Check out the new design

Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Pioneer Translation Center (Ruwwad at-Tarjama) * - Indice Traduzioni


Traduzione dei significati Sura: Ash-Shu‘arâ’   Versetto:

Ash-Shu'ara

طسٓمٓ
Tw'aa Siin Miim.
Esegesi in lingua araba:
تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ
Hizi ni Aya za Kitabu kinachobainisha.
Esegesi in lingua araba:
لَعَلَّكَ بَٰخِعٞ نَّفۡسَكَ أَلَّا يَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ
Huenda ukaihiliki nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
Esegesi in lingua araba:
إِن نَّشَأۡ نُنَزِّلۡ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةٗ فَظَلَّتۡ أَعۡنَٰقُهُمۡ لَهَا خَٰضِعِينَ
Tungependa, tungeliwateremshia kutoka mbinguni Ishara zikashinda zimezinyenyekea shingo zao.
Esegesi in lingua araba:
وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن ذِكۡرٖ مِّنَ ٱلرَّحۡمَٰنِ مُحۡدَثٍ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهُ مُعۡرِضِينَ
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman (Mwingi wa rehema), isipokuwa wao huupa mgongo.
Esegesi in lingua araba:
فَقَدۡ كَذَّبُواْ فَسَيَأۡتِيهِمۡ أَنۢبَٰٓؤُاْ مَا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Kwa yakini wamekwisha kanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia habari za yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.
Esegesi in lingua araba:
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَمۡ أَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجٖ كَرِيمٍ
Je, hawakuiona ardhi, ni mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Esegesi in lingua araba:
وَإِذۡ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئۡتِ ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na Mola wako Mlezi, alipomwita Musa, akamwambia: Nenda kwa kaumu madhalimu.
Esegesi in lingua araba:
قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَۚ أَلَا يَتَّقُونَ
Kaumu wa Firauni. Kwani hawamchi Mwenyezi Mungu?
Esegesi in lingua araba:
قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi, hakika mimi ninachelea kwamba watanikadhibisha.
Esegesi in lingua araba:
وَيَضِيقُ صَدۡرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرۡسِلۡ إِلَىٰ هَٰرُونَ
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
Esegesi in lingua araba:
وَلَهُمۡ عَلَيَّ ذَنۢبٞ فَأَخَافُ أَن يَقۡتُلُونِ
Na wao wana dhambi niliyowafanyia, kwa hivyo ninahofu wanaweza kuniua.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ كَلَّاۖ فَٱذۡهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسۡتَمِعُونَ
Akasema: Sivyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
Esegesi in lingua araba:
فَأۡتِيَا فِرۡعَوۡنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Basi nendeni kwa Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
أَنۡ أَرۡسِلۡ مَعَنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Kwamba: Waachilie Wana wa Israili waende pamoja nasi.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ أَلَمۡ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدٗا وَلَبِثۡتَ فِينَا مِنۡ عُمُرِكَ سِنِينَ
(Firauni) akasema: Je, sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa miongoni mwetu katika umri wako miaka mingi?
Esegesi in lingua araba:
وَفَعَلۡتَ فَعۡلَتَكَ ٱلَّتِي فَعَلۡتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na ukatenda kitendo chako ulichotenda, nawe ukawa miongoni mwa wenye kukufuru?
Esegesi in lingua araba:
قَالَ فَعَلۡتُهَآ إِذٗا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipokuwa miongoni mwa wale waliopotea.
Esegesi in lingua araba:
فَفَرَرۡتُ مِنكُمۡ لَمَّا خِفۡتُكُمۡ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكۡمٗا وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Basi nikawakimbia nilipowahofu, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
Esegesi in lingua araba:
وَتِلۡكَ نِعۡمَةٞ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنۡ عَبَّدتَّ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
Esegesi in lingua araba:
قَالَ فِرۡعَوۡنُ وَمَا رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Firauni akasema: Na ni nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
Esegesi in lingua araba:
قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ لِمَنۡ حَوۡلَهُۥٓ أَلَا تَسۡتَمِعُونَ
(Firauni) akawaambia waliomzunguka: Kwani hamsikilizi?
Esegesi in lingua araba:
قَالَ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِيٓ أُرۡسِلَ إِلَيۡكُمۡ لَمَجۡنُونٞ
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliyetumwa kwenu ni mwendawazimu.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡقِلُونَ
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذۡتَ إِلَٰهًا غَيۡرِي لَأَجۡعَلَنَّكَ مِنَ ٱلۡمَسۡجُونِينَ
(Firauni) akasema: Ukijifanyia mungu mwengine asiyekuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ أَوَلَوۡ جِئۡتُكَ بِشَيۡءٖ مُّبِينٖ
Akasema: Je, hata kama nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
Esegesi in lingua araba:
قَالَ فَأۡتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wakweli.
Esegesi in lingua araba:
فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhahiri.
Esegesi in lingua araba:
وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّٰظِرِينَ
Na akautoa nje mkono wake, mara ukawa mweupe kwa watazamao.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ لِلۡمَلَإِ حَوۡلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ
(Firauni) akawaambia waheshimiwa waliomzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
Esegesi in lingua araba:
يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُم بِسِحۡرِهِۦ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ
Anataka kuwatoa katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
Esegesi in lingua araba:
قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَٱبۡعَثۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Wakasema: Mpe muda yeye na kakaye na uwatume mijini wakusanyao watu.
Esegesi in lingua araba:
يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٖ
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
Esegesi in lingua araba:
فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Basi wakakusanywa wachawi kwa ajili ya miadi ya siku maalumu.
Esegesi in lingua araba:
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلۡ أَنتُم مُّجۡتَمِعُونَ
Na watu wakaambiwa: Je, mtakusanyika?
Esegesi in lingua araba:
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Huenda tutawafuata wachawi ikiwa wao ndio watakaoshinda.
Esegesi in lingua araba:
فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُواْ لِفِرۡعَوۡنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Basi walipokuja wachawi, wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira ikiwa sisi ndio tutakaoshinda?
Esegesi in lingua araba:
قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Akasema: Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ
Musa akwaambia: Tupeni mnavyotaka kutupa.
Esegesi in lingua araba:
فَأَلۡقَوۡاْ حِبَالَهُمۡ وَعِصِيَّهُمۡ وَقَالُواْ بِعِزَّةِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبُونَ
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
Esegesi in lingua araba:
فَأَلۡقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ
Basi Musa akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza vile walivyovizua.
Esegesi in lingua araba:
فَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ
Hapo wachawi hao walipinduka wakasujudu.
Esegesi in lingua araba:
قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ ءَامَنتُمۡ لَهُۥ قَبۡلَ أَنۡ ءَاذَنَ لَكُمۡۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِي عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحۡرَ فَلَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَرۡجُلَكُم مِّنۡ خِلَٰفٖ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمۡ أَجۡمَعِينَ
(Firauni) akasema: Je, mmemuamini kabla ya kuwaruhusu? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliyewafunza uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitawasulubisha misalabani nyote.
Esegesi in lingua araba:
قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّا نَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika sisi tunatumai kwamba Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa tumekuwa wa kwanza wa Waumini.
Esegesi in lingua araba:
۞ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَسۡرِ بِعِبَادِيٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Na tulimuamrisha Musa kwa ufunuo: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
Esegesi in lingua araba:
فَأَرۡسَلَ فِرۡعَوۡنُ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Basi Firauni akawatuma mijini wakusanyaji.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَشِرۡذِمَةٞ قَلِيلُونَ
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّهُمۡ لَنَا لَغَآئِظُونَ
Nao kwa hakika wanatuudhi.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
Esegesi in lingua araba:
فَأَخۡرَجۡنَٰهُم مِّن جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchemi.
Esegesi in lingua araba:
وَكُنُوزٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ
Na mahazina, na vyeo vya heshima,
Esegesi in lingua araba:
كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Vivyo hivyo, na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
Esegesi in lingua araba:
فَأَتۡبَعُوهُم مُّشۡرِقِينَ
Basi wakawafuata lilipochomoza jua.
Esegesi in lingua araba:
فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلۡجَمۡعَانِ قَالَ أَصۡحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدۡرَكُونَ
Na yalipoonana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumekutwa!
Esegesi in lingua araba:
قَالَ كَلَّآۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهۡدِينِ
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
Esegesi in lingua araba:
فَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡبَحۡرَۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرۡقٖ كَٱلطَّوۡدِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tulimletea Musa ufunuo tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
Esegesi in lingua araba:
وَأَزۡلَفۡنَا ثَمَّ ٱلۡأٓخَرِينَ
Na tukawasongesha hapo karibu wale wengine.
Esegesi in lingua araba:
وَأَنجَيۡنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Tukawaokoa Musa na wale waliokuwa pamoja naye wote.
Esegesi in lingua araba:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawazamisha hao wengine.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si wenye kuamini.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Esegesi in lingua araba:
وَٱتۡلُ عَلَيۡهِمۡ نَبَأَ إِبۡرَٰهِيمَ
Na wasomee habari za Ibrahim.
Esegesi in lingua araba:
إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَا تَعۡبُدُونَ
Alipomwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
Esegesi in lingua araba:
قَالُواْ نَعۡبُدُ أَصۡنَامٗا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ هَلۡ يَسۡمَعُونَكُمۡ إِذۡ تَدۡعُونَ
Akasema: Je, yanawasikia mnapoyaita?
Esegesi in lingua araba:
أَوۡ يَنفَعُونَكُمۡ أَوۡ يَضُرُّونَ
Au yanawafaa, au yanawadhuru?
Esegesi in lingua araba:
قَالُواْ بَلۡ وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفۡعَلُونَ
Wakasema: Bali tuliwakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ أَفَرَءَيۡتُم مَّا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ
Akasema: Je, mmewaona hawa mnaowaabudu?
Esegesi in lingua araba:
أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلۡأَقۡدَمُونَ
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
Esegesi in lingua araba:
فَإِنَّهُمۡ عَدُوّٞ لِّيٓ إِلَّا رَبَّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
ٱلَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهۡدِينِ
Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa
Esegesi in lingua araba:
وَٱلَّذِي هُوَ يُطۡعِمُنِي وَيَسۡقِينِ
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
Esegesi in lingua araba:
وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ
Na ninapougua, ni Yeye ndiye anayeniponesha.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحۡيِينِ
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلَّذِيٓ أَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لِي خَطِيٓـَٔتِي يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Na ambaye ndiye ninayemtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
Esegesi in lingua araba:
رَبِّ هَبۡ لِي حُكۡمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّٰلِحِينَ
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na walio wema.
Esegesi in lingua araba:
وَٱجۡعَل لِّي لِسَانَ صِدۡقٖ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na unijalie nitajwe kwa wema na watu watakaokuja baadaye.
Esegesi in lingua araba:
وَٱجۡعَلۡنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ
Na unijalie katika warithi wa Bustani za neema.
Esegesi in lingua araba:
وَٱغۡفِرۡ لِأَبِيٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
Esegesi in lingua araba:
وَلَا تُخۡزِنِي يَوۡمَ يُبۡعَثُونَ
Wala usinihizi Siku watakapofufuliwa.
Esegesi in lingua araba:
يَوۡمَ لَا يَنفَعُ مَالٞ وَلَا بَنُونَ
Siku ambayo kwamba mali haitafaa kitu wala wana.
Esegesi in lingua araba:
إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٖ سَلِيمٖ
Isipokuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
Esegesi in lingua araba:
وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ
Na Pepo itasogezwa kwa wachamungu.
Esegesi in lingua araba:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِلۡغَاوِينَ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
Esegesi in lingua araba:
وَقِيلَ لَهُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ
Na wataambiwa: Wako wapi mliokuwa mkiwaabudu
Esegesi in lingua araba:
مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلۡ يَنصُرُونَكُمۡ أَوۡ يَنتَصِرُونَ
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je, wanawasaidia, au wanajisaidia wenyewe?
Esegesi in lingua araba:
فَكُبۡكِبُواْ فِيهَا هُمۡ وَٱلۡغَاوُۥنَ
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu.
Esegesi in lingua araba:
وَجُنُودُ إِبۡلِيسَ أَجۡمَعُونَ
Na majeshi ya Ibilisi yote.
Esegesi in lingua araba:
قَالُواْ وَهُمۡ فِيهَا يَخۡتَصِمُونَ
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
Esegesi in lingua araba:
تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhahiri.
Esegesi in lingua araba:
إِذۡ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Tulipowafanya nyinyi ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلۡمُجۡرِمُونَ
Na hawakutupoteza isipokuwa wale wakosefu.
Esegesi in lingua araba:
فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ
Basi hatuna waombezi wowote.
Esegesi in lingua araba:
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٖ
Wala rafiki wa dhati.
Esegesi in lingua araba:
فَلَوۡ أَنَّ لَنَا كَرَّةٗ فَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Laiti tungelipata kurejea tena, tungelikuwa katika Waumini.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwingi wa kurehemu.
Esegesi in lingua araba:
كَذَّبَتۡ قَوۡمُ نُوحٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
Esegesi in lingua araba:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Nuhu: Je, hamumchi Mwenyezi Mungu?
Esegesi in lingua araba:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Esegesi in lingua araba:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na siwaulizi juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Esegesi in lingua araba:
۞ قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلۡأَرۡذَلُونَ
Wakasema: Je, tukuamini wewe, ilhali wanaokufuata ni watu duni?
Esegesi in lingua araba:
قَالَ وَمَا عِلۡمِي بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Akasema: Ninayajuaje waliyokuwa wakiyafanya?
Esegesi in lingua araba:
إِنۡ حِسَابُهُمۡ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّيۖ لَوۡ تَشۡعُرُونَ
Hesabu yao haiko isipokuwa kwa Mola wao Mlezi, laiti mngelitambua!
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
Esegesi in lingua araba:
إِنۡ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ
Mimi si chochote isipokuwa ni Mwonyaji wa dhahiri shahiri.
Esegesi in lingua araba:
قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمَرۡجُومِينَ
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوۡمِي كَذَّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikadhibisha.
Esegesi in lingua araba:
فَٱفۡتَحۡ بَيۡنِي وَبَيۡنَهُمۡ فَتۡحٗا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami miongoni mwa Waumini.
Esegesi in lingua araba:
فَأَنجَيۡنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِي ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na waliokuwa pamoja naye katika marikebu iliyosheheni.
Esegesi in lingua araba:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا بَعۡدُ ٱلۡبَاقِينَ
Kisha tukawazamisha baadaye waliobakia.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao waliokuwa Waumini.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Esegesi in lingua araba:
كَذَّبَتۡ عَادٌ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kina 'Aad waliwakanusha Mitume.
Esegesi in lingua araba:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Hud: Je, hamchi Mungu?
Esegesi in lingua araba:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Esegesi in lingua araba:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi juu yake ujira wowote, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
أَتَبۡنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةٗ تَعۡبَثُونَ
Je, mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
Esegesi in lingua araba:
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمۡ تَخۡلُدُونَ
Na mnajenga majengo ya kifahari kama kwamba mtaishi milele!
Esegesi in lingua araba:
وَإِذَا بَطَشۡتُم بَطَشۡتُمۡ جَبَّارِينَ
Na mnapotumia nguvu, mnatumia nguvu kwa ujabari.
Esegesi in lingua araba:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
Esegesi in lingua araba:
وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِيٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعۡلَمُونَ
Na mcheni aliyewapa haya mnayoyajua.
Esegesi in lingua araba:
أَمَدَّكُم بِأَنۡعَٰمٖ وَبَنِينَ
Aliwapa wanyama wa kufuga na wana.
Esegesi in lingua araba:
وَجَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ
Na mabustani na chemchemi.
Esegesi in lingua araba:
إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Hakika mimi ninawahofia adhabu ya Siku Kubwa.
Esegesi in lingua araba:
قَالُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡنَآ أَوَعَظۡتَ أَمۡ لَمۡ تَكُن مِّنَ ٱلۡوَٰعِظِينَ
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
Esegesi in lingua araba:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Haya si chochote isipokuwa ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
Esegesi in lingua araba:
وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ
Wala sisi hatutaadhibiwa.
Esegesi in lingua araba:
فَكَذَّبُوهُ فَأَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Wakamkadhibisha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Esegesi in lingua araba:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kina Thamud waliwakadhibisha Mitume.
Esegesi in lingua araba:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao Saleh: Je, hamumchi Mungu?
Esegesi in lingua araba:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Esegesi in lingua araba:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
أَتُتۡرَكُونَ فِي مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ
Je, mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
Esegesi in lingua araba:
فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Katika mabustani, na chemchemi?
Esegesi in lingua araba:
وَزُرُوعٖ وَنَخۡلٖ طَلۡعُهَا هَضِيمٞ
Na konde na mitende yenye makole yaliyowiva.
Esegesi in lingua araba:
وَتَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتٗا فَٰرِهِينَ
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
Esegesi in lingua araba:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Esegesi in lingua araba:
وَلَا تُطِيعُوٓاْ أَمۡرَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ
Wala msitii amri za waliopitiliza mipaka
Esegesi in lingua araba:
ٱلَّذِينَ يُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا يُصۡلِحُونَ
Ambao wanafanya uharibifu katika nchi, wala hawatengenezi.
Esegesi in lingua araba:
قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa.
Esegesi in lingua araba:
مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا فَأۡتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Wewe si chochote isipokuwa ni mtu kama sisi. Basi leta Ishara ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٞ لَّهَا شِرۡبٞ وَلَكُمۡ شِرۡبُ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
Esegesi in lingua araba:
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٖ فَيَأۡخُذَكُمۡ عَذَابُ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Wala msimguse kwa wovu, ikawashika adhabu ya Siku Kubwa.
Esegesi in lingua araba:
فَعَقَرُوهَا فَأَصۡبَحُواْ نَٰدِمِينَ
Lakini wakamuua, na wakawa wenye kujuta.
Esegesi in lingua araba:
فَأَخَذَهُمُ ٱلۡعَذَابُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Esegesi in lingua araba:
كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Watu wa Luti waliwakadhibisha Mitume.
Esegesi in lingua araba:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Luti: Je, hamumchi Mungu?
Esegesi in lingua araba:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
Esegesi in lingua araba:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini mimi.
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala mimi sikuwauliza ujira wowote juu yake; ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
أَتَأۡتُونَ ٱلذُّكۡرَانَ مِنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Je, katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
Esegesi in lingua araba:
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمۡ رَبُّكُم مِّنۡ أَزۡوَٰجِكُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٌ عَادُونَ
Na mnaacha alichowaumbia Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka!
Esegesi in lingua araba:
قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُخۡرَجِينَ
Wakasema: Ewe Luti! Usipoacha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanaotolewa mji!
Esegesi in lingua araba:
قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلۡقَالِينَ
Akasema: Hakika mimi ni katika wanaokichukia hiki kitendo chenu.
Esegesi in lingua araba:
رَبِّ نَجِّنِي وَأَهۡلِي مِمَّا يَعۡمَلُونَ
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
Esegesi in lingua araba:
فَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote.
Esegesi in lingua araba:
إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ
Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma.
Esegesi in lingua araba:
ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawaangamiza wale wengine.
Esegesi in lingua araba:
وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyoonywa.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Esegesi in lingua araba:
كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ لۡـَٔيۡكَةِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
Esegesi in lingua araba:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ شُعَيۡبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Shuaibu alipowaambia: Je, hamumchi Mungu?
Esegesi in lingua araba:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Esegesi in lingua araba:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
۞ أَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَلَا تَكُونُواْ مِنَ ٱلۡمُخۡسِرِينَ
Timizeni kipimo sawasawa, wala msiwe katika wanaopunja.
Esegesi in lingua araba:
وَزِنُواْ بِٱلۡقِسۡطَاسِ ٱلۡمُسۡتَقِيمِ
Na pimeni kwa haki iliyonyooka.
Esegesi in lingua araba:
وَلَا تَبۡخَسُواْ ٱلنَّاسَ أَشۡيَآءَهُمۡ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri katika ardhi kwa kufanya uharibifu.
Esegesi in lingua araba:
وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ وَٱلۡجِبِلَّةَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na mcheni aliyewaumba nyinyi na vizazi vilivyotangulia.
Esegesi in lingua araba:
قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ
Wakasema: Hakika wewe ni katika waliorogwa.
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلۡكَٰذِبِينَ
Na wewe si chochote isipokuwa ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
Esegesi in lingua araba:
فَأَسۡقِطۡ عَلَيۡنَا كِسَفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
Esegesi in lingua araba:
قَالَ رَبِّيٓ أَعۡلَمُ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayoyatenda.
Esegesi in lingua araba:
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمۡ عَذَابُ يَوۡمِ ٱلظُّلَّةِۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٍ
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya Siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya Siku kubwa.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Esegesi in lingua araba:
نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلۡأَمِينُ
Ameuteremsha Roho muaminifu.
Esegesi in lingua araba:
عَلَىٰ قَلۡبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُنذِرِينَ
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji.
Esegesi in lingua araba:
بِلِسَانٍ عَرَبِيّٖ مُّبِينٖ
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
Esegesi in lingua araba:
وَإِنَّهُۥ لَفِي زُبُرِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
Esegesi in lingua araba:
أَوَلَمۡ يَكُن لَّهُمۡ ءَايَةً أَن يَعۡلَمَهُۥ عُلَمَٰٓؤُاْ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Je, haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanauchoni wa Wana wa Israili?
Esegesi in lingua araba:
وَلَوۡ نَزَّلۡنَٰهُ عَلَىٰ بَعۡضِ ٱلۡأَعۡجَمِينَ
Na lau kuwa tungeliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa Waarabu.
Esegesi in lingua araba:
فَقَرَأَهُۥ عَلَيۡهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ مُؤۡمِنِينَ
Na akawasomea, wasingelikuwa wenye kuamini.
Esegesi in lingua araba:
كَذَٰلِكَ سَلَكۡنَٰهُ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wahalifu.
Esegesi in lingua araba:
لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُاْ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
Esegesi in lingua araba:
فَيَأۡتِيَهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana habari.
Esegesi in lingua araba:
فَيَقُولُواْ هَلۡ نَحۡنُ مُنظَرُونَ
Na watasema: Je, tutapewa muhula?
Esegesi in lingua araba:
أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ
Basi je, wanaihimiza adhabu yetu?
Esegesi in lingua araba:
أَفَرَءَيۡتَ إِن مَّتَّعۡنَٰهُمۡ سِنِينَ
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka.
Esegesi in lingua araba:
ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُواْ يُوعَدُونَ
Kisha yakawafikia waliyokuwa wakiahidiwa.
Esegesi in lingua araba:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يُمَتَّعُونَ
Yatawafaa nini yale waliyostareheshewa?
Esegesi in lingua araba:
وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
Wala hatukuangamiza mji wowote isipokuwa ulikuwa na waonyaji.
Esegesi in lingua araba:
ذِكۡرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
Esegesi in lingua araba:
وَمَا تَنَزَّلَتۡ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ
Wala Mashetani hawakuteremka nayo.
Esegesi in lingua araba:
وَمَا يَنۢبَغِي لَهُمۡ وَمَا يَسۡتَطِيعُونَ
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّهُمۡ عَنِ ٱلسَّمۡعِ لَمَعۡزُولُونَ
Hakika hao wametengwa na kusikia.
Esegesi in lingua araba:
فَلَا تَدۡعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُعَذَّبِينَ
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakaoadhibiwa.
Esegesi in lingua araba:
وَأَنذِرۡ عَشِيرَتَكَ ٱلۡأَقۡرَبِينَ
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
Esegesi in lingua araba:
وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na watwae kwa upole wanaokufuata miongoni mwa Waumini.
Esegesi in lingua araba:
فَإِنۡ عَصَوۡكَ فَقُلۡ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تَعۡمَلُونَ
Na ikiwa watakuasi, basi sema: Mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyatenda.
Esegesi in lingua araba:
وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Esegesi in lingua araba:
ٱلَّذِي يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ
Ambaye anakuona unaposimama.
Esegesi in lingua araba:
وَتَقَلُّبَكَ فِي ٱلسَّٰجِدِينَ
Na mageuko yako kati ya wanaosujudu.
Esegesi in lingua araba:
إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua zaidi.
Esegesi in lingua araba:
هَلۡ أُنَبِّئُكُمۡ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَٰطِينُ
Je, niwaambieni nani wanawashukia Mashetani?
Esegesi in lingua araba:
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٖ
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
Esegesi in lingua araba:
يُلۡقُونَ ٱلسَّمۡعَ وَأَكۡثَرُهُمۡ كَٰذِبُونَ
Wanawapelekea yale wanayoyasikia; na wengi wao ni waongo.
Esegesi in lingua araba:
وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلۡغَاوُۥنَ
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
Esegesi in lingua araba:
أَلَمۡ تَرَ أَنَّهُمۡ فِي كُلِّ وَادٖ يَهِيمُونَ
Je, huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
Esegesi in lingua araba:
وَأَنَّهُمۡ يَقُولُونَ مَا لَا يَفۡعَلُونَ
Na kwamba wao husema wasiyoyatenda?
Esegesi in lingua araba:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَذَكَرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا وَٱنتَصَرُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا ظُلِمُواْۗ وَسَيَعۡلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ أَيَّ مُنقَلَبٖ يَنقَلِبُونَ
Isipokuwa wale walioamini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapodhulumiwa. Na wanaodhulumu watakuja jua mgeuko gani watakaogeuka.
Esegesi in lingua araba:
 
Traduzione dei significati Sura: Ash-Shu‘arâ’
Indice delle Sure Numero di pagina
 
Traduzione dei Significati del Sacro Corano - Traduzione swahili - Pioneer Translation Center (Ruwwad at-Tarjama) - Indice Traduzioni

Tradotta dal team del centro di traduzione "Pioneers" in collaborazione con "Association for call and awareness of communities" di al-Rabwah e "Association for Service of Islamic Content in Languages".

Chiudi