Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Câu: (179) Chương: Chương Ali 'Imran
مَّا كَانَ ٱللَّهُ لِيَذَرَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ عَلَىٰ مَآ أَنتُمۡ عَلَيۡهِ حَتَّىٰ يَمِيزَ ٱلۡخَبِيثَ مِنَ ٱلطَّيِّبِۗ وَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيُطۡلِعَكُمۡ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ وَلَٰكِنَّ ٱللَّهَ يَجۡتَبِي مِن رُّسُلِهِۦ مَن يَشَآءُۖ فَـَٔامِنُواْ بِٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦۚ وَإِن تُؤۡمِنُواْ وَتَتَّقُواْ فَلَكُمۡ أَجۡرٌ عَظِيمٞ
Hakuwa Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaacha , enyi wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wenye kuzifuata Sheria Yake kivitendo, juu ya hivyo mlivyo ya kuchanganyikana mwenye Imani na mnafiki, mpaka Ampambanue muovu na mwema, ili ajulikune mnafiki na Muumini mkweli. Na haikuwa ni katika hekima ya Mwenyezi Mungu, enyi Waumini, kwamba Atawafunulia ghaibu Anayoijua kuhusu waja Wake, mkamjua Muumini kati yao na mnafiki. Lakini Yeye Anawapambanua kwa misukosuko na mitihani. Isipokuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anamteua Amtakaye katika wajumbe Wake ili kumuonesha ujuzi wa ghaibu kwa wahyi utokao Kwake. Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Na iwapo mtaamini, imani ya kweli, na mkamuogopa Mola wenu kwa kumtii, mtapata malipo makubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Câu: (179) Chương: Chương Ali 'Imran
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại