വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. * - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക


പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: സൂറത്തുൽ അഅ്ലാ   ആയത്ത്:

Surat Al-A'la

سَبِّحِ ٱسۡمَ رَبِّكَ ٱلۡأَعۡلَى
Takasa Jina la Mola wako Aliyetukuka na kuepukana na mshirika na kila sifa pungufu kwa namna inayonasibiana na utukufu Wake na utakatifu Wake.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱلَّذِي خَلَقَ فَسَوَّىٰ
Aliyeumba viumbe Akalitengeneza umbo lao na kulifanya zuri.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلَّذِي قَدَّرَ فَهَدَىٰ
Na Aliyekadiria kila kitu na kukipeleka njia inayonasibiana nacho.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلَّذِيٓ أَخۡرَجَ ٱلۡمَرۡعَىٰ
Na Aliyeotesha nyasi mbiti zenye rangi ya kijani,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَجَعَلَهُۥ غُثَآءً أَحۡوَىٰ
Akazifanya baadaye kuwa kavu zilizobadilika rangi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سَنُقۡرِئُكَ فَلَا تَنسَىٰٓ
Tutakusomea, ewe Mtume, hii Qur’ani kisomo ambacho hutakisahau.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِلَّا مَا شَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ يَعۡلَمُ ٱلۡجَهۡرَ وَمَا يَخۡفَىٰ
Isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Ataka usahau kwa hekima na maslahi anayoyajua Yeye. Kwani Yeye ni Mjuzi wa yaliyo wazi na yaliyofichika, ya maneno na ya vitendo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَنُيَسِّرُكَ لِلۡيُسۡرَىٰ
Tutakufanyia mapesi mambo yako yote; miongoni mwayo ni kukusahilishia kubeba majukumu ya utume na kuifanya nyepesi Dini uliyokuja nayo.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ
Basi wawaidhie kaumu zako, ewe Mtume, kwa namna tulivyokutayarishia ufanye kwenye wahyi ulioletewa, uwaongoze njia yenye kheri na wao na uwahusu kwa mawaidha yako wale wanaotarajiwa kuwaidhika nayo. Wala usijisumbue kuwashauri wale ambao mawidha hayawaathiri isipokuwa kuwatia ujeuri na kuwafanya wayakimbie.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
سَيَذَّكَّرُ مَن يَخۡشَىٰ
Atanufaika kwa mawaidha anayemcha Mola wke,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَيَتَجَنَّبُهَا ٱلۡأَشۡقَى
na atajiepusha na mawaidha aliye mbaya asiyemuogopa Mola wake
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ٱلَّذِي يَصۡلَى ٱلنَّارَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
atakayeingia kwenye Moto wa Jahanamu akiadhibika kwa ukali wake.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
ثُمَّ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ
Kisha hatakuwa ni mwenye kufa akapumzika wala ni mwenye kuishi akanufaika.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن تَزَكَّىٰ
Hakika amefuzu mwenye kuisafisha nafsi yake na tabia mbovu,
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَذَكَرَ ٱسۡمَ رَبِّهِۦ فَصَلَّىٰ
na akamtaja Mwenyezi Mungu, akampwekesha, akamuomba, akafanya vitendo vya kumridhisha na akasimamisha Swala kwa nyakati zake kwa kutaka radhi za Mwenyezi Mungu na kufuata sheria Aliyoiweka.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
بَلۡ تُؤۡثِرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Hakika yenu, nyinyi watu, mnafadhilisha pambo la maisha ya kilimwengu juu ya starehe za Akhera.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ وَأَبۡقَىٰٓ
Na hakika ya mambo ni kuwa nyumba ya Akhera na starehe zake ni bora zaidi kuliko ulimwngu na ni yenye kusalia zaidi.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
إِنَّ هَٰذَا لَفِي ٱلصُّحُفِ ٱلۡأُولَىٰ
Haya mlioosimuliwa ndani ya Sura hii ni miongoni mwa yaliyotajwa kimaana katika Kurasa zilizotangulia kuteremshwa kabla ya Qur’ani.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
صُحُفِ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ
Nazo ni Kurasa za Ibrāhīm na Mūsā, amani ziwashukie.
അറബി ഖുർആൻ വിവരണങ്ങൾ:
 
പരിഭാഷ അദ്ധ്യായം: സൂറത്തുൽ അഅ്ലാ
സൂറത്തുകളുടെ സൂചിക പേജ് നമ്പർ
 
വിശുദ്ധ ഖുർആൻ പരിഭാഷ - സവാഹിലി വിവർത്തനം - അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് & നാസ്വിർ ഖമീസ്. - വിവർത്തനങ്ങളുടെ സൂചിക

വിശുദ്ധ ഖുർആൻ ആശയ വിവർത്തനം സവാഹിലി ഭാഷയിൽ, ഡോ. അബ്ദുല്ലാഹ് മുഹമ്മദ് അബൂബക്ർ, ശൈഖ് നാസിർ ഖമീസ് എന്നിവർ നിർവഹിച്ചത്

അടക്കുക