Check out the new design

د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - د رواد الترجمې مرکز * - د ژباړو فهرست (لړلیک)


د معناګانو ژباړه سورت: قلم   آیت:

Al-Qalam

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ
Nuun. Ninaapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.
عربي تفسیرونه:
مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
عربي تفسیرونه:
وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyokatika.
عربي تفسیرونه:
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ
Na hakika wewe una tabia tukufu.
عربي تفسیرونه:
فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ
Karibu utaona, na wao wataona.
عربي تفسیرونه:
بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ
Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.
عربي تفسیرونه:
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliyeipotea Njia yake, na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.
عربي تفسیرونه:
فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ
Basi usiwatii wanaokadhibisha.
عربي تفسیرونه:
وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ
Wanatamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.
عربي تفسیرونه:
وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ
Wala usimtii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa.
عربي تفسیرونه:
هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ
Mtapitapi, apitaye akifitini.
عربي تفسیرونه:
مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ
Mwenye kuzuia mno heri, dhalimu, mwingi wa madhambi.
عربي تفسیرونه:
عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
عربي تفسیرونه:
أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
عربي تفسیرونه:
إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Anaposomewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uongo za watu wa zamani!
عربي تفسیرونه:
سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
عربي تفسیرونه:
إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyowajaribu wale wenye shamba, walipoapa kwamba watayavuna mazao yake itakapokuwa asubuhi.
عربي تفسیرونه:
وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
عربي تفسیرونه:
فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
عربي تفسیرونه:
فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ
Likawa kama usiku wa giza.
عربي تفسیرونه:
فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ
Asubuhi wakaitana.
عربي تفسیرونه:
أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
عربي تفسیرونه:
فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana.
عربي تفسیرونه:
أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
عربي تفسیرونه:
وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
عربي تفسیرونه:
فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ
Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!
عربي تفسیرونه:
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali tumenyimwa!
عربي تفسیرونه:
قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
عربي تفسیرونه:
قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
عربي تفسیرونه:
فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
عربي تفسیرونه:
قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
عربي تفسیرونه:
عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lililo bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
عربي تفسیرونه:
كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
عربي تفسیرونه:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Hakika wacha Mungu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
عربي تفسیرونه:
أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
عربي تفسیرونه:
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Mna nini? Mnahukumu vipi?
عربي تفسیرونه:
أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
عربي تفسیرونه:
إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Kuwa mtapata humo mnayoyapenda?
عربي تفسیرونه:
أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayojihukumia?
عربي تفسیرونه:
سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
عربي تفسیرونه:
أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
عربي تفسیرونه:
يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ
Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza
عربي تفسیرونه:
خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ وَقَدۡ كَانُواْ يُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمۡ سَٰلِمُونَ
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipokuwa wazima.
عربي تفسیرونه:
فَذَرۡنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِۖ سَنَسۡتَدۡرِجُهُم مِّنۡ حَيۡثُ لَا يَعۡلَمُونَ
Basi niache na wanaokadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kutokea mahali wasipopajua.
عربي تفسیرونه:
وَأُمۡلِي لَهُمۡۚ إِنَّ كَيۡدِي مَتِينٌ
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
عربي تفسیرونه:
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
عربي تفسیرونه:
أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
عربي تفسیرونه:
فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
عربي تفسیرونه:
لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ
Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angelitupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
عربي تفسیرونه:
فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
عربي تفسیرونه:
وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَيُزۡلِقُونَكَ بِأَبۡصَٰرِهِمۡ لَمَّا سَمِعُواْ ٱلذِّكۡرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجۡنُونٞ
Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanaposikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
عربي تفسیرونه:
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
عربي تفسیرونه:
 
د معناګانو ژباړه سورت: قلم
د سورتونو فهرست (لړلیک) د مخ نمبر
 
د قرآن کریم د معناګانو ژباړه - سواحلي ژباړه - د رواد الترجمې مرکز - د ژباړو فهرست (لړلیک)

دا ژباړه د مرکز رواد الترجمة ټیم لخوا د ربوہ د تبلیغ ټولنې او د اسلامي منځپانګې د خدماتو ټولنې په همکارۍ شوې.

بندول