Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis * - Vertimų turinys


Reikšmių vertimas Sūra: Sūra An-Naba’   Aja (Korano eilutė):

Surat An-Naba

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ
Kuhusu kitu gani baadhi ya makafiri wa Kikureshi wanaulizana?
Tafsyrai arabų kalba:
عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ
Wanaulizana kuhusu habari iliyo na uzito mkubwa kabisa,
Tafsyrai arabų kalba:
ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ
nayo ni Qur’ani tukufu inayotoa habari za kufufuliwa ambako makafiri wa Kikureshi wana shaka nako na wanakukanusha.
Tafsyrai arabų kalba:
كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Mambo sivyo kama wanavyodhania hawa washirikina. Hapo watajua hawa washirikina upeo wa kukanusha kwao na kitawadhihirikia waziwazi kile Atakachowatenda Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama.
Tafsyrai arabų kalba:
ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ
Kisha litahakikishika kwao jambo hilo na utahakikishika kwao ukweli wa yale aliyokuja nayo Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kuhusu Qur’ani na kufufuliwa. Huu ni utisho na makemeo kwao.
Tafsyrai arabų kalba:
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا
Kwani hatukuwatandazia ardhi kama tandiko?
Tafsyrai arabų kalba:
وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا
Na Tukawafanyia majabali kuwa ni vigingi, ili isitisike nanyi?
Tafsyrai arabų kalba:
وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا
Na Tukawaumba aina mbali-mbali, mume na mke.
Tafsyrai arabų kalba:
وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا
Na Tukafanya usingizi wenu ni mapumziko kwa viwiliwili vyenu: ndani yake mnatulia na kupumzika?
Tafsyrai arabų kalba:
وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا
Na Tukaufanya usiku kuwa ni vazi, unawavisha giza lake na kuwafinika, kama nguo inavyomsitiri mwenye kuivaa.
Tafsyrai arabų kalba:
وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا
Na Tukaufanya mchana ni kipindi cha kutafuta maisha, mnaenea humo kwa ajili ya maisha yenu na mnatembea humo kwa ajili ya maslahi yenu?
Tafsyrai arabų kalba:
وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا
Na Tukajenga juu yenu mbingu saba, madhubuti jengo lake, lilioumbwa kwa uzuri, halina mapasuko wala nyufa?
Tafsyrai arabų kalba:
وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا
Na Tukalifanya jua kuwa ni taa iwakayo na kung’ara?
Tafsyrai arabų kalba:
وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا
Na Tukateremsha kutoka kwenye mawingu yanyeshayo maji yamiminikayo kwa wingi,
Tafsyrai arabų kalba:
لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا
ili Tutoe kwa maji hayo nafaka inayoliwa na watu,
Tafsyrai arabų kalba:
وَجَنَّٰتٍ أَلۡفَافًا
nyasi zinazoliwa na wanyama na miti iliyosongamana kwa kutawanyika tagaa zake?
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا
Hakika Siku ya Uamuzi kati ya viumbe,
Tafsyrai arabų kalba:
يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا
nayo ni Siku ya Kiyama, imekuwa ni wakati na ahadi iliyowekewa muda maalimu kwa watu wa mwanzo na wa mwisho.
Tafsyrai arabų kalba:
وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا
Na zikafunguliwa mbingu zikawa ni zenye milango mingi kwa ajili ya kuteremka Malaika.
Tafsyrai arabų kalba:
وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا
Na yakalipuliwa majabali baada ya kuwa yamekita, yakawa ni kama mangati.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا
Hakika Jahanamu, Siku Hiyo, itawalindiza wenye ukafiri ambao Moto huo umeandaliwa wao.
Tafsyrai arabų kalba:
لِّلطَّٰغِينَ مَـَٔابٗا
Kwa makafiri ndio marejeo.
Tafsyrai arabų kalba:
لَّٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا
Watabakia humo muda mrefu ufuatanao, usiokoma.
Tafsyrai arabų kalba:
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا
Hawatakula humo chochote kitakachozizimisha joto la moto kwao.
Tafsyrai arabų kalba:
إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا
Wala kinywaji kitakachowaondolea kiu yao. Isipokuwa maji moto na usaha wa watu wa motoni.
Tafsyrai arabų kalba:
جَزَآءٗ وِفَاقًا
Watakuwa wanalipwa kwa hilo malipo ya sawa yanayolingana na vitendo vyao walivyovitenda duniani
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا
Hakika wao walikuwa hawaiyogopi Siku ya Hesabu, na kwa hivyo hawakujitayarisha nayo kwa kufanya matendo ya kuwafaa.
Tafsyrai arabų kalba:
وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا
Na waliyakanusha waziwazi yaliyoletwa na Mitume.
Tafsyrai arabų kalba:
وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا
Na kila kitu Tulikijua na Tukakiandika katika Ubao uliohifadhiwa (Al-Lawḥ Al-Maḥfūd).
Tafsyrai arabų kalba:
فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا
Basi Onjeni, enyi makafiri, hayo yakiwa ni malipo ya vitendo vyenu, Hatutawazidishia isipokuwa adhabu juu ya adhabu yenu.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا
Hakika kwa wale ambao wanamuogopa Mola wao na huku wanatenda mema kuna kufaulu kwa kuingia Peponi.
Tafsyrai arabų kalba:
حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا
Hakika watapata Mabustani makubwa na zabibu.
Tafsyrai arabų kalba:
وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا
Na watapata wanawake wenye umri mdogo, wenye vifua vilivyojaza, marika na waume zao.
Tafsyrai arabų kalba:
وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا
Na watapata glasi zlizojaa pombe.
Tafsyrai arabų kalba:
لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّٰبٗا
Hawatasikia katika Pepo hiyo maneno ya upotofu wala kudanganyana.
Tafsyrai arabų kalba:
جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا
Watayapata yote hayo yakiwa ni malipo na zawadi na kipewa kingi cha kuwatosha kutoka kwa Mwenyezi Mungu,
Tafsyrai arabų kalba:
رَّبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا ٱلرَّحۡمَٰنِۖ لَا يَمۡلِكُونَ مِنۡهُ خِطَابٗا
Mola wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati ya hizo, Mwenye kuwarehemu duniani na Akhera. Hawataweza kumuomba isipokuwa kile walichopewa ruhusa kumuomba.
Tafsyrai arabų kalba:
يَوۡمَ يَقُومُ ٱلرُّوحُ وَٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ صَفّٗاۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنۡ أَذِنَ لَهُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وَقَالَ صَوَابٗا
Siku atakaposimama Jibrili na Malaika wengine hali ya kujipanga mlolongo. Hawatamuombea isipokuwa yule aliyetolewa ruhusa na Mwingi wa Rehema ya kuombewa na akasema maneno ya haki na ya sawa.
Tafsyrai arabų kalba:
ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمُ ٱلۡحَقُّۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ مَـَٔابًا
Hiyo ndiyo siku ya haki isiyokuwa na shaka kuja kwake. Kwa hivyo, yule atakaye kuokoka na vituko vya Siku hiyo, na ajifanyie njia ya marejeo kwa Mola wake kutenda vitendo vyema.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّآ أَنذَرۡنَٰكُمۡ عَذَابٗا قَرِيبٗا يَوۡمَ يَنظُرُ ٱلۡمَرۡءُ مَا قَدَّمَتۡ يَدَاهُ وَيَقُولُ ٱلۡكَافِرُ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ تُرَٰبَۢا
Sisi Tunawaonya nyinyi adhabu ya Siku ya mwisho iliyo karibu. Siku ambayo atayaona kila mtu aliyoyatenda katika kheri au aliyoyachuma miongoni mwa madhambi. Na kafiri atasema, kwa kitisho cha Hesabu, «Laiti mimi nilikuwa mchanga na sikufufuliwa.»
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Sūra: Sūra An-Naba’
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Abdullah Muchammed ir Naser Khamis - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Dr. Abdullah Muchammed Abu Bakr ir šeichas Naser Khamis.

Uždaryti