Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis * - Përmbajtja e përkthimeve


Përkthimi i kuptimeve Surja: Suretu El Inshikak   Ajeti:

Surat Al-Inshiqaq

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتۡ
Pindi mbingu itakapopasuka na kudhihiri mawingu katika pasuko zake Siku ya Kiyama.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ipasuke, na inastahili kufuata amri hiyo.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ
Na pindi ardhi itakapotandikwa na kukunjuliwa.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ
Na milima yake kuvunjwa-vunjwa Siku hiyo.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ifanye hivyo, na inastahili kufuata amri hiyo.
Tefsiret në gjuhën arabe:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدۡحٗا فَمُلَٰقِيهِ
Ewe binadamu, wewe unaenda kwa Mwenyezi Mungu na unafanya amali nzuri na mbaya, kisha utakutana na Yeye Siku ya Kiyama. Na huna budi kupata kutoka Kwake malipo mazuri zaidi ya amali yako njema au yanayolingana na amali yako mbaya.
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ
Yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa mkono wake wa kulia,
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا
naye ni yule aliyemuamini Mola wake, atahesabiwa hesabu pesi.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا
Na atarudi kwa watu wake Peponi akiwa ni mwenye furaha.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ
Na yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa nyuma ya mgongo wake,
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا
naye ni yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu, ataita maangamvu na hasara,
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَيَصۡلَىٰ سَعِيرًا
na ataingia Motoni.
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِنَّهُۥ كَانَ فِيٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورًا
Hakika yeye alikuwa kwa watu wake ulimwenguni ni mwenye furaha na majivuno, hafikirii mwisho wake utakuwa namna gani.
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ
Alidhani hatarudi kwa Muumba wake, akiwa hai, kwa kuhesabiwa.
Tefsiret në gjuhën arabe:
بَلَىٰٓۚ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرٗا
Sivyo hivyo! Mwenyezi Mungu Atamrudisha kama alivomuumba na kumlipa kwa amali zake. Kwani Yeye kwake ni Mtambuzi na kwa hali yake ni Mjuzi kuanzia Alipomuumba mpaka kumfufua.
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلشَّفَقِ
Mwenyezi Mungu Ameapa kwa wekundu wa pambizo za mbingu wakati wa kutwa jua.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَٱلَّيۡلِ وَمَا وَسَقَ
Na kwa usiku na viunbe tofauti - tofauti vya kutambaa, kuruka na kutembea kwa miguu, uliokusanya.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ
Na kwa mwezi ukamilikapo mwangaza wake.
Tefsiret në gjuhën arabe:
لَتَرۡكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٖ
Mtapitia, enyi watu, miongo mbalimbali na hali tofauti : kutoka kwenye tone la manii, kuptia pande la damu, nofu la nyama hadi kutiwa roho, mpaka kufa na mpaka kufufuliwa. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, afanyapo hilo atakuwa ameingia kwenye ushirikina.
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَمَا لَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Ni kitu gani kinachowazuia kumwamini baada ya aya zake kufafanuliwa kwao?
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقُرۡءَانُ لَا يَسۡجُدُونَۤ۩
Na wana nini wao wanaposomewa Qur’ani hawamsujudii Mwenyezi Mungu wala hawajisalimishi kufuata yaliyokuja ndani yake?
Tefsiret në gjuhën arabe:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُكَذِّبُونَ
Hakika tabia ya waliokufuru ni kuikanusha na kuikataa haki.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يُوعُونَ
Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa ukaidi wao wanaouficha kwenye nyoyo zao hali wao wanajua kuwa yale yaliyoletwa na Qur’ani ni kweli.
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Basi wape bishara, ewe Mtume, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Amewaandalia adhabu yenye uchungu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونِۭ
Lakini wale wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakatekeleza amri waliyofaradhiwa na Mwenyezi Mungu watakuwa na malipo, Siku ya Akhera, yasiyokatika wala kupungua.
Tefsiret në gjuhën arabe:
 
Përkthimi i kuptimeve Surja: Suretu El Inshikak
Përmbajtja e sureve Numri i faqes
 
Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Përmbajtja e përkthimeve

Përkthimi i kuptimeve të Kuranit në suahilishte - Përkthyer nga Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Botuar nga Kompleksi Mbreti Fehd për Botimin e Mushafit Fisnik në Medinë. Viti i botimit: 1435 h.

Mbyll