クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis * - 対訳の目次


対訳 章: 割れる章   節:

Surat Al-Inshiqaq

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتۡ
Pindi mbingu itakapopasuka na kudhihiri mawingu katika pasuko zake Siku ya Kiyama.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ipasuke, na inastahili kufuata amri hiyo.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ
Na pindi ardhi itakapotandikwa na kukunjuliwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ
Na milima yake kuvunjwa-vunjwa Siku hiyo.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ
Na ikatii amri ya Mola wake ya kuwa ifanye hivyo, na inastahili kufuata amri hiyo.
アラビア語 クルアーン注釈:
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدۡحٗا فَمُلَٰقِيهِ
Ewe binadamu, wewe unaenda kwa Mwenyezi Mungu na unafanya amali nzuri na mbaya, kisha utakutana na Yeye Siku ya Kiyama. Na huna budi kupata kutoka Kwake malipo mazuri zaidi ya amali yako njema au yanayolingana na amali yako mbaya.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ
Yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa mkono wake wa kulia,
アラビア語 クルアーン注釈:
فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا
naye ni yule aliyemuamini Mola wake, atahesabiwa hesabu pesi.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا
Na atarudi kwa watu wake Peponi akiwa ni mwenye furaha.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ
Na yule mwenye kupewa waraka wa amali zake kwa nyuma ya mgongo wake,
アラビア語 クルアーン注釈:
فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا
naye ni yule aliyemkanusha Mwenyezi Mungu, ataita maangamvu na hasara,
アラビア語 クルアーン注釈:
وَيَصۡلَىٰ سَعِيرًا
na ataingia Motoni.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّهُۥ كَانَ فِيٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورًا
Hakika yeye alikuwa kwa watu wake ulimwenguni ni mwenye furaha na majivuno, hafikirii mwisho wake utakuwa namna gani.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ
Alidhani hatarudi kwa Muumba wake, akiwa hai, kwa kuhesabiwa.
アラビア語 クルアーン注釈:
بَلَىٰٓۚ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرٗا
Sivyo hivyo! Mwenyezi Mungu Atamrudisha kama alivomuumba na kumlipa kwa amali zake. Kwani Yeye kwake ni Mtambuzi na kwa hali yake ni Mjuzi kuanzia Alipomuumba mpaka kumfufua.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلشَّفَقِ
Mwenyezi Mungu Ameapa kwa wekundu wa pambizo za mbingu wakati wa kutwa jua.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱلَّيۡلِ وَمَا وَسَقَ
Na kwa usiku na viunbe tofauti - tofauti vya kutambaa, kuruka na kutembea kwa miguu, uliokusanya.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ
Na kwa mwezi ukamilikapo mwangaza wake.
アラビア語 クルアーン注釈:
لَتَرۡكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٖ
Mtapitia, enyi watu, miongo mbalimbali na hali tofauti : kutoka kwenye tone la manii, kuptia pande la damu, nofu la nyama hadi kutiwa roho, mpaka kufa na mpaka kufufuliwa. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, afanyapo hilo atakuwa ameingia kwenye ushirikina.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَمَا لَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ
Ni kitu gani kinachowazuia kumwamini baada ya aya zake kufafanuliwa kwao?
アラビア語 クルアーン注釈:
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقُرۡءَانُ لَا يَسۡجُدُونَۤ۩
Na wana nini wao wanaposomewa Qur’ani hawamsujudii Mwenyezi Mungu wala hawajisalimishi kufuata yaliyokuja ndani yake?
アラビア語 クルアーン注釈:
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُكَذِّبُونَ
Hakika tabia ya waliokufuru ni kuikanusha na kuikataa haki.
アラビア語 クルアーン注釈:
وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يُوعُونَ
Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi zaidi wa ukaidi wao wanaouficha kwenye nyoyo zao hali wao wanajua kuwa yale yaliyoletwa na Qur’ani ni kweli.
アラビア語 クルアーン注釈:
فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ
Basi wape bishara, ewe Mtume, kuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka na kuwa juu, Amewaandalia adhabu yenye uchungu.
アラビア語 クルアーン注釈:
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونِۭ
Lakini wale wanaomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na wakatekeleza amri waliyofaradhiwa na Mwenyezi Mungu watakuwa na malipo, Siku ya Akhera, yasiyokatika wala kupungua.
アラビア語 クルアーン注釈:
 
対訳 章: 割れる章
章名の目次 ページ番号
 
クルアーンの対訳 - スワヒリ語対訳 - Abdullah Muhammad and Nasir Khamis - 対訳の目次

クルアーン・スワヒリ語対訳 - Dr. Abdalla Mohamed Abubakar and Nassor Khamis

閉じる