《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 * - 译解目录

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

含义的翻译 章: 哈姆宰   段:

Surat Al-Humazah

وَيۡلٞ لِّكُلِّ هُمَزَةٖ لُّمَزَةٍ
Ole wake kila safihi, msengenyaji!
Atapata adhabu kali na maangamio huyo ambaye mtindo wake ni kuwafedhehi watu kwa kauli au kwa ishara, au kuwasengenya kuwavunjia hishima zao.
阿拉伯语经注:
ٱلَّذِي جَمَعَ مَالٗا وَعَدَّدَهُۥ
Aliye kusanya mali na kuyahisabu.
Ambaye amekusanya chungu ya mali na akawa kazi yake kuyahisabu tu, kwa kuona ladha huko kuhisabu.
阿拉伯语经注:
يَحۡسَبُ أَنَّ مَالَهُۥٓ أَخۡلَدَهُۥ
Anadhani ya kuwa mali yake yatambakisha milele!
Anadhani huyo kuwa mali yake yatamweka milele duniani, na yatamkinga na hayo anayo yachukia?
阿拉伯语经注:
كَلَّاۖ لَيُنۢبَذَنَّ فِي ٱلۡحُطَمَةِ
Hasha! Atavurumishwa katika H'ut'ama.
Na aache dhana hiyo! Wallahi! Hapana shaka yoyote kwa vitendo vyake viovu hivyo atakuja tumbukizwa katika Moto unao vuruga kila kinacho tupwa humo!
阿拉伯语经注:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحُطَمَةُ
Na nani atakujuvya ni nini H'ut'ama?
Na kitu gani kitacho kujuvya nini ukweli wa Moto huu wa H'ut'ama?
阿拉伯语经注:
نَارُ ٱللَّهِ ٱلۡمُوقَدَةُ
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa.
Moto wa Mwenyezi Mungu ulio washwa kwa amri yake, na daima unawaka!
阿拉伯语经注:
ٱلَّتِي تَطَّلِعُ عَلَى ٱلۡأَفۡـِٔدَةِ
Ambao unapanda nyoyoni.
Ambao unafikilia nyoyoni na kuzizunguka nyoyo.
阿拉伯语经注:
إِنَّهَا عَلَيۡهِم مُّؤۡصَدَةٞ
Hakika huo utafungiwa nao
Huo utakuwa umefungwa milango yake, na wao watakuwa wamefungwa humo ndani
阿拉伯语经注:
فِي عَمَدٖ مُّمَدَّدَةِۭ
Kwenye nguzo zilio nyooshwa.
Kwenye maguzo yaliyo nyooka. Hawawezi kutaharaki, wala kutoka.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 哈姆宰
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译-阿里·穆哈森·伯瓦尼 - 译解目录

古兰经斯瓦希里语译解,阿里·穆哈森·伯瓦尼翻译

关闭