قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى


مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: سۈرە بۇرۇج   ئايەت:

Surat Al-Buruj

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡبُرُوجِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu zenye njia za kupitia jua na mwezi.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡمَوۡعُودِ
Na kwa Siku ya Kiyama ambayo Amewaahidi viumbe kuwa Atawakusanya.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَشَاهِدٖ وَمَشۡهُودٖ
Na kwa shahidi, mwenye kutoa ushahidi, na mwenye kutolewa ushahidi juu yake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Anachokitaka. Lakini kiumbe hafai kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ
Wamelaaniwa waliofukua chini ya ardhi shimo kubwa ili kuwatesa Waumini.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ
Wakawasha moto mkubwa wenye kuni nyingi.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ
Wakawa wamekaa kwenye kingo za shimo hilo.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ
Wakishuhudia vitendo vya mateso na adhabu wanavyowafanyia Waumini.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ
Na hawakuwatesa mateso hayo isipokuwa wenye kuteswa walikuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu Mshindi Asiyeshindwa, Mhimidiwa wa maneno Yake vitendo Vyake na sifa Zake.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ
Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi Ambaye, kutakasika na sifa za upungufu ni kwake, Anashuhudia kila kitu, hakuna kinachofichika kwake.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ
Hakika, wale waliowachoma kwa moto Waumini, wa kike na wa kiume, ili kuwazuia watu na dini ya Mwenyezi Mungu, kisha wasitubie, watapata, Siku ya Akhera, adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu kali yenye kuchoma.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya amali njema, watapata Pepo ambayo chini ya majumba yake ya kifahari yapita mito. Huko ni kufaulu kukubwa.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
Hakika malipizo ya Mola wako kwa maadui Zake na mateso Yake juu yao ni mazito.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ
Ndiye Yeye Mwenye kuanzisha kuumba na kisha kurudisha.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ
Ndiye Yeye Mwingi wa kusamehe kwa wenye kutubia, Mwingi wa mapenzi kwa wanaoikurubisha kwake.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ
Mwenye Arshi tukufu.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ
Mfanya Alitakalo: hakuna kitu Anachotaka kiwe kisiwe.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ
Je, ewe Mtume, imekufikia habari ya makundi yaliyokufuru na kukanusha Mitume walioletwa, ya
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ
Firauni na Thamūd, misiba na adhabu iliyowashukia? Hawakuzingatia kwa habari hiyo.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ
Bali waliokufuru waendelea kukanusha kwao, kama walivyokuwa waliokuja kabla yao.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ
Na Mwenyezi Mungu Amewazunguka kwa Ujuzi na Uweza Wake, hakuna chenye kufichika Kwake kuhusu wao na vitendo vyao. Hii Qu’ani siyo kama wanavyodai wenye kukanusha katika washirikina kuwa ni mashairi na uchawi ndipo wakaikanusha.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ
Bali hii ni Qur’ani kubwa iliyo tukufu,
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ
iliyomo kwenye Ubao Uliohifadhiwa, haufikiwi na kubadilishwa wala kupotoshwa.
ئەرەپچە تەپسىرلەر:
 
مەنالار تەرجىمىسى سۈرە: سۈرە بۇرۇج
سۈرە مۇندەرىجىسى بەت نومۇرى
 
قۇرئان كەرىم مەنىلىرىنىڭ تەرجىمىسى - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - تەرجىمىلەر مۇندەرىجىسى

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

تاقاش