Wala wamchao Mungu hawana jukumu lolote kwao, lakini ni kukumbusha, asaa wapate kujiepusha. [69]
[69] Na wenye kumcha Mwenyezi Mungu hawana dhambi katika dhambi za hawa madhaalimu, ikiwa wataendelea na upotovu wao. Lakini yapasa kuwasemeza na kuwakumbusha, asaa huenda wakaiogopa adhabu ya Mwenyezi Mungu, na wakaacha upotovu.
Waachilie mbali walio ifanya dini yao ni mchezo na pumbao, na uhai wa dunia ukawaghuri. Nawe kumbusha kwayo, isije nafsi ikaangamizwa kwa sababu ya iliyo yachuma, nayo haina mlinzi wala mwombezi ila Mwenyezi Mungu. Na ingatoa kila fidia haitokubaliwa. Hao ndio walio angamizwa kwa sababu ya yale waliyo yachuma. Wao watapata kinywaji cha maji ya moto kabisa, na adhabu chungu. [70]
[70] Na ewe Nabii, waachilie mbali wale walio fanya sharia yao, mwendo wao, pumbao na mchezo, na wakakhadaika na maisha ya dunia wakaacha ya Akhera. Na daima kumbusha kwa Qur'ani, na wahadharishe vitisho vya Siku ambayo nafsi itafungika na a'mali yake, itapo kuwa hapana wa kunusuru wala wa kusaidia isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Na kila fidia ya kujiokoa haitokubaliwa. Hao makafiri watafungwa katika adhabu kwa sababu ya shari waliyo itenda. Katika Jahannamu watapewa kinywaji kimoto mwisho wa umoto, na adhabu chungu mno kwa sababu ya kufuru zao.
Sema: Je, tumuombe asiye kuwa Mwenyezi Mungu ambae hatufai wala hatudhuru, na turejee nyuma baada ya Mwenyezi Mungu kwisha tuhidi? Tuwe kama ambao mashet'ani wamempumbaza katika ardhi, amebabaika? Anao marafiki wanao mwita ende kwenye uwongofu, wakimwambia: Njoo kwetu! Sema: Hakika uwongofu wa Mwenyezi Mungu ndio Uwongofu. Nasi tumeamrishwa tusilimu kwa Mola Mlezi wa viumbe vyote, [71]
[71] Waambie hawa makafiri kwa kuwasibabi: Je, inasihi kuwa tumuabudu asiye kuwa Mwenyezi Mungu, asiye weza kutuletea nafuu wala dhara? Na turejee kwenye shirki baada ya kuwa Mwenyezi Mungu kesha tupa tawfiqi ya kufikia Imani? Na tuwe kama aliye zugwa na mashetani na wakampoteza katika ardhi, akawa yuko katika pweleo lisilo weza kumwongoa kufuata Njia iliyo nyooka, na hali anao marafiki walio ongoka nao wanajaribu kumwokoa atoke kwenye upotofu, huku wakisema: Rejea kwenye njia yetu iliyo sawa; naye akawa hawaitikii!! Sema ewe Nabii: Hakika Uislamu ndio uwongofu na ndio uwongozi, na vyenginevyo ni upotofu tu. Na Mwenyezi Mungu ametuamrisha tuufuate Uislamu. Naye ndiye Muumba wa viumbe vyote, na ndiye Mwenye kuviruzuku, na Mwenye kupanga mambo yao.
Na mshike Swala, na mcheni Yeye, na kwake Yeye ndiko mtako kusanywa. [72]
[72] Waachilieni mbali hao washirikina baada ya kuwa mmewaita kwenye uwongofu, na nendeni kwenye ibada ya Mola wenu Mlezi. Na timizeni SWala kwa njia ya unyenyekevu ulio kamilika kabisa. Na mkhofuni Mwenyezi Mungu, na timizeni amri zake. Kwani kwake Yeye ndio mtakusanywa nyote nyinyi.
Naye ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi kwa Haki. Na anaposema: Kuwa! Basi huwa. Kauli yake ni Haki. Na ufalme wote ni wake Siku litapo pulizwa barugumu, Mjuzi wa yaliyo fichikana na yanayo onekana. Naye ndiye Mwenye hikima na Mwenye khabari. [73]
[73] Na ni Mwenyezi Mungu peke yake ndiye aliye ziumba mbingu na ardhi, na akasimamia uumbaji wake kwa Haki na hikima. Na wakati wowote Mwenyezi Mungu akitaka kiwe kitu kinakuwa papo hapo. Vitu huwa kwa neno: "Kuwa". Na kila neno lake ni la kweli na la haki. Na Yeye peke yake ndiye Mwenye uweza wa kutenda usio na ukomo Siku ya Kiyama, siku litapo pulizwa barugumu la kutangazwa ufufuo. Naye, Subhanahu, ndiye Mwenye kutulia juu ya ujuzi wake wa mambo yaliyo fichikana na yanayo onekana. Na ndiye anaye endesha mambo yake yote kwa hikima, na ndiye Mwenye kukusanya katika ujuzi wake mambo yaliyo fichikana na mambo yaliyo dhihiri.
Contents of the translations can be downloaded and re-published, with the following terms and conditions:
1. No modification, addition, or deletion of the content.
2. Clearly referring to the publisher and the source (QuranEnc.com).
3. Mentioning the version number when re-publishing the translation.
4. Keeping the transcript information inside the document.
5. Notifying the source (QuranEnc.com) of any note on the translation.
6. Updating the translation according to the latest version issued from the source (QuranEnc.com).
7. Inappropriate advertisements must not be included when displaying translations of the meanings of the Noble Quran.
លទ្ធផលស្វែងរក:
API specs
Endpoints:
Sura translation
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/sura/{translation_key}/{sura_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified sura (by its number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114)
Returns:
json object containing array of objects, each object contains the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".
GET / https://quranenc.com/api/v1/translation/aya/{translation_key}/{sura_number}/{aya_number} description: get the specified translation (by its translation_key) for the speicified aya (by its number sura_number and aya_number)
Parameters: translation_key: (the key of the currently selected translation) sura_number: [1-114] (Sura number in the mosshaf which should be between 1 and 114) aya_number: [1-...] (Aya number in the sura)
Returns:
json object containing the "sura", "aya", "translation" and "footnotes".