Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs * - Lexique des traductions


Traduction des sens Sourate: AL-BOUROUJ   Verset:

Surat Al-Buruj

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡبُرُوجِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu zenye njia za kupitia jua na mwezi.
Les exégèses en arabe:
وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡمَوۡعُودِ
Na kwa Siku ya Kiyama ambayo Amewaahidi viumbe kuwa Atawakusanya.
Les exégèses en arabe:
وَشَاهِدٖ وَمَشۡهُودٖ
Na kwa shahidi, mwenye kutoa ushahidi, na mwenye kutolewa ushahidi juu yake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Anachokitaka. Lakini kiumbe hafai kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Les exégèses en arabe:
قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ
Wamelaaniwa waliofukua chini ya ardhi shimo kubwa ili kuwatesa Waumini.
Les exégèses en arabe:
ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ
Wakawasha moto mkubwa wenye kuni nyingi.
Les exégèses en arabe:
إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ
Wakawa wamekaa kwenye kingo za shimo hilo.
Les exégèses en arabe:
وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ
Wakishuhudia vitendo vya mateso na adhabu wanavyowafanyia Waumini.
Les exégèses en arabe:
وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ
Na hawakuwatesa mateso hayo isipokuwa wenye kuteswa walikuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu Mshindi Asiyeshindwa, Mhimidiwa wa maneno Yake vitendo Vyake na sifa Zake.
Les exégèses en arabe:
ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ
Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi Ambaye, kutakasika na sifa za upungufu ni kwake, Anashuhudia kila kitu, hakuna kinachofichika kwake.
Les exégèses en arabe:
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ
Hakika, wale waliowachoma kwa moto Waumini, wa kike na wa kiume, ili kuwazuia watu na dini ya Mwenyezi Mungu, kisha wasitubie, watapata, Siku ya Akhera, adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu kali yenye kuchoma.
Les exégèses en arabe:
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya amali njema, watapata Pepo ambayo chini ya majumba yake ya kifahari yapita mito. Huko ni kufaulu kukubwa.
Les exégèses en arabe:
إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
Hakika malipizo ya Mola wako kwa maadui Zake na mateso Yake juu yao ni mazito.
Les exégèses en arabe:
إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ
Ndiye Yeye Mwenye kuanzisha kuumba na kisha kurudisha.
Les exégèses en arabe:
وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ
Ndiye Yeye Mwingi wa kusamehe kwa wenye kutubia, Mwingi wa mapenzi kwa wanaoikurubisha kwake.
Les exégèses en arabe:
ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ
Mwenye Arshi tukufu.
Les exégèses en arabe:
فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ
Mfanya Alitakalo: hakuna kitu Anachotaka kiwe kisiwe.
Les exégèses en arabe:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ
Je, ewe Mtume, imekufikia habari ya makundi yaliyokufuru na kukanusha Mitume walioletwa, ya
Les exégèses en arabe:
فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ
Firauni na Thamūd, misiba na adhabu iliyowashukia? Hawakuzingatia kwa habari hiyo.
Les exégèses en arabe:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ
Bali waliokufuru waendelea kukanusha kwao, kama walivyokuwa waliokuja kabla yao.
Les exégèses en arabe:
وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ
Na Mwenyezi Mungu Amewazunguka kwa Ujuzi na Uweza Wake, hakuna chenye kufichika Kwake kuhusu wao na vitendo vyao. Hii Qu’ani siyo kama wanavyodai wenye kukanusha katika washirikina kuwa ni mashairi na uchawi ndipo wakaikanusha.
Les exégèses en arabe:
بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ
Bali hii ni Qur’ani kubwa iliyo tukufu,
Les exégèses en arabe:
فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ
iliyomo kwenye Ubao Uliohifadhiwa, haufikiwi na kubadilishwa wala kupotoshwa.
Les exégèses en arabe:
 
Traduction des sens Sourate: AL-BOUROUJ
Lexique des sourates Numéro de la page
 
Traduction des sens du Noble Coran - Traduction en Swahili - 'AbdaLlah Muhammad et Nasser Khamîs - Lexique des traductions

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Fermeture