Check out the new design

クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - ルゥワード翻訳事業センター * - 対訳の目次


対訳 章: 筆章   節:

Al-Qalam

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ
Nuun. Ninaapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.
アラビア語 クルアーン注釈:
مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyokatika.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ
Na hakika wewe una tabia tukufu.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ
Karibu utaona, na wao wataona.
アラビア語 クルアーン注釈:
بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ
Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliyeipotea Njia yake, na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ
Basi usiwatii wanaokadhibisha.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ
Wanatamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ
Wala usimtii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ
Mtapitapi, apitaye akifitini.
アラビア語 クルアーン注釈:
مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ
Mwenye kuzuia mno heri, dhalimu, mwingi wa madhambi.
アラビア語 クルアーン注釈:
عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
アラビア語 クルアーン注釈:
إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Anaposomewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uongo za watu wa zamani!
アラビア語 クルアーン注釈:
سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyowajaribu wale wenye shamba, walipoapa kwamba watayavuna mazao yake itakapokuwa asubuhi.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
アラビア語 クルアーン注釈:
فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
アラビア語 クルアーン注釈:
فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ
Likawa kama usiku wa giza.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ
Asubuhi wakaitana.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ
Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!
アラビア語 クルアーン注釈:
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali tumenyimwa!
アラビア語 クルアーン注釈:
قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
アラビア語 クルアーン注釈:
قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
アラビア語 クルアーン注釈:
قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
アラビア語 クルアーン注釈:
عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lililo bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
アラビア語 クルアーン注釈:
كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Hakika wacha Mungu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
アラビア語 クルアーン注釈:
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Mna nini? Mnahukumu vipi?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Kuwa mtapata humo mnayoyapenda?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayojihukumia?
アラビア語 クルアーン注釈:
سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
アラビア語 クルアーン注釈:
يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ
Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza
アラビア語 クルアーン注釈:
خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ وَقَدۡ كَانُواْ يُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمۡ سَٰلِمُونَ
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipokuwa wazima.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَذَرۡنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِۖ سَنَسۡتَدۡرِجُهُم مِّنۡ حَيۡثُ لَا يَعۡلَمُونَ
Basi niache na wanaokadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kutokea mahali wasipopajua.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَأُمۡلِي لَهُمۡۚ إِنَّ كَيۡدِي مَتِينٌ
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
アラビア語 クルアーン注釈:
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
アラビア語 クルアーン注釈:
أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
アラビア語 クルアーン注釈:
فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ
Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angelitupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَيُزۡلِقُونَكَ بِأَبۡصَٰرِهِمۡ لَمَّا سَمِعُواْ ٱلذِّكۡرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجۡنُونٞ
Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanaposikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 筆章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - ルゥワード翻訳事業センター - 対訳の目次

ルゥワード翻訳事業センターとラブワ招待協会およびイスラームコンテンツサービス協会の共訳

閉じる