அல்குர்ஆன் மொழிபெயர்ப்பு - சுவாஹிலி மொழிபெயர்ப்பு- அலி முஃசின் bபிர்வானி * - மொழிபெயர்ப்பு அட்டவணை

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

மொழிபெயர்ப்பு அத்தியாயம்: ஸூரா அல்முத்தஸ்ஸிர்   வசனம்:

Surat Al-Muddathir

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ
Ewe uliye jigubika!
அரபு விரிவுரைகள்:
قُمۡ فَأَنذِرۡ
Simama uonye!
அரபு விரிவுரைகள்:
وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
அரபு விரிவுரைகள்:
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ
Na nguo zako, zisafishe.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ
Na yaliyo machafu yahame!
அரபு விரிவுரைகள்:
وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
அரபு விரிவுரைகள்:
فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ
Basi litapo pulizwa barugumu,
அரபு விரிவுரைகள்:
فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
அரபு விரிவுரைகள்:
عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
அரபு விரிவுரைகள்:
ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا
Niache peke yangu na niliye muumba;
அரபு விரிவுரைகள்:
وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
அரபு விரிவுரைகள்:
وَبَنِينَ شُهُودٗا
Na wana wanao onekana,
அரபு விரிவுரைகள்:
وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
அரபு விரிவுரைகள்:
ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ
Kisha anatumai nimzidishie!
அரபு விரிவுரைகள்:
كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
அரபு விரிவுரைகள்:
سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
அரபு விரிவுரைகள்:
إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
அரபு விரிவுரைகள்:
ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
அரபு விரிவுரைகள்:
ثُمَّ نَظَرَ
Kisha akatazama,
அரபு விரிவுரைகள்:
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
அரபு விரிவுரைகள்:
ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
அரபு விரிவுரைகள்:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
அரபு விரிவுரைகள்:
سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
அரபு விரிவுரைகள்:
لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ
Haubakishi wala hausazi.
அரபு விரிவுரைகள்:
لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ
Unababua ngozi iwe nyeusi.
அரபு விரிவுரைகள்:
عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ
Juu yake wapo kumi na tisa.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ
Na hatukuwafanya walinzi wa Motoni ila ni Malaika, wala hatukuifanya idadi yao hiyo ila kuwatatanisha walio kufuru, wapate kuwa na yakini walio pewa Kitabu, na wazidi Imani wale walio amini, wala wasiwe na shaka walio pewa Kitabu na Waumini, na wapate kusema wenye maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humwacha apotee amtakaye, na humwongoa amtakaye. Na hapana yeyote anaye jua majeshi ya Mola wako Mlezi ila Yeye tu. Na haya si chochote ila ni ukumbusho kwa binaadamu.
அரபு விரிவுரைகள்:
كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ
Hasha! Naapa kwa mwezi!
அரபு விரிவுரைகள்:
وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ
Na kwa usiku unapo kucha!
அரபு விரிவுரைகள்:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ
Na kwa asubuhi inapo pambazuka!
அரபு விரிவுரைகள்:
إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ
Hakika huo Moto ni katika mambo yaliyo makubwa kabisa!
அரபு விரிவுரைகள்:
نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ
Ni onyo kwa binaadamu,
அரபு விரிவுரைகள்:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ
Kwa anaye taka miongoni mwenu kutangulia au kuchelewa.
அரபு விரிவுரைகள்:
كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ
Kila nafsi imo rahanini kwa mabaya iliyo yachuma.
அரபு விரிவுரைகள்:
إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ
Isipo kuwa watu wa kuliani.
அரபு விரிவுரைகள்:
فِي جَنَّٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ
Hao watakuwa katika Mabustani, wawe wanaulizana
அரபு விரிவுரைகள்:
عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Khabari za wakosefu:
அரபு விரிவுரைகள்:
مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ
Ni nini kilicho kupelekeni Motoni?
அரபு விரிவுரைகள்:
قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ
Waseme: Hatukuwa miongoni walio kuwa wakiswali.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ
Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ
Na tulikuwa tukizama pamoja na walio zama katika maovu.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na tulikuwa tukiikanusha siku ya malipo.
அரபு விரிவுரைகள்:
حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ
Mpaka yakini ilipo tufikia.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّٰفِعِينَ
Basi hautawafaa kitu uombezi wa waombezi.
அரபு விரிவுரைகள்:
فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ
Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?
அரபு விரிவுரைகள்:
كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ
Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,
அரபு விரிவுரைகள்:
فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ
Wanao mkimbia simba!
அரபு விரிவுரைகள்:
بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ
Ati kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo funuliwa.
அரபு விரிவுரைகள்:
كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Hasha! Kwani wao hawaiogopi Akhera?
அரபு விரிவுரைகள்:
كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ
Hasha! Kwa hakika huu ni ukumbusho!
அரபு விரிவுரைகள்:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anaye taka atakumbuka.
அரபு விரிவுரைகள்:
وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ
Na hawatakumbuka isipo kuwa Mwenyezi Mungu atake. Uchamngu ni kwake Yeye, na msamaha ni wake Yeye.
அரபு விரிவுரைகள்:
 
மொழிபெயர்ப்பு அத்தியாயம்: ஸூரா அல்முத்தஸ்ஸிர்
அத்தியாயங்களின் அட்டவணை பக்க எண்
 
அல்குர்ஆன் மொழிபெயர்ப்பு - சுவாஹிலி மொழிபெயர்ப்பு- அலி முஃசின் bபிர்வானி - மொழிபெயர்ப்பு அட்டவணை

புனித அல் குர்ஆனுக்கான சுவாஹிலி மொழிபெயர்ப்பு- அலி முஃசின் பிர்வானி மூலம் மொழிபெயர்க்கப்பட்டது

மூடுக