Check out the new design

แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - ศูนย์การแปลรุว๊าด * - สารบัญ​คำแปล


แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Al-Hijr   อายะฮ์:

Al-hijr

الٓرۚ تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ وَقُرۡءَانٖ مُّبِينٖ
Alif Lam Ra.[1] Hizi ni Aya za Kitabu na Qur-ani inayobainisha.
[1] Herufi hizi "Alif Laam Raa" na herufi nyinginezo za mkato zilizo mwanzoni mwa sura mbalimbali zinaonyesha hali ya ushindi wa Qur-ani. Kwani, washirikina walipewa changamoto kwayo, lakini wakashindwa na hawakuweza kuipinga, ilhali inajumuisha herufi hizi zinazounda lugha ya Kiarabu. Kwa hivyo, kutoweza kwa Waarabu kuleta kitu kama hicho - ingawa walikuwa ndio watu wenye ufasaha zaidi - kunaonyesha kwamba Qur-ani ni ufunuo (wahyi) kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
رُّبَمَا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡ كَانُواْ مُسۡلِمِينَ
Huenda ikawa wale waliokufuru wakatamani kwamba wangekuwa Waislamu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ذَرۡهُمۡ يَأۡكُلُواْ وَيَتَمَتَّعُواْ وَيُلۡهِهِمُ ٱلۡأَمَلُۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ
Waache wale, na wastarehe, na yawazuge matumaini. Basi watakujajua.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا وَلَهَا كِتَابٞ مَّعۡلُومٞ
Na hatukuuangamiza mji wowote ule isipokuwa ulikuwa na muda wake maalumu ulioandikiwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
مَّا تَسۡبِقُ مِنۡ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ
Hawawezi umma wowote kuutangulia muda wao, wala kuchelewa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَقَالُواْ يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِي نُزِّلَ عَلَيۡهِ ٱلذِّكۡرُ إِنَّكَ لَمَجۡنُونٞ
Na walisema, "Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَّوۡمَا تَأۡتِينَا بِٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wakweli?"
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
مَا نُنَزِّلُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَمَا كَانُوٓاْ إِذٗا مُّنظَرِينَ
Sisi hatuwateremshi Malaika isipokuwa kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّا نَحۡنُ نَزَّلۡنَا ٱلذِّكۡرَ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَٰفِظُونَ
Hakika Sisi ndio tuliouteremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutakaoulinda.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ فِي شِيَعِ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na hakika tulikwishatuma Mitume kabla yako kwa mataifa ya mwanzo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Na hakuwajia Mtume yeyote isipokuwa walikuwa wakimfanyia stihizai.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَذَٰلِكَ نَسۡلُكُهُۥ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Na kama hivi ndivyo tunavyoyaingiza katika nyoyo za wahalifu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ وَقَدۡ خَلَتۡ سُنَّةُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Hawayaamini haya, na ilhali imekwishawapitia desturi ya wa mwanzo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَوۡ فَتَحۡنَا عَلَيۡهِم بَابٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ فَظَلُّواْ فِيهِ يَعۡرُجُونَ
Na lau tungeliwafungulia mlango huko mbinguni, wakawa wanapanda kupitia humo,
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَقَالُوٓاْ إِنَّمَا سُكِّرَتۡ أَبۡصَٰرُنَا بَلۡ نَحۡنُ قَوۡمٞ مَّسۡحُورُونَ
Basi wangelisema: Hakika macho yetu yameleweshwa tu. Bali sisi wenyewe ni kaumu tuliofanyiwa uchawi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَقَدۡ جَعَلۡنَا فِي ٱلسَّمَآءِ بُرُوجٗا وَزَيَّنَّٰهَا لِلنَّٰظِرِينَ
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَحَفِظۡنَٰهَا مِن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٍ
Na tumezilinda kutokana na kila shetani aliyelaaniwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّا مَنِ ٱسۡتَرَقَ ٱلسَّمۡعَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ مُّبِينٞ
Isipokuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kilicho dhahiri.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلۡأَرۡضَ مَدَدۡنَٰهَا وَأَلۡقَيۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ وَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ شَيۡءٖ مَّوۡزُونٖ
Na ardhi tumeitandaza, na humo tumeweka milima madhubuti, na tumeotesha ndani yake katika kila kitu kwa kiasi chake.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَجَعَلۡنَا لَكُمۡ فِيهَا مَعَٰيِشَ وَمَن لَّسۡتُمۡ لَهُۥ بِرَٰزِقِينَ
Na tumewafanyia humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِن مِّن شَيۡءٍ إِلَّا عِندَنَا خَزَآئِنُهُۥ وَمَا نُنَزِّلُهُۥٓ إِلَّا بِقَدَرٖ مَّعۡلُومٖ
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi isipokuwa kwa kipimo maalumu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَرۡسَلۡنَا ٱلرِّيَٰحَ لَوَٰقِحَ فَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَسۡقَيۡنَٰكُمُوهُ وَمَآ أَنتُمۡ لَهُۥ بِخَٰزِنِينَ
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayoyaweka.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّا لَنَحۡنُ نُحۡيِۦ وَنُمِيتُ وَنَحۡنُ ٱلۡوَٰرِثُونَ
Na hakika Sisi ndio tunaohuisha na tunaofisha. Na Sisi ndio Warithi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَقَدۡ عَلِمۡنَا ٱلۡمُسۡتَقۡدِمِينَ مِنكُمۡ وَلَقَدۡ عَلِمۡنَا ٱلۡمُسۡتَـٔۡخِرِينَ
Na hakika tunawajua waliotangulia katika nyinyi, na tunawajua waliobaki nyuma.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحۡشُرُهُمۡۚ إِنَّهُۥ حَكِيمٌ عَلِيمٞ
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakayewakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hekima, Mwenye kujua mno.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ
Na hakika tulimuumba Mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱلۡجَآنَّ خَلَقۡنَٰهُ مِن قَبۡلُ مِن نَّارِ ٱلسَّمُومِ
Naye Jini tulimuumba hapo kabla kutokana na moto wa upepo umoto.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِنِّي خَٰلِقُۢ بَشَرٗا مِّن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ
Na Mola wako Mlezi alipowaambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَإِذَا سَوَّيۡتُهُۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُواْ لَهُۥ سَٰجِدِينَ
Basi nitakapomtengeneza sawasawa, na nikampulizia roho yangu, basi angukeni kumsujudia.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَسَجَدَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ كُلُّهُمۡ أَجۡمَعُونَ
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّآ إِبۡلِيسَ أَبَىٰٓ أَن يَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ
Isipokuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na waliosujudu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ يَٰٓإِبۡلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na waliosujudu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ لَمۡ أَكُن لِّأَسۡجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقۡتَهُۥ مِن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ
Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliyemuumba kutokana na udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyotiwa sura.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٞ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umefukuziliwa mbali!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ عَلَيۡكَ ٱللَّعۡنَةَ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ
Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watakapofufuliwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ
(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika waliopewa muhula.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ
Mpaka siku ya wakati maalumu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ رَبِّ بِمَآ أَغۡوَيۡتَنِي لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ
Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyokuwa umenipoteza, basi hakika nitawapambia katika dunia na hakika nitawapoteza wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ
Isipokuwa waja wako walioteuliwa miongoni mwao.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ هَٰذَا صِرَٰطٌ عَلَيَّ مُسۡتَقِيمٌ
Akasema: Hii ni njia ya kujia kwangu iliyonyooka.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ عِبَادِي لَيۡسَ لَكَ عَلَيۡهِمۡ سُلۡطَٰنٌ إِلَّا مَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡغَاوِينَ
Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipokuwa wale wapotofu waliokufuata.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوۡعِدُهُمۡ أَجۡمَعِينَ
Na hakika Jahannamu ndipo mahali pao walipoahidiwa wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَهَا سَبۡعَةُ أَبۡوَٰبٖ لِّكُلِّ بَابٖ مِّنۡهُمۡ جُزۡءٞ مَّقۡسُومٌ
Ina milango saba; kila mlango ulitengewa sehemu miongoni mwao.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ
Hakika wachamungu watakuwa katika Mabustani na chemchemi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ٱدۡخُلُوهَا بِسَلَٰمٍ ءَامِنِينَ
(Wataambiwa:) Ingieni humo kwa salama na amani.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَنَزَعۡنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنۡ غِلٍّ إِخۡوَٰنًا عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ
Na tutaondoa chuki iliyokuwa vifuani mwao, wawe ndugu, juu ya viti vya kifahari huku wameelekeana.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَا يَمَسُّهُمۡ فِيهَا نَصَبٞ وَمَا هُم مِّنۡهَا بِمُخۡرَجِينَ
Humo hayatawagusa machovu, wala hawatatolewa humo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
۞ نَبِّئۡ عِبَادِيٓ أَنِّيٓ أَنَا ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ
Wape habari waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe zaidi, Mwingi wa kurehemu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَنَّ عَذَابِي هُوَ ٱلۡعَذَابُ ٱلۡأَلِيمُ
Na kwamba adhabu yangu ndiyo adhabu iliyo chungu!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَنَبِّئۡهُمۡ عَن ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ
Na wape habari za wageni wa Ibrahim.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمٗا قَالَ إِنَّا مِنكُمۡ وَجِلُونَ
Walipoingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunawaogopa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ لَا تَوۡجَلۡ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٖ
Wakasema: Usiogope. Hakika, Sisi tunakubashiria kijana mwenye elimu mno.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ أَبَشَّرۡتُمُونِي عَلَىٰٓ أَن مَّسَّنِيَ ٱلۡكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ
Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi ni kwa njia gani mnanibashiria?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ بَشَّرۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ ٱلۡقَٰنِطِينَ
Wakasema: Tunakubashiria kwa haki, basi usiwe miongoni mwa wanaokata tamaa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ وَمَن يَقۡنَطُ مِن رَّحۡمَةِ رَبِّهِۦٓ إِلَّا ٱلضَّآلُّونَ
Akasema: Na ni nani anayekata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi isipokuwa wapotovu?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ فَمَا خَطۡبُكُمۡ أَيُّهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ
Akasema: Hebu mna jambo gani, enyi wajumbe?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُوٓاْ إِنَّآ أُرۡسِلۡنَآ إِلَىٰ قَوۡمٖ مُّجۡرِمِينَ
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wahalifu!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمۡ أَجۡمَعِينَ
Isipokuwa watu wa familia ya Lut'. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ قَدَّرۡنَآ إِنَّهَا لَمِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ
Isipokuwa mkewe. Tumekwishapitisha kwamba huyo hakika atakuwa miongoni mwa watakaosalia nyuma.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَلَمَّا جَآءَ ءَالَ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلُونَ
Basi wajumbe hao walipowajia watu wa familia ya Lut'.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ إِنَّكُمۡ قَوۡمٞ مُّنكَرُونَ
(Lut') Alisema: Hakika nyinyi ni kaumu msiojulikana.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُواْ بَلۡ جِئۡنَٰكَ بِمَا كَانُواْ فِيهِ يَمۡتَرُونَ
Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyokuwa wakiyafanyia shaka.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَأَتَيۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ
Na tumekujia kwa Haki, na hakika sisi ni wakweli.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَسۡرِ بِأَهۡلِكَ بِقِطۡعٖ مِّنَ ٱلَّيۡلِ وَٱتَّبِعۡ أَدۡبَٰرَهُمۡ وَلَا يَلۡتَفِتۡ مِنكُمۡ أَحَدٞ وَٱمۡضُواْ حَيۡثُ تُؤۡمَرُونَ
Basi ondoka na ahali zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende huko mnakoamrishwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَقَضَيۡنَآ إِلَيۡهِ ذَٰلِكَ ٱلۡأَمۡرَ أَنَّ دَابِرَ هَٰٓؤُلَآءِ مَقۡطُوعٞ مُّصۡبِحِينَ
Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa amekwishakatiliwa mbali.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَجَآءَ أَهۡلُ ٱلۡمَدِينَةِ يَسۡتَبۡشِرُونَ
Na wakaja watu wa mji huo huku wamefurahi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ ضَيۡفِي فَلَا تَفۡضَحُونِ
Akasema: Hakika hawa ni wageni wangu. Basi msinifedheheshe.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُخۡزُونِ
Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالُوٓاْ أَوَلَمۡ نَنۡهَكَ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wakasema: Kwani hatukukukataza (kuwakaribisha) walimwengu hawa?
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
قَالَ هَٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِيٓ إِن كُنتُمۡ فَٰعِلِينَ
Akasema, "Hawa binti zangu (waoeni)[1], ikiwa nyinyi ni watendaji."
[1] Lut'i, amani iwe juu yake, alimaanisha kwamba hawa ni binti zangu miongoni mwa wanawake wenu, basi waoeni hao.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَعَمۡرُكَ إِنَّهُمۡ لَفِي سَكۡرَتِهِمۡ يَعۡمَهُونَ
Ninaapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُشۡرِقِينَ
Basi ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَجَعَلۡنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن سِجِّيلٍ
Kwa hivyo, tukaugeuza mji huo juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa kutoka Motoni.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّلۡمُتَوَسِّمِينَ
Hakika katika hayo zipo ishara kwa wanaotafakari na kuzingatia.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٖ مُّقِيمٍ
Na hakika miji hii ipo kwenye njia wazi inayopitiwa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ
Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَإِن كَانَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ لَظَٰلِمِينَ
Na hakika watu wa Kichakani walikuwa madhalimu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱنتَقَمۡنَا مِنۡهُمۡ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٖ مُّبِينٖ
Kwa hivyo tukawaadhibu. Na hakika miji miwili hii iko kwenye njia iliyo wazi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَقَدۡ كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡحِجۡرِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ
Na bila ya shaka wakazi wa Hijr waliwakadhibisha Mitume.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَءَاتَيۡنَٰهُمۡ ءَايَٰتِنَا فَكَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ
Na tuliwaletea ishara zetu, nao wakawa wanazipa migongo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَكَانُواْ يَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتًا ءَامِنِينَ
Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُصۡبِحِينَ
Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَمَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ
Na hayakuwafaa yale waliyokuwa wakiyachuma.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۗ وَإِنَّ ٱلسَّاعَةَ لَأٓتِيَةٞۖ فَٱصۡفَحِ ٱلصَّفۡحَ ٱلۡجَمِيلَ
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyo ndani yake isipokuwa kwa haki. Na hakika Saa ya Kiyama itafika. Basi samehe msamaha mzuri.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ ٱلۡخَلَّٰقُ ٱلۡعَلِيمُ
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji, Mwenye kujua zaidi.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَٰكَ سَبۡعٗا مِّنَ ٱلۡمَثَانِي وَٱلۡقُرۡءَانَ ٱلۡعَظِيمَ
Na hakika tumekupa (aya) saba zinazosomwa mara kwa mara, na Qur-ani Tukufu.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
لَا تَمُدَّنَّ عَيۡنَيۡكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعۡنَا بِهِۦٓ أَزۡوَٰجٗا مِّنۡهُمۡ وَلَا تَحۡزَنۡ عَلَيۡهِمۡ وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِلۡمُؤۡمِنِينَ
Kamwe usivinyoshee macho yako vitu tulivyowastarehesha kwavyo makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَقُلۡ إِنِّيٓ أَنَا ٱلنَّذِيرُ ٱلۡمُبِينُ
Na sema: Hakika mimi ndiye mwonyaji mwenye kubainisha.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
كَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَى ٱلۡمُقۡتَسِمِينَ
Kama hivyo tuliwateremshia waliogawa.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ٱلَّذِينَ جَعَلُواْ ٱلۡقُرۡءَانَ عِضِينَ
Ambao waliifanya Qur-ani vipande vipande.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَوَرَبِّكَ لَنَسۡـَٔلَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ
Basi ninaapa kwa Mola wako Mlezi! Lazima tutawauliza wote.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
عَمَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Kuhusu yale waliyokuwa wakiyatenda.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَٱصۡدَعۡ بِمَا تُؤۡمَرُ وَأَعۡرِضۡ عَنِ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Basi wewe yadhihirishe yale uliyoamrishwa, na jitenge mbali na washirikina.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
إِنَّا كَفَيۡنَٰكَ ٱلۡمُسۡتَهۡزِءِينَ
Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanaofanya stihizai.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
ٱلَّذِينَ يَجۡعَلُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَۚ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ
Ambao wanafanya mungu mwingine kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi watakujajua!
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَلَقَدۡ نَعۡلَمُ أَنَّكَ يَضِيقُ صَدۡرُكَ بِمَا يَقُولُونَ
Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَكُن مِّنَ ٱلسَّٰجِدِينَ
Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumsifu, na uwe miongoni mwa wanaomsujudia.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
وَٱعۡبُدۡ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأۡتِيَكَ ٱلۡيَقِينُ
Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.
ตัฟสีรต่างๆ​ ภาษาอาหรับ:
 
แปลความหมาย​ สูเราะฮ์: Al-Hijr
สารบัญสูเราะฮ์ หมายเลข​หน้า​
 
แปล​ความหมาย​อัลกุรอาน​ - คำแปลภาษาสวาฮิลี - ศูนย์การแปลรุว๊าด - สารบัญ​คำแปล

แปลโดยทีมงานศูนย์แปลรุว๊าด ร่วมกับสมาคมการเผยแพร่ศาสนาอิสลามที่รอบวะฮ์ และสมาคมบริการเนื้อหาอิสลามด้วยภาษาต่าง ๆ

ปิด