Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis * - Indise ng mga Salin


Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Inshiqāq   Ayah:

Surat Al-Inshiqaq

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتۡ
Pindi mbingu itakapopasuka na kudhihiri mawingu katika pasuko zake Siku ya Kiyama.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ipasuke, na inastahili kufuata amri hiyo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ
Na pindi ardhi itakapotandikwa na kukunjuliwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ
Na milima yake kuvunjwa-vunjwa Siku hiyo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ifanye hivyo, na inastahili kufuata amri hiyo.
Ang mga Tafsir na Arabe:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدۡحٗا فَمُلَٰقِيهِ
Ewe binadamu, wewe unaenda kwa Mwenyezi Mungu na unafanya amali nzuri na mbaya, kisha utakutana na Yeye Siku ya Kiyama. Na huna budi kupata kutoka Kwake malipo mazuri zaidi ya amali yako njema au yanayolingana na amali yako mbaya.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ
Yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa mkono wake wa kulia,
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا
naye ni yule aliyemuamini Mola wake, atahesabiwa hesabu pesi.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا
Na atarudi kwa watu wake Peponi akiwa ni mwenye furaha.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ
Na yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa nyuma ya mgongo wake,
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا
naye ni yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu, ataita maangamvu na hasara,
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَيَصۡلَىٰ سَعِيرًا
na ataingia Motoni.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُۥ كَانَ فِيٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورًا
Hakika yeye alikuwa kwa watu wake ulimwenguni ni mwenye furaha na majivuno, hafikirii mwisho wake utakuwa namna gani.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ
Alidhani hatarudi kwa Muumba wake, akiwa hai, kwa kuhesabiwa.
Ang mga Tafsir na Arabe:
بَلَىٰٓۚ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرٗا
Sivyo hivyo! Mwenyezi Mungu Atamrudisha kama alivomuumba na kumlipa kwa amali zake. Kwani Yeye kwake ni Mtambuzi na kwa hali yake ni Mjuzi kuanzia Alipomuumba mpaka kumfufua.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلشَّفَقِ
Mwenyezi Mungu Ameapa kwa wekundu wa pambizo za mbingu wakati wa kutwa jua.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلَّيۡلِ وَمَا وَسَقَ
Na kwa usiku na viunbe tofauti - tofauti vya kutambaa, kuruka na kutembea kwa miguu, uliokusanya.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ
Na kwa mwezi ukamilikapo mwangaza wake.
Ang mga Tafsir na Arabe:
لَتَرۡكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٖ
Mtapitia, enyi watu, miongo mbalimbali na hali tofauti : kutoka kwenye tone la manii, kuptia pande la damu, nofu la nyama hadi kutiwa roho, mpaka kufa na mpaka kufufuliwa. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, afanyapo hilo atakuwa ameingia kwenye ushirikina.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَمَا لَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Ni kitu gani kinachowazuia kumwamini baada ya aya zake kufafanuliwa kwao?
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقُرۡءَانُ لَا يَسۡجُدُونَۤ۩
Na wana nini wao wanaposomewa Qur’ani hawamsujudii Mwenyezi Mungu wala hawajisalimishi kufuata yaliyokuja ndani yake?
Ang mga Tafsir na Arabe:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُكَذِّبُونَ
Hakika tabia ya waliokufuru ni kuikanusha na kuikataa haki.
Ang mga Tafsir na Arabe:
وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يُوعُونَ
Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa ukaidi wao wanaouficha kwenye nyoyo zao hali wao wanajua kuwa yale yaliyoletwa na Qur’ani ni kweli.
Ang mga Tafsir na Arabe:
فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Basi wape bishara, ewe Mtume, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Amewaandalia adhabu yenye uchungu.
Ang mga Tafsir na Arabe:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونِۭ
Lakini wale wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakatekeleza amri waliyofaradhiwa na Mwenyezi Mungu watakuwa na malipo, Siku ya Akhera, yasiyokatika wala kupungua.
Ang mga Tafsir na Arabe:
 
Salin ng mga Kahulugan Surah: Al-Inshiqāq
Indise ng mga Surah Numero ng Pahina
 
Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an - Salin sa Wikang Swahili nina Abdullah Muhammad at Nasir Khamis - Indise ng mga Salin

Salin ng mga Kahulugan ng Marangal na Qur'an sa Wikang Swahili. Isinalin ito nina Doktor Abdullah Muhammad Abu Bakr at Shaykh Nasir Khamis. Inilathala ito ng King Fahd Glorious Quran Printing Complex sa Madinah Munawwarah, imprenta ng taong 1435 H.

Isara