۡرَكَ
Na tukakunyanyulia utajo wako?
Na tumelitukuza jina lako, tukalifanya linatajwa na ulimi wa kila Muumini pamoja na jina letu.
تفسیرهای عربی:
فَإِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرًا
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi!
Hizo ni baadhi ya neema zetu juu yako. Basi kuwa na yakini na uweza wa Mwenyezi Mtukufu, kwani pamoja na uzito upo wepesi mwingi unao kuja nao.
تفسیرهای عربی:
إِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرٗا
Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
Hakika pamoja na uzito (wakati huo huo ijapo kuwa wewe hujui), upo wepesi mwingi vile vile.
تفسیرهای عربی:
فَإِذَا فَرَغۡتَ فَٱنصَبۡ
Na ukipata faragha, fanya juhudi.
Basi ukipata nafasi katika kazi ya kuwalingania watu, na mambo yaliyo khusiana na Jihadi, endelea na jitihada ya ibada na jishughulishe nafsi yako katika hayo.
تفسیرهای عربی:
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرۡغَب
Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.
Kwa Mola wako Mlezi tu ndio uelekee kwa kumwomba na kumhitajia.
تفسیرهای عربی:
 
ترجمهٔ معانی سوره: سوره شرح
فهرست سوره ها شماره صفحه
 
ترجمهٔ معانی قرآن کریم - ترجمهٔ سواحلی ـ علی محسن البروانی - لیست ترجمه ها

ترجمهٔ معانی قرآن کریم به زبان سواحلی ـ ترجمهٔ علی محسن البروانی.

بستن