Check out the new design

ශුද්ධවූ අල් කුර්ආන් අර්ථ කථනය - ස්වහීලී පරිවර්තනය - අබ්දුල්ලා මුහම්මද් සහ නාසර් ඛමීස් * - පරිවර්තන පටුන


අර්ථ කථනය පරිච්ඡේදය: අස් සාෆ්ෆාත්   වාක්‍යය:

As-Saffat

وَٱلصَّٰٓفَّٰتِ صَفّٗا
Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anaapa kwa Malaika wanaojipanga, katika kuabudu kwao, mistari iliyofuatana na kushikana,
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
فَٱلزَّٰجِرَٰتِ زَجۡرٗا
na kwa Malaika wanaofukuza mawingu na kuyaongoza kwa amri ya MwenyeziMungu,
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
فَٱلتَّٰلِيَٰتِ ذِكۡرًا
na kwa Malaika wanaosoma utajo wa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na maneno Yake,
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
إِنَّ إِلَٰهَكُمۡ لَوَٰحِدٞ
kwamba muabudiwa wenu, enyi watu, ni Mmoja, Asiye na mshirika. Hivyo basi mtakasieni ibada na utiifu. Na Anaapa Mwenyezi Mungu kwa Anachotaka miongoni mwa viumbe Vyake. Ama kiumbe, hafai kuapa isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu, kwani kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَرَبُّ ٱلۡمَشَٰرِقِ
Yeye Ndiye Muumba mbingu na ardhi na vilivyoko baina ya hivyo viwili, na Ndiye Mpelekeshaji jua katika sehemu zake za kuchomozea na zile za kuchwea.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِزِينَةٍ ٱلۡكَوَاكِبِ
Sisi tumeupamba uwingu wa karibu kwa pambo la nyota.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَحِفۡظٗا مِّن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ مَّارِدٖ
Na tumeuhifadhi huo uwingu, kwa nyota, na kila shetani mwenye kuasi, mjeuri, aliyefukuzwa (kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu).
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰ وَيُقۡذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٖ
Hawawezi hao Mashetani kufika kwenye viumbe vya juu, navyo ni mbingu na Malaika waliyomo ndani yake, wakapata kuwasikiliza wanapoutamka wahyi ambao Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anauleta, unaokusanya sheria Yake na makadirio Yake, na wanavurumizwa vimondo katika kila upande,
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
دُحُورٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ وَاصِبٌ
kwa kuwafukuza ili wasipate kusikiliza. Na huko kwenye Nyumba ya Akhera watakuwa na adhabu ya daima yenye kuumiza.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
إِلَّا مَنۡ خَطِفَ ٱلۡخَطۡفَةَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ ثَاقِبٞ
Isipokuwa yule aliyenyakuwa, miongoni mwa Mashetani, mnyakuo wa haraka, nao ni lile neno analolisikia mbinguni kwa haraka, akamtupia aliyekuwa chini yake, na yule mwingine akamtupia aliyekuwa chini yake. Basi pengine huenda akafikiwa na kimondo chenye kutoa mwangaza kabla hajalitupa, na pengine huwa amelitupa kwa makadirio ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kabla ya kujiwa na kimondo kikamchoma, na yule mwingine akaenda nalo hadi kwa makuhani wakaongeza juu ya neno hilo maneno mia moja ya urongo.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَهُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَم مَّنۡ خَلَقۡنَآۚ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّن طِينٖ لَّازِبِۭ
Basi waulize, ewe Mtume, wenye kukanusha Kufufuliwa: Je kuumbwa kwao ni kugumu zaidi au ni hivyi viumbe tulivyoviumba? Kwa hakika, tulimuumba baba yao Ādam kwa udongo ulioshikana na kuambatana.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
بَلۡ عَجِبۡتَ وَيَسۡخَرُونَ
Bali ulistaajabu, ewe Mtume, kwa ukanushaji wao na kukataa kwao Kufufuliwa. Na la kustaajabiwa zaidi na lililo kubwa zaidi kuliko lile la kukataa kwao ni kwamba wao wanakucheza shere na kulidharau neno lako.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَإِذَا ذُكِّرُواْ لَا يَذۡكُرُونَ
Na wanapokumbushwa walichokisahau au walichoghafilika nacho, hawanufaiki kwa huo ukumbusho wala hawazingatii.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَإِذَا رَأَوۡاْ ءَايَةٗ يَسۡتَسۡخِرُونَ
Na wanapoiona miujiza yenye kutolea dalili unabii wako, wanakufanyia shere na wanastaajabu.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَقَالُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٌ
Na wanasema, «Halikuwa hili ulilotuletea isipokuwa ni uchawi uliojitokeza waziwazi.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
Je, tunapokufa na tukawa ni mchanga na mifupa iliyochakaa, je sisi ni wenye kufufuliwa kutoka makaburini mwetu tukiwa hai?
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ
au pia watafufuliwa baba zetu waliopita kabla yetu?»
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
قُلۡ نَعَمۡ وَأَنتُمۡ دَٰخِرُونَ
Waambie, ewe Mtume, «Ndio mtafufuliwa hali mkiwa wanyonge, watwevu.»
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ فَإِذَا هُمۡ يَنظُرُونَ
Hakika ni kwamba huo utakuwa ni Mvuvio mmoja, wakitahamaki wao wamesimama kutoka makaburini mwao, wanatazama vituko vya Kiyama.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَقَالُواْ يَٰوَيۡلَنَا هَٰذَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Na watasema, «Ewe maangamivu yetu! Hii ni siku ya kuhesabiwa na kulipwa!»
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ
Hapo wataambiwa, «Hii ndiyo Siku ya Uamuzi wa haki baina ya viumbe, ambayo mlikuwa mkiikanusha duniani na mkiikataa.»
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
۞ ٱحۡشُرُواْ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَأَزۡوَٰجَهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَعۡبُدُونَ
Na Malaika wataambiwa, «Wakusanyeni wale waliomkanusha Mwenyezi Mungu na wafananao na wao na waungu wao waliokuwa wakiwaabudu
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهۡدُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡجَحِيمِ
badala ya Mwenyezi Mungu, na muwasukume kwa nguvu hadi kwenye moto wa Jahanamu.
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
وَقِفُوهُمۡۖ إِنَّهُم مَّسۡـُٔولُونَ
«Na muwafunge kabla hawajafika kwenye moto wa Jahanamu, kwa kuwa wao ni wenye kuulizwa kuhusu matendo yao na maneno yao yaliyotokana na wao duniani, kwa namna ya kumshtukia kuwakaripia.»
අල්කුර්ආන් අරාබි අර්ථ විවරණ:
 
අර්ථ කථනය පරිච්ඡේදය: අස් සාෆ්ෆාත්
සූරා පටුන පිටු අංක
 
ශුද්ධවූ අල් කුර්ආන් අර්ථ කථනය - ස්වහීලී පරිවර්තනය - අබ්දුල්ලා මුහම්මද් සහ නාසර් ඛමීස් - පරිවර්තන පටුන

මෙය ආචාර්ය අබ්දුල්ලාහ් මුහම්මද් අබූ බක්ර් සහ අෂ්-ෂෙයික් නාසර් කමීස් විසින් පරිවර්තනය කරන ලදී.

වසන්න