Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Ali Muchsen Al-Beruany * - Vertimų turinys

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Al-Muddassir   Aja (Korano eilutė):

Surat Al-Muddathir

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ
Ewe uliye jigubika!
Tafsyrai arabų kalba:
قُمۡ فَأَنذِرۡ
Simama uonye!
Tafsyrai arabų kalba:
وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
Tafsyrai arabų kalba:
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ
Na nguo zako, zisafishe.
Tafsyrai arabų kalba:
وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ
Na yaliyo machafu yahame!
Tafsyrai arabų kalba:
وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
Tafsyrai arabų kalba:
وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
Tafsyrai arabų kalba:
فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ
Basi litapo pulizwa barugumu,
Tafsyrai arabų kalba:
فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
Tafsyrai arabų kalba:
عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
Tafsyrai arabų kalba:
ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا
Niache peke yangu na niliye muumba;
Tafsyrai arabų kalba:
وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
Tafsyrai arabų kalba:
وَبَنِينَ شُهُودٗا
Na wana wanao onekana,
Tafsyrai arabų kalba:
وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
Tafsyrai arabų kalba:
ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ
Kisha anatumai nimzidishie!
Tafsyrai arabų kalba:
كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
Tafsyrai arabų kalba:
سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
Tafsyrai arabų kalba:
فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
Tafsyrai arabų kalba:
ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
Tafsyrai arabų kalba:
ثُمَّ نَظَرَ
Kisha akatazama,
Tafsyrai arabų kalba:
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
Tafsyrai arabų kalba:
ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
Tafsyrai arabų kalba:
فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
Tafsyrai arabų kalba:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
Tafsyrai arabų kalba:
سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
Tafsyrai arabų kalba:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
Tafsyrai arabų kalba:
لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ
Haubakishi wala hausazi.
Tafsyrai arabų kalba:
لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ
Unababua ngozi iwe nyeusi.
Tafsyrai arabų kalba:
عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ
Juu yake wapo kumi na tisa.
Tafsyrai arabų kalba:
وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
Tafsyrai arabų kalba:
كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ
Hasha! Naapa kwa mwezi!
Tafsyrai arabų kalba:
وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ
Na kwa usiku unapo kucha!
Tafsyrai arabų kalba:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
Tafsyrai arabų kalba:
إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
Tafsyrai arabų kalba:
نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ
Ni onyo kwa binaadamu,
Tafsyrai arabų kalba:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
Tafsyrai arabų kalba:
كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
Tafsyrai arabų kalba:
إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ
Isipo kuwa watu wa kuliani.
Tafsyrai arabų kalba:
فِي جَنَّٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
Tafsyrai arabų kalba:
عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Khabari za wakosefu:
Tafsyrai arabų kalba:
مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
Tafsyrai arabų kalba:
قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakiswali.
Tafsyrai arabų kalba:
وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
Tafsyrai arabų kalba:
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
Tafsyrai arabų kalba:
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
Tafsyrai arabų kalba:
حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ
Mpaka yakini ilipo tufikia.
Tafsyrai arabų kalba:
فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّٰفِعِينَ
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
Tafsyrai arabų kalba:
فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
Tafsyrai arabų kalba:
كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
Tafsyrai arabų kalba:
فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ
Wanao mkimbia simba!
Tafsyrai arabų kalba:
بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
Tafsyrai arabų kalba:
كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
Tafsyrai arabų kalba:
كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
Tafsyrai arabų kalba:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye taka atakumbuka.
Tafsyrai arabų kalba:
وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
Tafsyrai arabų kalba:
 
Reikšmių vertimas Sūra: Sūra Al-Muddassir
Sūrų turinys Puslapio numeris
 
Kilniojo Korano reikšmių vertimas - Suahilių k. vertimas - Ali Muchsen Al-Beruany - Vertimų turinys

Kilniojo Korano reikšmių vertimas į suahilių k., išvertė Ali Muchsin Al-Birvany.

Uždaryti