Check out the new design

《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 舍尔拉仪   段:

Ash-Shu'ara

طسٓمٓ
Tw'a Siin Miim.[1]
[1] Herufi hizi "Tw'aa, Sin, Miim" na herufi nyinginezo za mkato zilizo mwanzoni mwa sura mbalimbali zinaonyesha hali ya ushindi wa Qur-ani. Kwani, washirikina walipewa changamoto kwayo, lakini wakashindwa na hawakuweza kuipinga, ilhali inajumuisha herufi hizi zinazounda lugha ya Kiarabu. Kwa hivyo, kutoweza kwa Waarabu kuleta kitu kama hicho - ingawa walikuwa ndio watu wenye ufasaha zaidi - kunaonyesha kwamba Qur-ani ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
阿拉伯语经注:
تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ
Hizi ni Aya za Kitabu kinachobainisha.
阿拉伯语经注:
لَعَلَّكَ بَٰخِعٞ نَّفۡسَكَ أَلَّا يَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ
Huenda ukaihiliki nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
阿拉伯语经注:
إِن نَّشَأۡ نُنَزِّلۡ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ ءَايَةٗ فَظَلَّتۡ أَعۡنَٰقُهُمۡ لَهَا خَٰضِعِينَ
Tungependa, tungeliwateremshia kutoka mbinguni Ishara zikashinda zimezinyenyekea shingo zao.
阿拉伯语经注:
وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن ذِكۡرٖ مِّنَ ٱلرَّحۡمَٰنِ مُحۡدَثٍ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهُ مُعۡرِضِينَ
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman (Mwingi wa rehema), isipokuwa wao huupa mgongo.
阿拉伯语经注:
فَقَدۡ كَذَّبُواْ فَسَيَأۡتِيهِمۡ أَنۢبَٰٓؤُاْ مَا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Kwa yakini wamekwisha kanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia habari za yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.
阿拉伯语经注:
أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَمۡ أَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجٖ كَرِيمٍ
Je, hawakuiona ardhi, ni mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
阿拉伯语经注:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
阿拉伯语经注:
وَإِذۡ نَادَىٰ رَبُّكَ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱئۡتِ ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّٰلِمِينَ
Na Mola wako Mlezi, alipomwita Musa, akamwambia: Nenda kwa kaumu madhalimu.
阿拉伯语经注:
قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَۚ أَلَا يَتَّقُونَ
Kaumu wa Firauni. Kwani hawamchi Mwenyezi Mungu?
阿拉伯语经注:
قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi, hakika mimi ninachelea kwamba watanikadhibisha.
阿拉伯语经注:
وَيَضِيقُ صَدۡرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرۡسِلۡ إِلَىٰ هَٰرُونَ
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
阿拉伯语经注:
وَلَهُمۡ عَلَيَّ ذَنۢبٞ فَأَخَافُ أَن يَقۡتُلُونِ
Na wao wana dhambi niliyowafanyia, kwa hivyo ninahofu wanaweza kuniua.
阿拉伯语经注:
قَالَ كَلَّاۖ فَٱذۡهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسۡتَمِعُونَ
Akasema: Sivyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
阿拉伯语经注:
فَأۡتِيَا فِرۡعَوۡنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Basi nendeni kwa Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
أَنۡ أَرۡسِلۡ مَعَنَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Kwamba: Waachilie Wana wa Israili waende pamoja nasi.
阿拉伯语经注:
قَالَ أَلَمۡ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدٗا وَلَبِثۡتَ فِينَا مِنۡ عُمُرِكَ سِنِينَ
(Firauni) akasema: Je, sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa miongoni mwetu katika umri wako miaka mingi?
阿拉伯语经注:
وَفَعَلۡتَ فَعۡلَتَكَ ٱلَّتِي فَعَلۡتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na ukatenda kitendo chako ulichotenda, nawe ukawa miongoni mwa wenye kukufuru?
阿拉伯语经注:
قَالَ فَعَلۡتُهَآ إِذٗا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipokuwa miongoni mwa wale waliopotea.
阿拉伯语经注:
فَفَرَرۡتُ مِنكُمۡ لَمَّا خِفۡتُكُمۡ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكۡمٗا وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Basi nikawakimbia nilipowahofu, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
阿拉伯语经注:
وَتِلۡكَ نِعۡمَةٞ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنۡ عَبَّدتَّ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
阿拉伯语经注:
قَالَ فِرۡعَوۡنُ وَمَا رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Firauni akasema: Na ni nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
阿拉伯语经注:
قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
阿拉伯语经注:
قَالَ لِمَنۡ حَوۡلَهُۥٓ أَلَا تَسۡتَمِعُونَ
(Firauni) akawaambia waliomzunguka: Kwani hamsikilizi?
阿拉伯语经注:
قَالَ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
阿拉伯语经注:
قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِيٓ أُرۡسِلَ إِلَيۡكُمۡ لَمَجۡنُونٞ
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliyetumwa kwenu ni mwendawazimu.
阿拉伯语经注:
قَالَ رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡقِلُونَ
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyo baina yake, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
阿拉伯语经注:
قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذۡتَ إِلَٰهًا غَيۡرِي لَأَجۡعَلَنَّكَ مِنَ ٱلۡمَسۡجُونِينَ
(Firauni) akasema: Ukijifanyia mungu mwingine asiyekuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
阿拉伯语经注:
قَالَ أَوَلَوۡ جِئۡتُكَ بِشَيۡءٖ مُّبِينٖ
Akasema: Je, hata kama nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
阿拉伯语经注:
قَالَ فَأۡتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wakweli.
阿拉伯语经注:
فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ
Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhahiri.
阿拉伯语经注:
وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّٰظِرِينَ
Na akautoa nje mkono wake, mara ukawa mweupe kwa watazamao.
阿拉伯语经注:
قَالَ لِلۡمَلَإِ حَوۡلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ
(Firauni) akawaambia waheshimiwa waliomzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu.
阿拉伯语经注:
يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُم بِسِحۡرِهِۦ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ
Anataka kuwatoa katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?
阿拉伯语经注:
قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَٱبۡعَثۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Wakasema: Mpe muda yeye na kakaye na uwatume mijini wakusanyao watu.
阿拉伯语经注:
يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٖ
Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu.
阿拉伯语经注:
فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Basi wakakusanywa wachawi kwa ajili ya miadi ya siku maalumu.
阿拉伯语经注:
وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلۡ أَنتُم مُّجۡتَمِعُونَ
Na watu wakaambiwa: Je, mtakusanyika?
阿拉伯语经注:
لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Huenda tutawafuata wachawi ikiwa wao ndio watakaoshinda.
阿拉伯语经注:
فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُواْ لِفِرۡعَوۡنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ
Basi walipokuja wachawi, wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira ikiwa sisi ndio tutakaoshinda?
阿拉伯语经注:
قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ
Akasema: Naam! Na hakika mtakuwa katika watu wa mbele.
阿拉伯语经注:
قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ
Musa akawaambia: Tupeni mnavyotaka kutupa.
阿拉伯语经注:
فَأَلۡقَوۡاْ حِبَالَهُمۡ وَعِصِيَّهُمۡ وَقَالُواْ بِعِزَّةِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّا لَنَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبُونَ
Basi wakatupa kamba zao na fimbo zao, na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi hapana shaka ni wenye kushinda.
阿拉伯语经注:
فَأَلۡقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ
Basi Musa akatupa fimbo yake, nayo mara ikavimeza vile walivyovizua.
阿拉伯语经注:
فَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ
Hapo wachawi hao walipinduka wakasujudu.
阿拉伯语经注:
قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wakasema: Tumemuamini Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
رَبِّ مُوسَىٰ وَهَٰرُونَ
Mola Mlezi wa Musa na Harun.
阿拉伯语经注:
قَالَ ءَامَنتُمۡ لَهُۥ قَبۡلَ أَنۡ ءَاذَنَ لَكُمۡۖ إِنَّهُۥ لَكَبِيرُكُمُ ٱلَّذِي عَلَّمَكُمُ ٱلسِّحۡرَ فَلَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَۚ لَأُقَطِّعَنَّ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَرۡجُلَكُم مِّنۡ خِلَٰفٖ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمۡ أَجۡمَعِينَ
(Firauni) akasema: Je, mmemuamini kabla ya kuwaruhusu? Bila ya shaka yeye basi ndiye mkubwa wenu aliyewafunza uchawi. Basi mtakuja jua! Nitakatakata mikono yenu na miguu yenu kwa kutofautisha. Na nitawasulubisha misalabani nyote.
阿拉伯语经注:
قَالُواْ لَا ضَيۡرَۖ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ
Wakasema: Haidhuru, kwani sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
阿拉伯语经注:
إِنَّا نَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَٰيَٰنَآ أَن كُنَّآ أَوَّلَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika sisi tunatumai kwamba Mola wetu Mlezi atatusamehe makosa yetu, kwa kuwa tumekuwa wa kwanza wa Waumini.
阿拉伯语经注:
۞ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَسۡرِ بِعِبَادِيٓ إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ
Na tulimuamrisha Musa kwa ufunuo: Nenda na waja wangu wakati wa usiku. Kwa hakika mtafuatwa.
阿拉伯语经注:
فَأَرۡسَلَ فِرۡعَوۡنُ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ
Basi Firauni akawatuma mijini wakusanyaji.
阿拉伯语经注:
إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَشِرۡذِمَةٞ قَلِيلُونَ
(Wakieneza): Hakika hawa ni kikundi kidogo.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّهُمۡ لَنَا لَغَآئِظُونَ
Nao kwa hakika wanatuudhi.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَٰذِرُونَ
Na sisi ni wengi, wenye kuchukua hadhari.
阿拉伯语经注:
فَأَخۡرَجۡنَٰهُم مِّن جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Basi tukawatoa katika mabustani na chemchemi.
阿拉伯语经注:
وَكُنُوزٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ
Na mahazina, na vyeo vya heshima,
阿拉伯语经注:
كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Vivyo hivyo, na tukawarithisha hayo Wana wa Israili.
阿拉伯语经注:
فَأَتۡبَعُوهُم مُّشۡرِقِينَ
Basi wakawafuata lilipochomoza jua.
阿拉伯语经注:
فَلَمَّا تَرَٰٓءَا ٱلۡجَمۡعَانِ قَالَ أَصۡحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدۡرَكُونَ
Na yalipoonana majeshi mawili haya, watu wa Musa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumekutwa!
阿拉伯语经注:
قَالَ كَلَّآۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهۡدِينِ
(Musa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!
阿拉伯语经注:
فَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡبَحۡرَۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرۡقٖ كَٱلطَّوۡدِ ٱلۡعَظِيمِ
Na tulimletea Musa ufunuo tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa.
阿拉伯语经注:
وَأَزۡلَفۡنَا ثَمَّ ٱلۡأٓخَرِينَ
Na tukawasongesha hapo karibu wale wengine.
阿拉伯语经注:
وَأَنجَيۡنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Tukawaokoa Musa na wale waliokuwa pamoja naye wote.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawazamisha hao wengine.
阿拉伯语经注:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si wenye kuamini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
阿拉伯语经注:
وَٱتۡلُ عَلَيۡهِمۡ نَبَأَ إِبۡرَٰهِيمَ
Na wasomee habari za Ibrahim.
阿拉伯语经注:
إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَا تَعۡبُدُونَ
Alipomwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?
阿拉伯语经注:
قَالُواْ نَعۡبُدُ أَصۡنَامٗا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ
Wakasema: Tunaabudu masanamu, daima tunayanyenyekea.
阿拉伯语经注:
قَالَ هَلۡ يَسۡمَعُونَكُمۡ إِذۡ تَدۡعُونَ
Akasema: Je, yanawasikia mnapoyaita?
阿拉伯语经注:
أَوۡ يَنفَعُونَكُمۡ أَوۡ يَضُرُّونَ
Au yanawafaa, au yanawadhuru?
阿拉伯语经注:
قَالُواْ بَلۡ وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفۡعَلُونَ
Wakasema: Bali tuliwakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo.
阿拉伯语经注:
قَالَ أَفَرَءَيۡتُم مَّا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ
Akasema: Je, mmewaona hawa mnaowaabudu?
阿拉伯语经注:
أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلۡأَقۡدَمُونَ
Nyinyi na baba zenu wa zamani?
阿拉伯语经注:
فَإِنَّهُمۡ عَدُوّٞ لِّيٓ إِلَّا رَبَّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
ٱلَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهۡدِينِ
Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa
阿拉伯语经注:
وَٱلَّذِي هُوَ يُطۡعِمُنِي وَيَسۡقِينِ
Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha.
阿拉伯语经注:
وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ
Na ninapougua, ni Yeye ndiye anayeniponesha.
阿拉伯语经注:
وَٱلَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحۡيِينِ
Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha.
阿拉伯语经注:
وَٱلَّذِيٓ أَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لِي خَطِيٓـَٔتِي يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Na ambaye ndiye ninayemtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo.
阿拉伯语经注:
رَبِّ هَبۡ لِي حُكۡمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّٰلِحِينَ
Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na walio wema.
阿拉伯语经注:
وَٱجۡعَل لِّي لِسَانَ صِدۡقٖ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ
Na unijalie nitajwe kwa wema na watu watakaokuja baadaye.
阿拉伯语经注:
وَٱجۡعَلۡنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ
Na unijalie katika warithi wa Bustani za neema.
阿拉伯语经注:
وَٱغۡفِرۡ لِأَبِيٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ
Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu.
阿拉伯语经注:
وَلَا تُخۡزِنِي يَوۡمَ يُبۡعَثُونَ
Wala usinihizi Siku watakapofufuliwa.
阿拉伯语经注:
يَوۡمَ لَا يَنفَعُ مَالٞ وَلَا بَنُونَ
Siku ambayo kwamba mali haitafaa kitu wala wana.
阿拉伯语经注:
إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٖ سَلِيمٖ
Isipokuwa mwenye kumjia Mwenyezi Mungu na moyo safi.
阿拉伯语经注:
وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ
Na Bustani ya mbiguni itasogezwa kwa wacha Mungu.
阿拉伯语经注:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِلۡغَاوِينَ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa wapotovu.
阿拉伯语经注:
وَقِيلَ لَهُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ
Na wataambiwa: Wako wapi mliokuwa mkiwaabudu
阿拉伯语经注:
مِن دُونِ ٱللَّهِ هَلۡ يَنصُرُونَكُمۡ أَوۡ يَنتَصِرُونَ
Badala ya Mwenyezi Mungu? Je, wanawasaidia, au wanajisaidia wenyewe?
阿拉伯语经注:
فَكُبۡكِبُواْ فِيهَا هُمۡ وَٱلۡغَاوُۥنَ
Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu.
阿拉伯语经注:
وَجُنُودُ إِبۡلِيسَ أَجۡمَعُونَ
Na majeshi ya Ibilisi yote.
阿拉伯语经注:
قَالُواْ وَهُمۡ فِيهَا يَخۡتَصِمُونَ
Watasema, na hali ya kuwa wanazozana humo:
阿拉伯语经注:
تَٱللَّهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ
Wallahi! Kwa yakini tulikuwa katika upotovu ulio dhahiri.
阿拉伯语经注:
إِذۡ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Tulipowafanya nyinyi ni sawa na Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَضَلَّنَآ إِلَّا ٱلۡمُجۡرِمُونَ
Na hawakutupoteza isipokuwa wale wakosefu.
阿拉伯语经注:
فَمَا لَنَا مِن شَٰفِعِينَ
Basi hatuna waombezi wowote.
阿拉伯语经注:
وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٖ
Wala rafiki wa dhati.
阿拉伯语经注:
فَلَوۡ أَنَّ لَنَا كَرَّةٗ فَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Laiti tungelipata kurejea tena, tungelikuwa katika Waumini.
阿拉伯语经注:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwingi wa kurehemu.
阿拉伯语经注:
كَذَّبَتۡ قَوۡمُ نُوحٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.
阿拉伯语经注:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Nuhu: Je, hamumchi Mwenyezi Mungu?
阿拉伯语经注:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
阿拉伯语经注:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na siwaulizi juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
阿拉伯语经注:
۞ قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلۡأَرۡذَلُونَ
Wakasema: Je, tukuamini wewe, ilhali wanaokufuata ni watu duni?
阿拉伯语经注:
قَالَ وَمَا عِلۡمِي بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Akasema: Ninayajuaje waliyokuwa wakiyafanya?
阿拉伯语经注:
إِنۡ حِسَابُهُمۡ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّيۖ لَوۡ تَشۡعُرُونَ
Hesabu yao haiko isipokuwa kwa Mola wao Mlezi, laiti mngelitambua!
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.
阿拉伯语经注:
إِنۡ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ
Mimi si chochote isipokuwa ni Mwonyaji wa dhahiri shahiri.
阿拉伯语经注:
قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمَرۡجُومِينَ
Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.
阿拉伯语经注:
قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوۡمِي كَذَّبُونِ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikadhibisha.
阿拉伯语经注:
فَٱفۡتَحۡ بَيۡنِي وَبَيۡنَهُمۡ فَتۡحٗا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami miongoni mwa Waumini.
阿拉伯语经注:
فَأَنجَيۡنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِي ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ
Kwa hivyo tukamwokoa yeye na waliokuwa pamoja naye katika marikebu iliyosheheni.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا بَعۡدُ ٱلۡبَاقِينَ
Kisha tukawazamisha baadaye waliobakia.
阿拉伯语经注:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao waliokuwa Waumini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
阿拉伯语经注:
كَذَّبَتۡ عَادٌ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kina 'Aad waliwakanusha Mitume.
阿拉伯语经注:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Hud: Je, hamumchi Mungu?
阿拉伯语经注:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
阿拉伯语经注:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi juu yake ujira wowote, kwani ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
أَتَبۡنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةٗ تَعۡبَثُونَ
Je, mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?
阿拉伯语经注:
وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمۡ تَخۡلُدُونَ
Na mnajenga majengo ya kifahari kama kwamba mtaishi milele!
阿拉伯语经注:
وَإِذَا بَطَشۡتُم بَطَشۡتُمۡ جَبَّارِينَ
Na mnapotumia nguvu, mnatumia nguvu kwa ujabari.
阿拉伯语经注:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
阿拉伯语经注:
وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِيٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعۡلَمُونَ
Na mcheni aliyewapa haya mnayoyajua.
阿拉伯语经注:
أَمَدَّكُم بِأَنۡعَٰمٖ وَبَنِينَ
Aliwapa wanyama wa kufuga na wana.
阿拉伯语经注:
وَجَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ
Na mabustani na chemchemi.
阿拉伯语经注:
إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Hakika mimi ninawahofia adhabu ya Siku Kubwa.
阿拉伯语经注:
قَالُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡنَآ أَوَعَظۡتَ أَمۡ لَمۡ تَكُن مِّنَ ٱلۡوَٰعِظِينَ
Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.
阿拉伯语经注:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Haya si chochote isipokuwa ni mtindo wa watu wa tokea zamani.
阿拉伯语经注:
وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ
Wala sisi hatutaadhibiwa.
阿拉伯语经注:
فَكَذَّبُوهُ فَأَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Wakamkadhibisha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
阿拉伯语经注:
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Kina Thamud waliwakadhibisha Mitume.
阿拉伯语经注:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao Saleh: Je, hamumchi Mungu?
阿拉伯语经注:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
阿拉伯语经注:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini.
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
أَتُتۡرَكُونَ فِي مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ
Je, mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?
阿拉伯语经注:
فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٖ
Katika mabustani, na chemchemi?
阿拉伯语经注:
وَزُرُوعٖ وَنَخۡلٖ طَلۡعُهَا هَضِيمٞ
Na konde na mitende yenye makole yaliyowiva.
阿拉伯语经注:
وَتَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتٗا فَٰرِهِينَ
Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.
阿拉伯语经注:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
阿拉伯语经注:
وَلَا تُطِيعُوٓاْ أَمۡرَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ
Wala msitii amri za waliopitiliza mipaka
阿拉伯语经注:
ٱلَّذِينَ يُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا يُصۡلِحُونَ
Ambao wanafanya uharibifu katika nchi, wala hawatengenezi.
阿拉伯语经注:
قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ
Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa.
阿拉伯语经注:
مَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا فَأۡتِ بِـَٔايَةٍ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Wewe si chochote isipokuwa ni mtu kama sisi. Basi leta Ishara ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
阿拉伯语经注:
قَالَ هَٰذِهِۦ نَاقَةٞ لَّهَا شِرۡبٞ وَلَكُمۡ شِرۡبُ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa, na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalumu.
阿拉伯语经注:
وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوٓءٖ فَيَأۡخُذَكُمۡ عَذَابُ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Wala msimguse kwa wovu, ikawashika adhabu ya Siku Kubwa.
阿拉伯语经注:
فَعَقَرُوهَا فَأَصۡبَحُواْ نَٰدِمِينَ
Lakini wakamuua, na wakawa wenye kujuta.
阿拉伯语经注:
فَأَخَذَهُمُ ٱلۡعَذَابُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Basi ikawapata adhabu. Hakika katika hayo ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
阿拉伯语经注:
كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Watu wa Luti waliwakadhibisha Mitume.
阿拉伯语经注:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Alipowaambia ndugu yao, Luti: Je, hamumchi Mungu?
阿拉伯语经注:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu kwenu.
阿拉伯语经注:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini mimi.
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala mimi sikuwauliza ujira wowote juu yake; ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
أَتَأۡتُونَ ٱلذُّكۡرَانَ مِنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Je, katika viumbe vyote mnawaingilia wanaume?
阿拉伯语经注:
وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمۡ رَبُّكُم مِّنۡ أَزۡوَٰجِكُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٌ عَادُونَ
Na mnaacha alichowaumbia Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka!
阿拉伯语经注:
قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُخۡرَجِينَ
Wakasema: Ewe Luti! Usipoacha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanaotolewa mji!
阿拉伯语经注:
قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلۡقَالِينَ
Akasema: Hakika mimi ni katika wanaokichukia hiki kitendo chenu.
阿拉伯语经注:
رَبِّ نَجِّنِي وَأَهۡلِي مِمَّا يَعۡمَلُونَ
Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo.
阿拉伯语经注:
فَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ
Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote.
阿拉伯语经注:
إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ
Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ
Kisha tukawaangamiza wale wengine.
阿拉伯语经注:
وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلۡمُنذَرِينَ
Na tukawanyeshea mvua, basi ni ovu mno mvua ya waliyoonywa.
阿拉伯语经注:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
阿拉伯语经注:
كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ لۡـَٔيۡكَةِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Watu wa Machakani waliwakanusha Mitume.
阿拉伯语经注:
إِذۡ قَالَ لَهُمۡ شُعَيۡبٌ أَلَا تَتَّقُونَ
Shuaibu alipowaambia: Je, hamumchi Mungu?
阿拉伯语经注:
إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ
Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.
阿拉伯语经注:
فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ
Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nitiini mimi.
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wala siwaulizi ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
۞ أَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَلَا تَكُونُواْ مِنَ ٱلۡمُخۡسِرِينَ
Timizeni kipimo sawasawa, wala msiwe katika wanaopunja.
阿拉伯语经注:
وَزِنُواْ بِٱلۡقِسۡطَاسِ ٱلۡمُسۡتَقِيمِ
Na pimeni kwa haki iliyonyooka.
阿拉伯语经注:
وَلَا تَبۡخَسُواْ ٱلنَّاسَ أَشۡيَآءَهُمۡ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ
Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri katika ardhi kwa kufanya uharibifu.
阿拉伯语经注:
وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ وَٱلۡجِبِلَّةَ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na mcheni aliyewaumba nyinyi na vizazi vilivyotangulia.
阿拉伯语经注:
قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ
Wakasema: Hakika wewe ni katika waliorogwa.
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلۡكَٰذِبِينَ
Na wewe si chochote isipokuwa ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo.
阿拉伯语经注:
فَأَسۡقِطۡ عَلَيۡنَا كِسَفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.
阿拉伯语经注:
قَالَ رَبِّيٓ أَعۡلَمُ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayoyatenda.
阿拉伯语经注:
فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمۡ عَذَابُ يَوۡمِ ٱلظُّلَّةِۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٍ
Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya Siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya Siku kubwa.
阿拉伯语经注:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ
Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ
Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na bila ya shaka hii ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
阿拉伯语经注:
نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلۡأَمِينُ
Ameuteremsha Roho muaminifu.
阿拉伯语经注:
عَلَىٰ قَلۡبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُنذِرِينَ
Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji.
阿拉伯语经注:
بِلِسَانٍ عَرَبِيّٖ مُّبِينٖ
Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi.
阿拉伯语经注:
وَإِنَّهُۥ لَفِي زُبُرِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale.
阿拉伯语经注:
أَوَلَمۡ يَكُن لَّهُمۡ ءَايَةً أَن يَعۡلَمَهُۥ عُلَمَٰٓؤُاْ بَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ
Je, haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanauchoni wa Wana wa Israili?
阿拉伯语经注:
وَلَوۡ نَزَّلۡنَٰهُ عَلَىٰ بَعۡضِ ٱلۡأَعۡجَمِينَ
Na lau kuwa tungeliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa Waarabu.
阿拉伯语经注:
فَقَرَأَهُۥ عَلَيۡهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ مُؤۡمِنِينَ
Na akawasomea, wasingelikuwa wenye kuamini.
阿拉伯语经注:
كَذَٰلِكَ سَلَكۡنَٰهُ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wahalifu.
阿拉伯语经注:
لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُاْ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ
Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.
阿拉伯语经注:
فَيَأۡتِيَهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ
Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana habari.
阿拉伯语经注:
فَيَقُولُواْ هَلۡ نَحۡنُ مُنظَرُونَ
Na watasema: Je, tutapewa muhula?
阿拉伯语经注:
أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ
Basi je, wanaihimiza adhabu yetu?
阿拉伯语经注:
أَفَرَءَيۡتَ إِن مَّتَّعۡنَٰهُمۡ سِنِينَ
Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُواْ يُوعَدُونَ
Kisha yakawafikia waliyokuwa wakiahidiwa.
阿拉伯语经注:
مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يُمَتَّعُونَ
Yatawafaa nini yale waliyostareheshewa?
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ
Wala hatukuangamiza mji wowote isipokuwa ulikuwa na waonyaji.
阿拉伯语经注:
ذِكۡرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu.
阿拉伯语经注:
وَمَا تَنَزَّلَتۡ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ
Wala Mashetani hawakuteremka nayo.
阿拉伯语经注:
وَمَا يَنۢبَغِي لَهُمۡ وَمَا يَسۡتَطِيعُونَ
Wala haitakiwi kwao, na wala hawawezi.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُمۡ عَنِ ٱلسَّمۡعِ لَمَعۡزُولُونَ
Hakika hao wametengwa na kusikia.
阿拉伯语经注:
فَلَا تَدۡعُ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُعَذَّبِينَ
Basi usimwombe mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakaoadhibiwa.
阿拉伯语经注:
وَأَنذِرۡ عَشِيرَتَكَ ٱلۡأَقۡرَبِينَ
Na uwaonye jamaa zako walio karibu nawe.
阿拉伯语经注:
وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِمَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ
Na watwae kwa upole wanaokufuata miongoni mwa Waumini.
阿拉伯语经注:
فَإِنۡ عَصَوۡكَ فَقُلۡ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تَعۡمَلُونَ
Na ikiwa watakuasi, basi sema: Mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyatenda.
阿拉伯语经注:
وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ
Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu, Mwingi wa kurehemu.
阿拉伯语经注:
ٱلَّذِي يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ
Ambaye anakuona unaposimama.
阿拉伯语经注:
وَتَقَلُّبَكَ فِي ٱلسَّٰجِدِينَ
Na mageuko yako kati ya wanaosujudu.
阿拉伯语经注:
إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua zaidi.
阿拉伯语经注:
هَلۡ أُنَبِّئُكُمۡ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ ٱلشَّيَٰطِينُ
Je, niwaambieni nani wanawashukia Mashetani?
阿拉伯语经注:
تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٖ
Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi.
阿拉伯语经注:
يُلۡقُونَ ٱلسَّمۡعَ وَأَكۡثَرُهُمۡ كَٰذِبُونَ
Wanawapelekea yale wanayoyasikia; na wengi wao ni waongo.
阿拉伯语经注:
وَٱلشُّعَرَآءُ يَتَّبِعُهُمُ ٱلۡغَاوُۥنَ
Na watungaji mashairi ni wapotofu ndio wanawafuata.
阿拉伯语经注:
أَلَمۡ تَرَ أَنَّهُمۡ فِي كُلِّ وَادٖ يَهِيمُونَ
Je, huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?
阿拉伯语经注:
وَأَنَّهُمۡ يَقُولُونَ مَا لَا يَفۡعَلُونَ
Na kwamba wao husema wasiyoyatenda?
阿拉伯语经注:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ وَذَكَرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا وَٱنتَصَرُواْ مِنۢ بَعۡدِ مَا ظُلِمُواْۗ وَسَيَعۡلَمُ ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ أَيَّ مُنقَلَبٖ يَنقَلِبُونَ
Isipokuwa wale walioamini, na wakatenda mema, na wakamkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi, na wakajitetea wanapodhulumiwa. Na wanaodhulumu watakuja jua mgeuko gani watakaogeuka.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 舍尔拉仪
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 - 译解目录

由拉瓦德翻译中心团队与拉布瓦 الدعوة协会和伊斯兰内容服务协会合作翻译。

关闭