Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Burūj   Ayah:

Surat Al-Buruj

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلۡبُرُوجِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu zenye njia za kupitia jua na mwezi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡمَوۡعُودِ
Na kwa Siku ya Kiyama ambayo Amewaahidi viumbe kuwa Atawakusanya.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَشَاهِدٖ وَمَشۡهُودٖ
Na kwa shahidi, mwenye kutoa ushahidi, na mwenye kutolewa ushahidi juu yake. Mwenyezi Mungu Huapa kwa Anachokitaka. Lakini kiumbe hafai kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Ang mga Tafsir na Arabe:
قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ
Wamelaaniwa waliofukua chini ya ardhi shimo kubwa ili kuwatesa Waumini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ
Wakawasha moto mkubwa wenye kuni nyingi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ
Wakawa wamekaa kwenye kingo za shimo hilo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ
Wakishuhudia vitendo vya mateso na adhabu wanavyowafanyia Waumini.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ
Na hawakuwatesa mateso hayo isipokuwa wenye kuteswa walikuwa wanamuamini Mwenyezi Mungu Mshindi Asiyeshindwa, Mhimidiwa wa maneno Yake vitendo Vyake na sifa Zake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ
Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi Ambaye, kutakasika na sifa za upungufu ni kwake, Anashuhudia kila kitu, hakuna kinachofichika kwake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ
Hakika, wale waliowachoma kwa moto Waumini, wa kike na wa kiume, ili kuwazuia watu na dini ya Mwenyezi Mungu, kisha wasitubie, watapata, Siku ya Akhera, adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu kali yenye kuchoma.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ
Wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya amali njema, watapata Pepo ambayo chini ya majumba yake ya kifahari yapita mito. Huko ni kufaulu kukubwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ
Hakika malipizo ya Mola wako kwa maadui Zake na mateso Yake juu yao ni mazito.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ
Ndiye Yeye Mwenye kuanzisha kuumba na kisha kurudisha.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ
Ndiye Yeye Mwingi wa kusamehe kwa wenye kutubia, Mwingi wa mapenzi kwa wanaoikurubisha kwake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ
Mwenye Arshi tukufu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ
Mfanya Alitakalo: hakuna kitu Anachotaka kiwe kisiwe.
Ang mga Tafsir na Arabe:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ
Je, ewe Mtume, imekufikia habari ya makundi yaliyokufuru na kukanusha Mitume walioletwa, ya
Ang mga Tafsir na Arabe:
فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ
Firauni na Thamūd, misiba na adhabu iliyowashukia? Hawakuzingatia kwa habari hiyo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ
Bali waliokufuru waendelea kukanusha kwao, kama walivyokuwa waliokuja kabla yao.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ
Na Mwenyezi Mungu Amewazunguka kwa Ujuzi na Uweza Wake, hakuna chenye kufichika Kwake kuhusu wao na vitendo vyao. Hii Qu’ani siyo kama wanavyodai wenye kukanusha katika washirikina kuwa ni mashairi na uchawi ndipo wakaikanusha.
Ang mga Tafsir na Arabe:
بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ
Bali hii ni Qur’ani kubwa iliyo tukufu,
Ang mga Tafsir na Arabe:
فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ
iliyomo kwenye Ubao Uliohifadhiwa, haufikiwi na kubadilishwa wala kupotoshwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Burūj
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis - Indise ng mga Salin

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an sa Wikang Swahili. Isinalin ito nina Doktor Abdullah Muhammad Abu Bakr at Shaykh Nasir Khamis. Inilathala ito ng King Fahd Glorious Quran Printing Complex sa Madinah Munawwarah, imprenta ng taong 1435 H.

Isara