Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis * - Indice Traduzioni


Traduzione dei significati Sura: Al-A‘lâ   Versetto:

Surat Al-A'la

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى
Takasa Jina la Mola wako Aliyetukuka na kuepukana na mshirika na kila sifa pungufu kwa namna inayonasibiana na utukufu Wake na utakatifu Wake.
Esegesi in lingua araba:
ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Aliyeumba viumbe Akalitengeneza umbo lao na kulifanya zuri.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Na Aliyekadiria kila kitu na kukipeleka njia inayonasibiana nacho.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ
Na Aliyeotesha nyasi mbiti zenye rangi ya kijani,
Esegesi in lingua araba:
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ
Akazifanya baadaye kuwa kavu zilizobadilika rangi.
Esegesi in lingua araba:
سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Tutakusomea, ewe Mtume, hii Qur’ani kisomo ambacho hutakisahau.
Esegesi in lingua araba:
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ
Isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Ataka usahau kwa hekima na maslahi anayoyajua Yeye. Kwani Yeye ni Mjuzi wa yaliyo wazi na yaliyofichika, ya maneno na ya vitendo.
Esegesi in lingua araba:
وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutakufanyia mapesi mambo yako yote; miongoni mwayo ni kukusahilishia kubeba majukumu ya utume na kuifanya nyepesi Dini uliyokuja nayo.
Esegesi in lingua araba:
فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ
Basi wawaidhie kaumu zako, ewe Mtume, kwa namna tulivyokutayarishia ufanye kwenye wahyi ulioletewa, uwaongoze njia yenye kheri na wao na uwahusu kwa mawaidha yako wale wanaotarajiwa kuwaidhika nayo. Wala usijisumbue kuwashauri wale ambao mawidha hayawaathiri isipokuwa kuwatia ujeuri na kuwafanya wayakimbie.
Esegesi in lingua araba:
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ
Atanufaika kwa mawaidha anayemcha Mola wke,
Esegesi in lingua araba:
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى
na atajiepusha na mawaidha aliye mbaya asiyemuogopa Mola wake
Esegesi in lingua araba:
ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
atakayeingia kwenye Moto wa Jahanamu akiadhibika kwa ukali wake.
Esegesi in lingua araba:
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ
Kisha hatakuwa ni mwenye kufa akapumzika wala ni mwenye kuishi akanufaika.
Esegesi in lingua araba:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake na tabia mbovu,
Esegesi in lingua araba:
وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
na akamtaja Mwenyezi Mungu, akampwekesha, akamuomba, akafanya vitendo vya kumridhisha na akasimamisha Swala kwa nyakati zake kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kufuata sheria Aliyoiweka.
Esegesi in lingua araba:
بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Hakika yenu, nyinyi watu, mnafadhilisha pambo la maisha ya kilimwengu juu ya starehe za Akhera.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ
Na hakika ya mambo ni kuwa nyumba ya Akhera na starehe zake ni bora zaidi kuliko ulimwngu na ni yenye kusalia zaidi.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ
Haya mlioosimuliwa ndani ya Sura hii ni miongoni mwa yaliyotajwa kimaana katika Kurasa zilizotangulia kuteremshwa kabla ya Qur’ani.
Esegesi in lingua araba:
صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Nazo ni Kurasa za Ibrāhīm na Mūsā, amani ziwashukie.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Sura: Al-A‘lâ
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Abdullah Mohammed e Nasser Khamis - Indice Traduzioni

Traduzione dei significati del Nobile Corano in swahili di Abdullah Mohammed ِAbu Bakr e Shaikh Nasser Khamis

Chiudi