Check out the new design

Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Centro de tradução Rawad * - Índice de tradução


Tradução dos significados Surah: Ash-Shu'araa   Versículo:

Ash-Shu'ara

طسٓمٓ
Tw'aa Siin Miim.
Os Tafssir em língua árabe:
تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ
Hizi ni Aya za Kitabu kinachobainisha.
Os Tafssir em língua árabe:
لَعَلَّكَ بَٰخِعٞ نَّفۡسَكَ أَلَّا يَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ
Huenda ukaihiliki nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
Os Tafssir em língua árabe:
إِن نَّشَأۡ نُنَزِّلۡ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةٗ فَظَلَّتۡ أَعۡنَٰقُهُمۡ لَهَا خَٰضِعِينَ
Tungependa, tungeliwateremshia kutoka mbinguni Ishara zikashinda zimezinyenyekea shingo zao.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن ذِكۡرٖ مِّنَ ٱلرَّحۡمَٰنِ مُحۡدَثٍ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهُ مُعۡرِضِينَ
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman (Mwingi wa rehema), isipokuwa wao huupa mgongo.
Os Tafssir em língua árabe:
فَقَدۡ كَذَّبُواْ فَسَيَأۡتِيهِمۡ أَنۢبَٰٓؤُاْ مَا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Kwa yakini wamekwisha kanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia habari za yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.
Os Tafssir em língua árabe:
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَمۡ أَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجٖ كَرِيمٍ
Je, hawakuiona ardhi, ni mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِذۡ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئۡتِ ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na Mola wako Mlezi, alipomwita Musa, akamwambia: Nenda kwa kaumu madhalimu.
Os Tafssir em língua árabe:
قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَۚ أَلَا يَتَّقُونَ
Kaumu wa Firauni. Kwani hawamchi Mwenyezi Mungu?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi, hakika mimi ninachelea kwamba watanikadhibisha.
Os Tafssir em língua árabe:
وَيَضِيقُ صَدۡرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرۡسِلۡ إِلَىٰ هَٰرُونَ
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَهُمۡ عَلَيَّ ذَنۢبٞ فَأَخَافُ أَن يَقۡتُلُونِ
Na wao wana dhambi niliyowafanyia, kwa hivyo ninahofu wanaweza kuniua.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ كَلَّاۖ فَٱذۡهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسۡتَمِعُونَ
Akasema: Sivyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأۡتِيَا فِرۡعَوۡنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Basi nendeni kwa Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
أَنۡ أَرۡسِلۡ مَعَنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Kwamba: Waachilie Wana wa Israili waende pamoja nasi.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ أَلَمۡ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدٗا وَلَبِثۡتَ فِينَا مِنۡ عُمُرِكَ سِنِينَ
(Firauni) akasema: Je, sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa miongoni mwetu katika umri wako miaka mingi?
Os Tafssir em língua árabe:
وَفَعَلۡتَ فَعۡلَتَكَ ٱلَّتِي فَعَلۡتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na ukatenda kitendo chako ulichotenda, nawe ukawa miongoni mwa wenye kukufuru?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ فَعَلۡتُهَآ إِذٗا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipokuwa miongoni mwa wale waliopotea.
Os Tafssir em língua árabe:
فَفَرَرۡتُ مِنكُمۡ لَمَّا خِفۡتُكُمۡ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكۡمٗا وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Basi nikawakimbia nilipowahofu, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
Os Tafssir em língua árabe:
وَتِلۡكَ نِعۡمَةٞ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنۡ عَبَّدتَّ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ فِرۡعَوۡنُ وَمَا رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Firauni akasema: Na ni nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ لِمَنۡ حَوۡلَهُۥٓ أَلَا تَسۡتَمِعُونَ
(Firauni) akawaambia waliomzunguka: Kwani hamsikilizi?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِيٓ أُرۡسِلَ إِلَيۡكُمۡ لَمَجۡنُونٞ
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliyetumwa kwenu ni mwendawazimu.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡقِلُونَ
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذۡتَ إِلَٰهًا غَيۡرِي لَأَجۡعَلَنَّكَ مِنَ ٱلۡمَسۡجُونِينَ
(Firauni) akasema: Ukijifanyia mungu mwengine asiyekuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ أَوَلَوۡ جِئۡتُكَ بِشَيۡءٖ مُّبِينٖ
Akasema: Je, hata kama nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ فَأۡتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wakweli.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhahiri.
Os Tafssir em língua árabe:
وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّٰظِرِينَ
Na akautoa nje mkono wake, mara ukawa mweupe kwa watazamao.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ لِلۡمَلَإِ حَوۡلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ
(Firauni) akawaambia waheshimiwa waliomzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
Os Tafssir em língua árabe:
يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُم بِسِحۡرِهِۦ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ
Anataka kuwatoa katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَٱبۡعَثۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Wakasema: Mpe muda yeye na kakaye na uwatume mijini wakusanyao watu.
Os Tafssir em língua árabe:
يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٖ
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Basi wakakusanywa wachawi kwa ajili ya miadi ya siku maalumu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلۡ أَنتُم مُّجۡتَمِعُونَ
Na watu wakaambiwa: Je, mtakusanyika?
Os Tafssir em língua árabe:
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Huenda tutawafuata wachawi ikiwa wao ndio watakaoshinda.
Os Tafssir em língua árabe:
فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُواْ لِفِرۡعَوۡنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Basi walipokuja wachawi, wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira ikiwa sisi ndio tutakaoshinda?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Akasema: Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ
Musa akwaambia: Tupeni mnavyotaka kutupa.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَلۡقَوۡاْ حِبَالَهُمۡ وَعِصِيَّهُمۡ وَقَالُواْ بِعِزَّةِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبُونَ
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَلۡقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ
Basi Musa akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza vile walivyovizua.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ
Hapo wachawi hao walipinduka wakasujudu.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ ءَامَنتُمۡ لَهُۥ قَبۡلَ أَنۡ ءَاذَنَ لَكُمۡۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِي عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحۡرَ فَلَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَرۡجُلَكُم مِّنۡ خِلَٰفٖ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمۡ أَجۡمَعِينَ
(Firauni) akasema: Je, mmemuamini kabla ya kuwaruhusu? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliyewafunza uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitawasulubisha misalabani nyote.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّا نَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika sisi tunatumai kwamba Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa tumekuwa wa kwanza wa Waumini.
Os Tafssir em língua árabe:
۞ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَسۡرِ بِعِبَادِيٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Na tulimuamrisha Musa kwa ufunuo: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَرۡسَلَ فِرۡعَوۡنُ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Basi Firauni akawatuma mijini wakusanyaji.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَشِرۡذِمَةٞ قَلِيلُونَ
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّهُمۡ لَنَا لَغَآئِظُونَ
Nao kwa hakika wanatuudhi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَخۡرَجۡنَٰهُم مِّن جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchemi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَكُنُوزٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ
Na mahazina, na vyeo vya heshima,
Os Tafssir em língua árabe:
كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Vivyo hivyo, na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَتۡبَعُوهُم مُّشۡرِقِينَ
Basi wakawafuata lilipochomoza jua.
Os Tafssir em língua árabe:
فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلۡجَمۡعَانِ قَالَ أَصۡحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدۡرَكُونَ
Na yalipoonana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumekutwa!
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ كَلَّآۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهۡدِينِ
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡبَحۡرَۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرۡقٖ كَٱلطَّوۡدِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tulimletea Musa ufunuo tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
Os Tafssir em língua árabe:
وَأَزۡلَفۡنَا ثَمَّ ٱلۡأٓخَرِينَ
Na tukawasongesha hapo karibu wale wengine.
Os Tafssir em língua árabe:
وَأَنجَيۡنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Tukawaokoa Musa na wale waliokuwa pamoja naye wote.
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawazamisha hao wengine.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si wenye kuamini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱتۡلُ عَلَيۡهِمۡ نَبَأَ إِبۡرَٰهِيمَ
Na wasomee habari za Ibrahim.
Os Tafssir em língua árabe:
إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَا تَعۡبُدُونَ
Alipomwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُواْ نَعۡبُدُ أَصۡنَامٗا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ هَلۡ يَسۡمَعُونَكُمۡ إِذۡ تَدۡعُونَ
Akasema: Je, yanawasikia mnapoyaita?
Os Tafssir em língua árabe:
أَوۡ يَنفَعُونَكُمۡ أَوۡ يَضُرُّونَ
Au yanawafaa, au yanawadhuru?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُواْ بَلۡ وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفۡعَلُونَ
Wakasema: Bali tuliwakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ أَفَرَءَيۡتُم مَّا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ
Akasema: Je, mmewaona hawa mnaowaabudu?
Os Tafssir em língua árabe:
أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلۡأَقۡدَمُونَ
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
Os Tafssir em língua árabe:
فَإِنَّهُمۡ عَدُوّٞ لِّيٓ إِلَّا رَبَّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
ٱلَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهۡدِينِ
Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلَّذِي هُوَ يُطۡعِمُنِي وَيَسۡقِينِ
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ
Na ninapougua, ni Yeye ndiye anayeniponesha.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحۡيِينِ
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلَّذِيٓ أَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لِي خَطِيٓـَٔتِي يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Na ambaye ndiye ninayemtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
Os Tafssir em língua árabe:
رَبِّ هَبۡ لِي حُكۡمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّٰلِحِينَ
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na walio wema.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱجۡعَل لِّي لِسَانَ صِدۡقٖ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na unijalie nitajwe kwa wema na watu watakaokuja baadaye.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱجۡعَلۡنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ
Na unijalie katika warithi wa Bustani za neema.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱغۡفِرۡ لِأَبِيٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَا تُخۡزِنِي يَوۡمَ يُبۡعَثُونَ
Wala usinihizi Siku watakapofufuliwa.
Os Tafssir em língua árabe:
يَوۡمَ لَا يَنفَعُ مَالٞ وَلَا بَنُونَ
Siku ambayo kwamba mali haitafaa kitu wala wana.
Os Tafssir em língua árabe:
إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٖ سَلِيمٖ
Isipokuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ
Na Pepo itasogezwa kwa wachamungu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِلۡغَاوِينَ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَقِيلَ لَهُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ
Na wataambiwa: Wako wapi mliokuwa mkiwaabudu
Os Tafssir em língua árabe:
مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلۡ يَنصُرُونَكُمۡ أَوۡ يَنتَصِرُونَ
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je, wanawasaidia, au wanajisaidia wenyewe?
Os Tafssir em língua árabe:
فَكُبۡكِبُواْ فِيهَا هُمۡ وَٱلۡغَاوُۥنَ
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَجُنُودُ إِبۡلِيسَ أَجۡمَعُونَ
Na majeshi ya Ibilisi yote.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُواْ وَهُمۡ فِيهَا يَخۡتَصِمُونَ
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
Os Tafssir em língua árabe:
تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhahiri.
Os Tafssir em língua árabe:
إِذۡ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Tulipowafanya nyinyi ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلۡمُجۡرِمُونَ
Na hawakutupoteza isipokuwa wale wakosefu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ
Basi hatuna waombezi wowote.
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٖ
Wala rafiki wa dhati.
Os Tafssir em língua árabe:
فَلَوۡ أَنَّ لَنَا كَرَّةٗ فَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Laiti tungelipata kurejea tena, tungelikuwa katika Waumini.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwingi wa kurehemu.
Os Tafssir em língua árabe:
كَذَّبَتۡ قَوۡمُ نُوحٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
Os Tafssir em língua árabe:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Nuhu: Je, hamumchi Mwenyezi Mungu?
Os Tafssir em língua árabe:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na siwaulizi juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Os Tafssir em língua árabe:
۞ قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلۡأَرۡذَلُونَ
Wakasema: Je, tukuamini wewe, ilhali wanaokufuata ni watu duni?
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ وَمَا عِلۡمِي بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Akasema: Ninayajuaje waliyokuwa wakiyafanya?
Os Tafssir em língua árabe:
إِنۡ حِسَابُهُمۡ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّيۖ لَوۡ تَشۡعُرُونَ
Hesabu yao haiko isipokuwa kwa Mola wao Mlezi, laiti mngelitambua!
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنۡ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ
Mimi si chochote isipokuwa ni Mwonyaji wa dhahiri shahiri.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمَرۡجُومِينَ
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوۡمِي كَذَّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikadhibisha.
Os Tafssir em língua árabe:
فَٱفۡتَحۡ بَيۡنِي وَبَيۡنَهُمۡ فَتۡحٗا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami miongoni mwa Waumini.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَنجَيۡنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِي ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na waliokuwa pamoja naye katika marikebu iliyosheheni.
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا بَعۡدُ ٱلۡبَاقِينَ
Kisha tukawazamisha baadaye waliobakia.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao waliokuwa Waumini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Os Tafssir em língua árabe:
كَذَّبَتۡ عَادٌ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kina 'Aad waliwakanusha Mitume.
Os Tafssir em língua árabe:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Hud: Je, hamchi Mungu?
Os Tafssir em língua árabe:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi juu yake ujira wowote, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
أَتَبۡنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةٗ تَعۡبَثُونَ
Je, mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
Os Tafssir em língua árabe:
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمۡ تَخۡلُدُونَ
Na mnajenga majengo ya kifahari kama kwamba mtaishi milele!
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِذَا بَطَشۡتُم بَطَشۡتُمۡ جَبَّارِينَ
Na mnapotumia nguvu, mnatumia nguvu kwa ujabari.
Os Tafssir em língua árabe:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِيٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعۡلَمُونَ
Na mcheni aliyewapa haya mnayoyajua.
Os Tafssir em língua árabe:
أَمَدَّكُم بِأَنۡعَٰمٖ وَبَنِينَ
Aliwapa wanyama wa kufuga na wana.
Os Tafssir em língua árabe:
وَجَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ
Na mabustani na chemchemi.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Hakika mimi ninawahofia adhabu ya Siku Kubwa.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡنَآ أَوَعَظۡتَ أَمۡ لَمۡ تَكُن مِّنَ ٱلۡوَٰعِظِينَ
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Haya si chochote isipokuwa ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ
Wala sisi hatutaadhibiwa.
Os Tafssir em língua árabe:
فَكَذَّبُوهُ فَأَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Wakamkadhibisha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Os Tafssir em língua árabe:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kina Thamud waliwakadhibisha Mitume.
Os Tafssir em língua árabe:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao Saleh: Je, hamumchi Mungu?
Os Tafssir em língua árabe:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
أَتُتۡرَكُونَ فِي مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ
Je, mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
Os Tafssir em língua árabe:
فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Katika mabustani, na chemchemi?
Os Tafssir em língua árabe:
وَزُرُوعٖ وَنَخۡلٖ طَلۡعُهَا هَضِيمٞ
Na konde na mitende yenye makole yaliyowiva.
Os Tafssir em língua árabe:
وَتَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتٗا فَٰرِهِينَ
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
Os Tafssir em língua árabe:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَا تُطِيعُوٓاْ أَمۡرَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ
Wala msitii amri za waliopitiliza mipaka
Os Tafssir em língua árabe:
ٱلَّذِينَ يُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا يُصۡلِحُونَ
Ambao wanafanya uharibifu katika nchi, wala hawatengenezi.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa.
Os Tafssir em língua árabe:
مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا فَأۡتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Wewe si chochote isipokuwa ni mtu kama sisi. Basi leta Ishara ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٞ لَّهَا شِرۡبٞ وَلَكُمۡ شِرۡبُ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٖ فَيَأۡخُذَكُمۡ عَذَابُ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Wala msimguse kwa wovu, ikawashika adhabu ya Siku Kubwa.
Os Tafssir em língua árabe:
فَعَقَرُوهَا فَأَصۡبَحُواْ نَٰدِمِينَ
Lakini wakamuua, na wakawa wenye kujuta.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَخَذَهُمُ ٱلۡعَذَابُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Os Tafssir em língua árabe:
كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Watu wa Luti waliwakadhibisha Mitume.
Os Tafssir em língua árabe:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Luti: Je, hamumchi Mungu?
Os Tafssir em língua árabe:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini mimi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala mimi sikuwauliza ujira wowote juu yake; ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
أَتَأۡتُونَ ٱلذُّكۡرَانَ مِنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Je, katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
Os Tafssir em língua árabe:
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمۡ رَبُّكُم مِّنۡ أَزۡوَٰجِكُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٌ عَادُونَ
Na mnaacha alichowaumbia Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka!
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُخۡرَجِينَ
Wakasema: Ewe Luti! Usipoacha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanaotolewa mji!
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلۡقَالِينَ
Akasema: Hakika mimi ni katika wanaokichukia hiki kitendo chenu.
Os Tafssir em língua árabe:
رَبِّ نَجِّنِي وَأَهۡلِي مِمَّا يَعۡمَلُونَ
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
Os Tafssir em língua árabe:
فَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote.
Os Tafssir em língua árabe:
إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ
Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma.
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawaangamiza wale wengine.
Os Tafssir em língua árabe:
وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyoonywa.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Os Tafssir em língua árabe:
كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ لۡـَٔيۡكَةِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
Os Tafssir em língua árabe:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ شُعَيۡبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Shuaibu alipowaambia: Je, hamumchi Mungu?
Os Tafssir em língua árabe:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
۞ أَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَلَا تَكُونُواْ مِنَ ٱلۡمُخۡسِرِينَ
Timizeni kipimo sawasawa, wala msiwe katika wanaopunja.
Os Tafssir em língua árabe:
وَزِنُواْ بِٱلۡقِسۡطَاسِ ٱلۡمُسۡتَقِيمِ
Na pimeni kwa haki iliyonyooka.
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَا تَبۡخَسُواْ ٱلنَّاسَ أَشۡيَآءَهُمۡ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri katika ardhi kwa kufanya uharibifu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ وَٱلۡجِبِلَّةَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na mcheni aliyewaumba nyinyi na vizazi vilivyotangulia.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ
Wakasema: Hakika wewe ni katika waliorogwa.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلۡكَٰذِبِينَ
Na wewe si chochote isipokuwa ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
Os Tafssir em língua árabe:
فَأَسۡقِطۡ عَلَيۡنَا كِسَفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
Os Tafssir em língua árabe:
قَالَ رَبِّيٓ أَعۡلَمُ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayoyatenda.
Os Tafssir em língua árabe:
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمۡ عَذَابُ يَوۡمِ ٱلظُّلَّةِۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٍ
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya Siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya Siku kubwa.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Os Tafssir em língua árabe:
نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلۡأَمِينُ
Ameuteremsha Roho muaminifu.
Os Tafssir em língua árabe:
عَلَىٰ قَلۡبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُنذِرِينَ
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji.
Os Tafssir em língua árabe:
بِلِسَانٍ عَرَبِيّٖ مُّبِينٖ
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
Os Tafssir em língua árabe:
وَإِنَّهُۥ لَفِي زُبُرِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
Os Tafssir em língua árabe:
أَوَلَمۡ يَكُن لَّهُمۡ ءَايَةً أَن يَعۡلَمَهُۥ عُلَمَٰٓؤُاْ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Je, haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanauchoni wa Wana wa Israili?
Os Tafssir em língua árabe:
وَلَوۡ نَزَّلۡنَٰهُ عَلَىٰ بَعۡضِ ٱلۡأَعۡجَمِينَ
Na lau kuwa tungeliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa Waarabu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَقَرَأَهُۥ عَلَيۡهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ مُؤۡمِنِينَ
Na akawasomea, wasingelikuwa wenye kuamini.
Os Tafssir em língua árabe:
كَذَٰلِكَ سَلَكۡنَٰهُ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wahalifu.
Os Tafssir em língua árabe:
لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُاْ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
Os Tafssir em língua árabe:
فَيَأۡتِيَهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana habari.
Os Tafssir em língua árabe:
فَيَقُولُواْ هَلۡ نَحۡنُ مُنظَرُونَ
Na watasema: Je, tutapewa muhula?
Os Tafssir em língua árabe:
أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ
Basi je, wanaihimiza adhabu yetu?
Os Tafssir em língua árabe:
أَفَرَءَيۡتَ إِن مَّتَّعۡنَٰهُمۡ سِنِينَ
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka.
Os Tafssir em língua árabe:
ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُواْ يُوعَدُونَ
Kisha yakawafikia waliyokuwa wakiahidiwa.
Os Tafssir em língua árabe:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يُمَتَّعُونَ
Yatawafaa nini yale waliyostareheshewa?
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
Wala hatukuangamiza mji wowote isipokuwa ulikuwa na waonyaji.
Os Tafssir em língua árabe:
ذِكۡرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَا تَنَزَّلَتۡ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ
Wala Mashetani hawakuteremka nayo.
Os Tafssir em língua árabe:
وَمَا يَنۢبَغِي لَهُمۡ وَمَا يَسۡتَطِيعُونَ
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّهُمۡ عَنِ ٱلسَّمۡعِ لَمَعۡزُولُونَ
Hakika hao wametengwa na kusikia.
Os Tafssir em língua árabe:
فَلَا تَدۡعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُعَذَّبِينَ
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakaoadhibiwa.
Os Tafssir em língua árabe:
وَأَنذِرۡ عَشِيرَتَكَ ٱلۡأَقۡرَبِينَ
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na watwae kwa upole wanaokufuata miongoni mwa Waumini.
Os Tafssir em língua árabe:
فَإِنۡ عَصَوۡكَ فَقُلۡ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تَعۡمَلُونَ
Na ikiwa watakuasi, basi sema: Mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyatenda.
Os Tafssir em língua árabe:
وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
Os Tafssir em língua árabe:
ٱلَّذِي يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ
Ambaye anakuona unaposimama.
Os Tafssir em língua árabe:
وَتَقَلُّبَكَ فِي ٱلسَّٰجِدِينَ
Na mageuko yako kati ya wanaosujudu.
Os Tafssir em língua árabe:
إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua zaidi.
Os Tafssir em língua árabe:
هَلۡ أُنَبِّئُكُمۡ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَٰطِينُ
Je, niwaambieni nani wanawashukia Mashetani?
Os Tafssir em língua árabe:
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٖ
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
Os Tafssir em língua árabe:
يُلۡقُونَ ٱلسَّمۡعَ وَأَكۡثَرُهُمۡ كَٰذِبُونَ
Wanawapelekea yale wanayoyasikia; na wengi wao ni waongo.
Os Tafssir em língua árabe:
وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلۡغَاوُۥنَ
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
Os Tafssir em língua árabe:
أَلَمۡ تَرَ أَنَّهُمۡ فِي كُلِّ وَادٖ يَهِيمُونَ
Je, huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
Os Tafssir em língua árabe:
وَأَنَّهُمۡ يَقُولُونَ مَا لَا يَفۡعَلُونَ
Na kwamba wao husema wasiyoyatenda?
Os Tafssir em língua árabe:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَذَكَرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا وَٱنتَصَرُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا ظُلِمُواْۗ وَسَيَعۡلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ أَيَّ مُنقَلَبٖ يَنقَلِبُونَ
Isipokuwa wale walioamini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapodhulumiwa. Na wanaodhulumu watakuja jua mgeuko gani watakaogeuka.
Os Tafssir em língua árabe:
 
Tradução dos significados Surah: Ash-Shu'araa
Índice de capítulos Número de página
 
Tradução dos significados do Nobre Qur’an. - Tradução Suaíli - Centro de tradução Rawad - Índice de tradução

Tradução realizada pela equipe do Centro de Tradução Rowwad em cooperação com a Associação de Chamada em Al-Rabwah e a Associação para o Serviço do Conteúdo Islâmico em Idiomas.

Fechar