Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилийча таржима - Али Муҳсин ал-Бервааний * - Таржималар мундарижаси

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Маънолар таржимаси Сура: Ҳумаза сураси   Оят:

Surat Al-Humazah

وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ
Ole wake kila safihi, msengenyaji!
Atapata adhabu kali na maangamio huyo ambaye mtindo wake ni kuwafedhehi watu kwa kauli au kwa ishara, au kuwasengenya kuwavunjia hishima zao.
Арабча тафсирлар:
ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ
Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
Ambaye amekusanya chungu ya mali na akawa kazi yake kuyahisabu tu, kwa kuona ladha huko kuhisabu.
Арабча тафсирлар:
يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
Anadhani huyo kuwa mali yake yatamweka milele duniani, na yatamkinga na hayo anayo yachukia?
Арабча тафсирлар:
كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
Na aache dhana hiyo! Wallahi! Hapana shaka yoyote kwa vitendo vyake viovu hivyo atakuja tumbukizwa katika Moto unao vuruga kila kinacho tupwa humo!
Арабча тафсирлар:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
Na kitu gani kitacho kujuvya nini ukweli wa Moto huu wa H'ut'ama?
Арабча тафсирлар:
نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa kwa amri yake, na daima unawaka!
Арабча тафсирлар:
ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ
Ambao unapanda nyoyoni.
Ambao unafikilia nyoyoni na kuzizunguka nyoyo.
Арабча тафсирлар:
إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ
Hakika huo utafungiwa nao
Huo utakuwa umefungwa milango yake, na wao watakuwa wamefungwa humo ndani
Арабча тафсирлар:
فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ
Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
Kwenye maguzo yaliyo nyooka. Hawawezi kutaharaki, wala kutoka.
Арабча тафсирлар:
 
Маънолар таржимаси Сура: Ҳумаза сураси
Суралар мундарижаси Бет рақами
 
Қуръони Карим маъноларининг таржимаси - Савоҳилийча таржима - Али Муҳсин ал-Бервааний - Таржималар мундарижаси

Қуръон Карим маъноларининг савоҳилийча таржимаси, мутаржим: Али Муҳсин ал-Бервааний

Ёпиш