Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani * - Index van vertaling

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Vertaling van de betekenissen Surah: Soerat Al-Fiel (De Olifant)   Vers:

Surat Al-Fil

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصۡحَٰبِ ٱلۡفِيلِ
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?
Hakika, ewe Muhammad, unajua kwa ujuzi usio ingiliwa na shaka yoyote, alivyo fanya Mola wako Mlezi kuwafanyia wale watu wenye tembo (ndovu), wakataka kuishambulia Nyumba takatifu ya Al-Kaaba.
Arabische uitleg van de Qur'an:
أَلَمۡ يَجۡعَلۡ كَيۡدَهُمۡ فِي تَضۡلِيلٖ
Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
Unajua ya kwamba hakika Mwenyezi Mungu amejaalia juhudi yao kutaka kuibomoa Al-Kaaba ivize na ipotelee mbali. Juhudi yao ikapeperuka, na wao wasipate makusudio yao.
Arabische uitleg van de Qur'an:
وَأَرۡسَلَ عَلَيۡهِمۡ طَيۡرًا أَبَابِيلَ
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,
Na Mwenyezi Mungu aliwasalitisha na majeshi ya ndege yaliyo watokea makundi kwa makundi yakifuatana, na yakawazunguka kila upande.
Arabische uitleg van de Qur'an:
تَرۡمِيهِم بِحِجَارَةٖ مِّن سِجِّيلٖ
Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,
Wakiwatupia mawe kutoka Jahannamu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
فَجَعَلَهُمۡ كَعَصۡفٖ مَّأۡكُولِۭ
Akawafanya kama majani yaliyo liwa!
Akawafanya kama majani ya mimea yaliyo sibiwa yakatilifu.
Arabische uitleg van de Qur'an:
 
Vertaling van de betekenissen Surah: Soerat Al-Fiel (De Olifant)
Surah's Index Pagina nummer
 
Vertaling van de betekenissen Edele Qur'an - Kiswahili vertaling - Ali Mohsin Al-Barwani - Index van vertaling

Vertaling van de betekenissen van de Heilige Koran naar het Swahili, vertaald door Ali Mohsin Al-Barwani.

Sluit