Check out the new design

แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - ศูนย์การแปลรุว๊าด * - สารบัญ​คำแปล


แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Ash-Shu‘arā’   อายะฮ์:

Ash-Shu'ara

طسٓمٓ
Tw'aa Siin Miim.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ
Hizi ni Aya za Kitabu kinachobainisha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَعَلَّكَ بَٰخِعٞ نَّفۡسَكَ أَلَّا يَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ
Huenda ukaihiliki nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِن نَّشَأۡ نُنَزِّلۡ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةٗ فَظَلَّتۡ أَعۡنَٰقُهُمۡ لَهَا خَٰضِعِينَ
Tungependa, tungeliwateremshia kutoka mbinguni Ishara zikashinda zimezinyenyekea shingo zao.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن ذِكۡرٖ مِّنَ ٱلرَّحۡمَٰنِ مُحۡدَثٍ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهُ مُعۡرِضِينَ
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman (Mwingi wa rehema), isipokuwa wao huupa mgongo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَقَدۡ كَذَّبُواْ فَسَيَأۡتِيهِمۡ أَنۢبَٰٓؤُاْ مَا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Kwa yakini wamekwisha kanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia habari za yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَمۡ أَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجٖ كَرِيمٍ
Je, hawakuiona ardhi, ni mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِذۡ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئۡتِ ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na Mola wako Mlezi, alipomwita Musa, akamwambia: Nenda kwa kaumu madhalimu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَۚ أَلَا يَتَّقُونَ
Kaumu wa Firauni. Kwani hawamchi Mwenyezi Mungu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi, hakika mimi ninachelea kwamba watanikadhibisha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَيَضِيقُ صَدۡرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرۡسِلۡ إِلَىٰ هَٰرُونَ
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَهُمۡ عَلَيَّ ذَنۢبٞ فَأَخَافُ أَن يَقۡتُلُونِ
Na wao wana dhambi niliyowafanyia, kwa hivyo ninahofu wanaweza kuniua.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ كَلَّاۖ فَٱذۡهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسۡتَمِعُونَ
Akasema: Sivyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأۡتِيَا فِرۡعَوۡنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Basi nendeni kwa Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَنۡ أَرۡسِلۡ مَعَنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Kwamba: Waachilie Wana wa Israili waende pamoja nasi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ أَلَمۡ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدٗا وَلَبِثۡتَ فِينَا مِنۡ عُمُرِكَ سِنِينَ
(Firauni) akasema: Je, sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa miongoni mwetu katika umri wako miaka mingi?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَفَعَلۡتَ فَعۡلَتَكَ ٱلَّتِي فَعَلۡتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na ukatenda kitendo chako ulichotenda, nawe ukawa miongoni mwa wenye kukufuru?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ فَعَلۡتُهَآ إِذٗا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipokuwa miongoni mwa wale waliopotea.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَفَرَرۡتُ مِنكُمۡ لَمَّا خِفۡتُكُمۡ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكۡمٗا وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Basi nikawakimbia nilipowahofu, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَتِلۡكَ نِعۡمَةٞ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنۡ عَبَّدتَّ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ فِرۡعَوۡنُ وَمَا رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Firauni akasema: Na ni nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ لِمَنۡ حَوۡلَهُۥٓ أَلَا تَسۡتَمِعُونَ
(Firauni) akawaambia waliomzunguka: Kwani hamsikilizi?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِيٓ أُرۡسِلَ إِلَيۡكُمۡ لَمَجۡنُونٞ
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliyetumwa kwenu ni mwendawazimu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡقِلُونَ
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذۡتَ إِلَٰهًا غَيۡرِي لَأَجۡعَلَنَّكَ مِنَ ٱلۡمَسۡجُونِينَ
(Firauni) akasema: Ukijifanyia mungu mwengine asiyekuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ أَوَلَوۡ جِئۡتُكَ بِشَيۡءٖ مُّبِينٖ
Akasema: Je, hata kama nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ فَأۡتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wakweli.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhahiri.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّٰظِرِينَ
Na akautoa nje mkono wake, mara ukawa mweupe kwa watazamao.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ لِلۡمَلَإِ حَوۡلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ
(Firauni) akawaambia waheshimiwa waliomzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُم بِسِحۡرِهِۦ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ
Anataka kuwatoa katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَٱبۡعَثۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Wakasema: Mpe muda yeye na kakaye na uwatume mijini wakusanyao watu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٖ
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Basi wakakusanywa wachawi kwa ajili ya miadi ya siku maalumu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلۡ أَنتُم مُّجۡتَمِعُونَ
Na watu wakaambiwa: Je, mtakusanyika?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Huenda tutawafuata wachawi ikiwa wao ndio watakaoshinda.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُواْ لِفِرۡعَوۡنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Basi walipokuja wachawi, wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira ikiwa sisi ndio tutakaoshinda?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Akasema: Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ
Musa akwaambia: Tupeni mnavyotaka kutupa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَلۡقَوۡاْ حِبَالَهُمۡ وَعِصِيَّهُمۡ وَقَالُواْ بِعِزَّةِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبُونَ
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَلۡقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ
Basi Musa akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza vile walivyovizua.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ
Hapo wachawi hao walipinduka wakasujudu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ ءَامَنتُمۡ لَهُۥ قَبۡلَ أَنۡ ءَاذَنَ لَكُمۡۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِي عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحۡرَ فَلَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَرۡجُلَكُم مِّنۡ خِلَٰفٖ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمۡ أَجۡمَعِينَ
(Firauni) akasema: Je, mmemuamini kabla ya kuwaruhusu? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliyewafunza uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitawasulubisha misalabani nyote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّا نَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika sisi tunatumai kwamba Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa tumekuwa wa kwanza wa Waumini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
۞ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَسۡرِ بِعِبَادِيٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Na tulimuamrisha Musa kwa ufunuo: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَرۡسَلَ فِرۡعَوۡنُ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Basi Firauni akawatuma mijini wakusanyaji.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَشِرۡذِمَةٞ قَلِيلُونَ
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّهُمۡ لَنَا لَغَآئِظُونَ
Nao kwa hakika wanatuudhi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَخۡرَجۡنَٰهُم مِّن جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchemi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَكُنُوزٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ
Na mahazina, na vyeo vya heshima,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Vivyo hivyo, na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَتۡبَعُوهُم مُّشۡرِقِينَ
Basi wakawafuata lilipochomoza jua.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلۡجَمۡعَانِ قَالَ أَصۡحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدۡرَكُونَ
Na yalipoonana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumekutwa!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ كَلَّآۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهۡدِينِ
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡبَحۡرَۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرۡقٖ كَٱلطَّوۡدِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tulimletea Musa ufunuo tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَزۡلَفۡنَا ثَمَّ ٱلۡأٓخَرِينَ
Na tukawasongesha hapo karibu wale wengine.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَنجَيۡنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Tukawaokoa Musa na wale waliokuwa pamoja naye wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawazamisha hao wengine.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si wenye kuamini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱتۡلُ عَلَيۡهِمۡ نَبَأَ إِبۡرَٰهِيمَ
Na wasomee habari za Ibrahim.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَا تَعۡبُدُونَ
Alipomwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ نَعۡبُدُ أَصۡنَامٗا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ هَلۡ يَسۡمَعُونَكُمۡ إِذۡ تَدۡعُونَ
Akasema: Je, yanawasikia mnapoyaita?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَوۡ يَنفَعُونَكُمۡ أَوۡ يَضُرُّونَ
Au yanawafaa, au yanawadhuru?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ بَلۡ وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفۡعَلُونَ
Wakasema: Bali tuliwakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ أَفَرَءَيۡتُم مَّا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ
Akasema: Je, mmewaona hawa mnaowaabudu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلۡأَقۡدَمُونَ
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَإِنَّهُمۡ عَدُوّٞ لِّيٓ إِلَّا رَبَّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ٱلَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهۡدِينِ
Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلَّذِي هُوَ يُطۡعِمُنِي وَيَسۡقِينِ
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ
Na ninapougua, ni Yeye ndiye anayeniponesha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحۡيِينِ
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلَّذِيٓ أَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لِي خَطِيٓـَٔتِي يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Na ambaye ndiye ninayemtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
رَبِّ هَبۡ لِي حُكۡمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّٰلِحِينَ
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na walio wema.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱجۡعَل لِّي لِسَانَ صِدۡقٖ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na unijalie nitajwe kwa wema na watu watakaokuja baadaye.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱجۡعَلۡنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ
Na unijalie katika warithi wa Bustani za neema.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱغۡفِرۡ لِأَبِيٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَا تُخۡزِنِي يَوۡمَ يُبۡعَثُونَ
Wala usinihizi Siku watakapofufuliwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
يَوۡمَ لَا يَنفَعُ مَالٞ وَلَا بَنُونَ
Siku ambayo kwamba mali haitafaa kitu wala wana.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٖ سَلِيمٖ
Isipokuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ
Na Pepo itasogezwa kwa wachamungu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِلۡغَاوِينَ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَقِيلَ لَهُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ
Na wataambiwa: Wako wapi mliokuwa mkiwaabudu
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلۡ يَنصُرُونَكُمۡ أَوۡ يَنتَصِرُونَ
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je, wanawasaidia, au wanajisaidia wenyewe?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَكُبۡكِبُواْ فِيهَا هُمۡ وَٱلۡغَاوُۥنَ
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَجُنُودُ إِبۡلِيسَ أَجۡمَعُونَ
Na majeshi ya Ibilisi yote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ وَهُمۡ فِيهَا يَخۡتَصِمُونَ
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhahiri.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِذۡ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Tulipowafanya nyinyi ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلۡمُجۡرِمُونَ
Na hawakutupoteza isipokuwa wale wakosefu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ
Basi hatuna waombezi wowote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٖ
Wala rafiki wa dhati.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَلَوۡ أَنَّ لَنَا كَرَّةٗ فَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Laiti tungelipata kurejea tena, tungelikuwa katika Waumini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَذَّبَتۡ قَوۡمُ نُوحٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Nuhu: Je, hamumchi Mwenyezi Mungu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na siwaulizi juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
۞ قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلۡأَرۡذَلُونَ
Wakasema: Je, tukuamini wewe, ilhali wanaokufuata ni watu duni?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ وَمَا عِلۡمِي بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Akasema: Ninayajuaje waliyokuwa wakiyafanya?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنۡ حِسَابُهُمۡ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّيۖ لَوۡ تَشۡعُرُونَ
Hesabu yao haiko isipokuwa kwa Mola wao Mlezi, laiti mngelitambua!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنۡ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ
Mimi si chochote isipokuwa ni Mwonyaji wa dhahiri shahiri.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمَرۡجُومِينَ
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوۡمِي كَذَّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikadhibisha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱفۡتَحۡ بَيۡنِي وَبَيۡنَهُمۡ فَتۡحٗا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami miongoni mwa Waumini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَنجَيۡنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِي ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na waliokuwa pamoja naye katika marikebu iliyosheheni.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا بَعۡدُ ٱلۡبَاقِينَ
Kisha tukawazamisha baadaye waliobakia.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao waliokuwa Waumini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَذَّبَتۡ عَادٌ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kina 'Aad waliwakanusha Mitume.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Hud: Je, hamchi Mungu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi juu yake ujira wowote, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَتَبۡنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةٗ تَعۡبَثُونَ
Je, mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمۡ تَخۡلُدُونَ
Na mnajenga majengo ya kifahari kama kwamba mtaishi milele!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِذَا بَطَشۡتُم بَطَشۡتُمۡ جَبَّارِينَ
Na mnapotumia nguvu, mnatumia nguvu kwa ujabari.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِيٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعۡلَمُونَ
Na mcheni aliyewapa haya mnayoyajua.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَمَدَّكُم بِأَنۡعَٰمٖ وَبَنِينَ
Aliwapa wanyama wa kufuga na wana.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَجَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ
Na mabustani na chemchemi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Hakika mimi ninawahofia adhabu ya Siku Kubwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡنَآ أَوَعَظۡتَ أَمۡ لَمۡ تَكُن مِّنَ ٱلۡوَٰعِظِينَ
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Haya si chochote isipokuwa ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ
Wala sisi hatutaadhibiwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَكَذَّبُوهُ فَأَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Wakamkadhibisha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kina Thamud waliwakadhibisha Mitume.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao Saleh: Je, hamumchi Mungu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَتُتۡرَكُونَ فِي مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ
Je, mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Katika mabustani, na chemchemi?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَزُرُوعٖ وَنَخۡلٖ طَلۡعُهَا هَضِيمٞ
Na konde na mitende yenye makole yaliyowiva.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَتَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتٗا فَٰرِهِينَ
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَا تُطِيعُوٓاْ أَمۡرَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ
Wala msitii amri za waliopitiliza mipaka
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ٱلَّذِينَ يُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا يُصۡلِحُونَ
Ambao wanafanya uharibifu katika nchi, wala hawatengenezi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا فَأۡتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Wewe si chochote isipokuwa ni mtu kama sisi. Basi leta Ishara ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٞ لَّهَا شِرۡبٞ وَلَكُمۡ شِرۡبُ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٖ فَيَأۡخُذَكُمۡ عَذَابُ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Wala msimguse kwa wovu, ikawashika adhabu ya Siku Kubwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَعَقَرُوهَا فَأَصۡبَحُواْ نَٰدِمِينَ
Lakini wakamuua, na wakawa wenye kujuta.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَخَذَهُمُ ٱلۡعَذَابُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Watu wa Luti waliwakadhibisha Mitume.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Luti: Je, hamumchi Mungu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini mimi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala mimi sikuwauliza ujira wowote juu yake; ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَتَأۡتُونَ ٱلذُّكۡرَانَ مِنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Je, katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمۡ رَبُّكُم مِّنۡ أَزۡوَٰجِكُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٌ عَادُونَ
Na mnaacha alichowaumbia Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُخۡرَجِينَ
Wakasema: Ewe Luti! Usipoacha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanaotolewa mji!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلۡقَالِينَ
Akasema: Hakika mimi ni katika wanaokichukia hiki kitendo chenu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
رَبِّ نَجِّنِي وَأَهۡلِي مِمَّا يَعۡمَلُونَ
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ
Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawaangamiza wale wengine.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyoonywa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ لۡـَٔيۡكَةِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ شُعَيۡبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Shuaibu alipowaambia: Je, hamumchi Mungu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
۞ أَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَلَا تَكُونُواْ مِنَ ٱلۡمُخۡسِرِينَ
Timizeni kipimo sawasawa, wala msiwe katika wanaopunja.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَزِنُواْ بِٱلۡقِسۡطَاسِ ٱلۡمُسۡتَقِيمِ
Na pimeni kwa haki iliyonyooka.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَا تَبۡخَسُواْ ٱلنَّاسَ أَشۡيَآءَهُمۡ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri katika ardhi kwa kufanya uharibifu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ وَٱلۡجِبِلَّةَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na mcheni aliyewaumba nyinyi na vizazi vilivyotangulia.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ
Wakasema: Hakika wewe ni katika waliorogwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلۡكَٰذِبِينَ
Na wewe si chochote isipokuwa ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَسۡقِطۡ عَلَيۡنَا كِسَفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ رَبِّيٓ أَعۡلَمُ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayoyatenda.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمۡ عَذَابُ يَوۡمِ ٱلظُّلَّةِۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٍ
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya Siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya Siku kubwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلۡأَمِينُ
Ameuteremsha Roho muaminifu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
عَلَىٰ قَلۡبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُنذِرِينَ
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
بِلِسَانٍ عَرَبِيّٖ مُّبِينٖ
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّهُۥ لَفِي زُبُرِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَوَلَمۡ يَكُن لَّهُمۡ ءَايَةً أَن يَعۡلَمَهُۥ عُلَمَٰٓؤُاْ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Je, haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanauchoni wa Wana wa Israili?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَوۡ نَزَّلۡنَٰهُ عَلَىٰ بَعۡضِ ٱلۡأَعۡجَمِينَ
Na lau kuwa tungeliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa Waarabu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَقَرَأَهُۥ عَلَيۡهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ مُؤۡمِنِينَ
Na akawasomea, wasingelikuwa wenye kuamini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَذَٰلِكَ سَلَكۡنَٰهُ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wahalifu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُاْ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَيَأۡتِيَهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana habari.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَيَقُولُواْ هَلۡ نَحۡنُ مُنظَرُونَ
Na watasema: Je, tutapewa muhula?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ
Basi je, wanaihimiza adhabu yetu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَفَرَءَيۡتَ إِن مَّتَّعۡنَٰهُمۡ سِنِينَ
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُواْ يُوعَدُونَ
Kisha yakawafikia waliyokuwa wakiahidiwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يُمَتَّعُونَ
Yatawafaa nini yale waliyostareheshewa?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
Wala hatukuangamiza mji wowote isipokuwa ulikuwa na waonyaji.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ذِكۡرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَا تَنَزَّلَتۡ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ
Wala Mashetani hawakuteremka nayo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَا يَنۢبَغِي لَهُمۡ وَمَا يَسۡتَطِيعُونَ
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّهُمۡ عَنِ ٱلسَّمۡعِ لَمَعۡزُولُونَ
Hakika hao wametengwa na kusikia.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَلَا تَدۡعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُعَذَّبِينَ
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakaoadhibiwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَنذِرۡ عَشِيرَتَكَ ٱلۡأَقۡرَبِينَ
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na watwae kwa upole wanaokufuata miongoni mwa Waumini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَإِنۡ عَصَوۡكَ فَقُلۡ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تَعۡمَلُونَ
Na ikiwa watakuasi, basi sema: Mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyatenda.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ٱلَّذِي يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ
Ambaye anakuona unaposimama.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَتَقَلُّبَكَ فِي ٱلسَّٰجِدِينَ
Na mageuko yako kati ya wanaosujudu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua zaidi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
هَلۡ أُنَبِّئُكُمۡ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَٰطِينُ
Je, niwaambieni nani wanawashukia Mashetani?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٖ
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
يُلۡقُونَ ٱلسَّمۡعَ وَأَكۡثَرُهُمۡ كَٰذِبُونَ
Wanawapelekea yale wanayoyasikia; na wengi wao ni waongo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلۡغَاوُۥنَ
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
أَلَمۡ تَرَ أَنَّهُمۡ فِي كُلِّ وَادٖ يَهِيمُونَ
Je, huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَنَّهُمۡ يَقُولُونَ مَا لَا يَفۡعَلُونَ
Na kwamba wao husema wasiyoyatenda?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَذَكَرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا وَٱنتَصَرُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا ظُلِمُواْۗ وَسَيَعۡلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ أَيَّ مُنقَلَبٖ يَنقَلِبُونَ
Isipokuwa wale walioamini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapodhulumiwa. Na wanaodhulumu watakuja jua mgeuko gani watakaogeuka.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Ash-Shu‘arā’
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - ศูนย์การแปลรุว๊าด - สารบัญ​คำแปล

แปลโดยทีมงานศูนย์แปลรุว๊าด ร่วมกับสมาคมการเผยแพร่ศาสนาอิสลามที่รอบวะฮ์ และสมาคมบริการเนื้อหาอิสลามด้วยภาษาต่าง ๆ

ปิด