Check out the new design

அல்குர்ஆன் மொழிபெயர்ப்பு - சுவாஹிலி மொழிபெயர்ப்பு - மொழிபெயர்ப்பு முன்னோடிகள் மையம் * - மொழிபெயர்ப்பு அட்டவணை


மொழிபெயர்ப்பு அத்தியாயம்: அல்கலம்   வசனம்:

Al-Qalam

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ
Nuun. Ninaapa kwa kalamu na yale wayaandikayo.
அரபு விரிவுரைகள்:
مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyokatika.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ
Na hakika wewe una tabia tukufu.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ
Karibu utaona, na wao wataona.
அரபு விரிவுரைகள்:
بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ
Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.
அரபு விரிவுரைகள்:
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliyeipotea Njia yake, na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ
Basi usiwatii wanaokadhibisha.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ
Wanatamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ
Wala usimtii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa.
அரபு விரிவுரைகள்:
هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ
Mtapitapi, apitaye akifitini.
அரபு விரிவுரைகள்:
مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ
Mwenye kuzuia mno heri, dhalimu, mwingi wa madhambi.
அரபு விரிவுரைகள்:
عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
அரபு விரிவுரைகள்:
أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
அரபு விரிவுரைகள்:
إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Anaposomewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uongo za watu wa zamani!
அரபு விரிவுரைகள்:
سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
அரபு விரிவுரைகள்:
إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyowajaribu wale wenye shamba, walipoapa kwamba watayavuna mazao yake itakapokuwa asubuhi.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
அரபு விரிவுரைகள்:
فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
அரபு விரிவுரைகள்:
فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ
Likawa kama usiku wa giza.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ
Asubuhi wakaitana.
அரபு விரிவுரைகள்:
أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana.
அரபு விரிவுரைகள்:
أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ
Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!
அரபு விரிவுரைகள்:
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali tumenyimwa!
அரபு விரிவுரைகள்:
قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
அரபு விரிவுரைகள்:
قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
அரபு விரிவுரைகள்:
قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
அரபு விரிவுரைகள்:
عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lililo bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
அரபு விரிவுரைகள்:
كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
அரபு விரிவுரைகள்:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Hakika wacha Mungu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
அரபு விரிவுரைகள்:
أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
அரபு விரிவுரைகள்:
مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Mna nini? Mnahukumu vipi?
அரபு விரிவுரைகள்:
أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
அரபு விரிவுரைகள்:
إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
Kuwa mtapata humo mnayoyapenda?
அரபு விரிவுரைகள்:
أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayojihukumia?
அரபு விரிவுரைகள்:
سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
அரபு விரிவுரைகள்:
أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
அரபு விரிவுரைகள்:
يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ
Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza
அரபு விரிவுரைகள்:
خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ وَقَدۡ كَانُواْ يُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمۡ سَٰلِمُونَ
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipokuwa wazima.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَذَرۡنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِۖ سَنَسۡتَدۡرِجُهُم مِّنۡ حَيۡثُ لَا يَعۡلَمُونَ
Basi niache na wanaokadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kutokea mahali wasipopajua.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَأُمۡلِي لَهُمۡۚ إِنَّ كَيۡدِي مَتِينٌ
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
அரபு விரிவுரைகள்:
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
அரபு விரிவுரைகள்:
أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
அரபு விரிவுரைகள்:
فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
அரபு விரிவுரைகள்:
لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ
Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angelitupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَيُزۡلِقُونَكَ بِأَبۡصَٰرِهِمۡ لَمَّا سَمِعُواْ ٱلذِّكۡرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجۡنُونٞ
Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanaposikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
அரபு விரிவுரைகள்:
 
மொழிபெயர்ப்பு அத்தியாயம்: அல்கலம்
அத்தியாயங்களின் அட்டவணை பக்க எண்
 
அல்குர்ஆன் மொழிபெயர்ப்பு - சுவாஹிலி மொழிபெயர்ப்பு - மொழிபெயர்ப்பு முன்னோடிகள் மையம் - மொழிபெயர்ப்பு அட்டவணை

அர்ருவ்வாத் மொழிபெயர்ப்பு மையத்தின் குழு அல்-ரப்வா அழைப்பு சங்கம் மற்றும் பல் மொழிகளில் இஸ்லாமிய உள்ளடக்கத்திற்கு சேவை செய்யும் சங்கத்துடன் இணைந்து மொழிபெயர்த்துள்ளது.

மூடுக