Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis * - Mục lục các bản dịch


Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-Muddaththir   Câu:

Surat Al-Muddathir

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ
Ewe uliojifinika nguo zako!
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
قُمۡ فَأَنذِرۡ
Inuka kutoka kwenye malazi yako owaonye watu adhabu ya Menyezi Mungu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ
Na umkusudie Mola wako, Peke Yake, kwa kumtukuza, kumpwekesha na kumuabudu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ
Na usafishe nguo zako kutokana na najisi, kwani usafi wa nje ni katika kutimia usafi wa ndani.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ
Na uendelee daima kuyaepuka masanamu na mizimu, na matendo ya ushirikina yote usiyakaribie.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ
Na usitoe kitu kumpa mtu kwa lengo la kupata zaidi ya hiko. Na kwa ajili ya kupata radhi ya Mwenyezi Mungu,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ
vumilia juu ya maamrisho na makatazo.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَإِذَا نُقِرَ فِي ٱلنَّاقُورِ
Pindi patakapopulizwa kwenye barugumu mpulizo wa Ufufuzi na Uenezaji,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَذَٰلِكَ يَوۡمَئِذٖ يَوۡمٌ عَسِيرٌ
wakati huo ni wakati ambao ni mgumu kwa makafiri;
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ غَيۡرُ يَسِيرٖ
si rahisi kwao kusalimika na yale walionayo ya kujadiliwa hesabu zao na vituko vingine vikubwa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ذَرۡنِي وَمَنۡ خَلَقۡتُ وَحِيدٗا
Niache mimi, ewe Mtume, na huyu niliyemuumba ndani ya tumbo la mamake akiwa peke yake, hana mali wala watoto.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَجَعَلۡتُ لَهُۥ مَالٗا مَّمۡدُودٗا
Nikamfanya awe na mali mengi yenye kuenea na watoto waliyoko na yeye hapo Makkah hawamuondokei. Na
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَبَنِينَ شُهُودٗا
nikamsahilishia kwa kumrahisishia njia za maisha. Kisha yeye anatarajia, baada ya vitu hivi alivyopewa,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَمَهَّدتُّ لَهُۥ تَمۡهِيدٗا
nimuongezee kwenye mali yake na watoto wake na huku yeye amenikanusha. Mambo sivyo kama anavyodai huyu mwenye kuasi, mtenda dhambi.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ثُمَّ يَطۡمَعُ أَنۡ أَزِيدَ
Simuongezei zaidi ya hiko nilichompa,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَلَّآۖ إِنَّهُۥ كَانَ لِأٓيَٰتِنَا عَنِيدٗا
kwa kuwa yeye alikuwa mshindani mkanushaji wa Qur’ani na hoja za Mwenyezi Mungu kwa viumbe Wake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
سَأُرۡهِقُهُۥ صَعُودًا
Nitambebesha mateso magumu na usumbufu usio na mapumziko. Anayekusudiwa hapa ni Al-Walid mwana wa Al-Mughi rah aliyekuwa akishindana na haki na akijitokeza kupigana vita na Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. Haya ndiyo malipo ya kila mwenye kushindana na haki na kuipiga vita.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّهُۥ فَكَّرَ وَقَدَّرَ
Kwa kweli yeye aliwaza ndani ya nafsi yake akatayarisha la kusema kumtukana Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَقُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Hivyo basi akalaaniwa na akastahili, kwa hilo, maangamivu: alijiandaa vipi ndani ya nafsi yake kwa hayo matukano?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ثُمَّ قُتِلَ كَيۡفَ قَدَّرَ
Kisha pia akalaaniwa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ثُمَّ نَظَرَ
Kisha yeye alifikiria kuhusu kile alichokipanga na kukitayarisha cha kuitia dosari Qur’ani.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ
Kisha akafinya uso wake na akazidi katika hali ile ya ukunjaji uso kwa kukosa hila za kufanya na kutopata ila yoyote ya kuitia dosari Qur’ani.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ثُمَّ أَدۡبَرَ وَٱسۡتَكۡبَرَ
Kisha akarudi kuipa mgongo haki na akajiona ni mkubwa wa kutofaa kuikubali,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَقَالَ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ يُؤۡثَرُ
hapo akasema kuhusu Qur’ani, «Haya anayoyasema Muhammad si chochote isipokuwa ni uchawi uliopokewa kutoka kwa watu wa mwanzo waliopita.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا قَوۡلُ ٱلۡبَشَرِ
Haikuwa hi Qur’ani isipokuwa ni maneno ya viumbe ambayo Muhammad amejifunza kutoka kwao kisha akadai kuwa yanatoka kwa Mwenyezi Mungu.»
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ
Basi nitamuingiza kwenye moto wa Jahanamu ili alionje joto lake na achomeke kwa moto wake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ
Na ni lipi lililokujulisha wewe ni kitu gani hiyo Jahanamu?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ
Haibakishi nyama wala haiachi mfupa isipokuwa huvichoma.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ
Unageuza ngozi ya mwili, unazifanya ngozi kuwa nyeusi na unazichoma.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
عَلَيۡهَا تِسۡعَةَ عَشَرَ
Wanasimamia mambo yake na kushikilia kazi ya kuwatesa watu wake Malaika kumi na tisa katika washika zamu wa Motoni wenye nguvu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَمَا جَعَلۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ إِلَّا مَلَٰٓئِكَةٗۖ وَمَا جَعَلۡنَا عِدَّتَهُمۡ إِلَّا فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيَسۡتَيۡقِنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَيَزۡدَادَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِيمَٰنٗا وَلَا يَرۡتَابَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَ وَلِيَقُولَ ٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡكَٰفِرُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۚ كَذَٰلِكَ يُضِلُّ ٱللَّهُ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِي مَن يَشَآءُۚ وَمَا يَعۡلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَۚ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡبَشَرِ
Na hatukuwafanya washika hazina wa Motoni isipokuwa miongoni mwa Malaika washupavu. Na hatukuiweka idadi hiyo isipokuwa kuwatahini wale waliomkufuru Mwenyezi Mungu, na ili imani ya yakini ipatikane kwa wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu kwamba yaliyokuja ndani ya Qur’ani juu ya washika hazina wa Motoni ni ukweli utokao kwa Mwenyezi Mungu Aliyetukuka, kwani hayo yanaafikiana na vitabu vyao, na ili Waumini wazidi kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na waifuate Sheria Yake kivitendo, na ili wasilifanyie shaka hilo wale Mayahudi na Wanaswara waliopewa Vitabu wala wale wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na ili wapate kusema wale wenye unafiki ndani ya nyoyo zao na makafiri, «Ni lipi alilolikusudia Mwenyezi Mungu kwa idadi hii ya ajabu?» Kwa mfano wa hayo yaliyotajwa, Mwenyezi Mungu Anampoteza Anayetaka kumpoteza na Anamuongoza Anayetaka kumuongoza. Na hakuna ajuwaye idadi ya askari wa Mola wako, na miongoni mwao ni Malaika, isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke Yake. Na haukuwa huu Moto isipokuwa ni ukumbusho na mazingatio kwa watu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَلَّا وَٱلۡقَمَرِ
Mambo sivyo kama walivyotaja ya ukanushaji Mtume katika yale aliyokuja nayo! Anaapa Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kila sifa ya upungufu, kwa mwezi,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلَّيۡلِ إِذۡ أَدۡبَرَ
na kwa usiku unapogeuka kwenda zake,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلصُّبۡحِ إِذَآ أَسۡفَرَ
na kwa asubuhi inapotoa mwangaza na kufunuka,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّهَا لَإِحۡدَى ٱلۡكُبَرِ
hakika Moto ni mojawapo ya mambo makubwa,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
نَذِيرٗا لِّلۡبَشَرِ
kwa ajili ya kuwaonya na kuwatisha watu,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَتَقَدَّمَ أَوۡ يَتَأَخَّرَ
kwa anayetaka miongoni mwenu kujiweka karibu na Mola wake kwa kufanya matendo ya utiifu, au kujikalisha nyuma kwa kufanya matendo ya uasi.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ رَهِينَةٌ
Kila nafsi imefungwa na kuwekwa rahani kwa ilichokitenda, miongoni mwa matendo mema au mabaya, kwa kukichuma. Haifunguliwi mpaka itekeleze haki zilizo juu ya lazima yake na ipatiwe mateso yanayostahili kupatiwa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِلَّآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡيَمِينِ
Isipokuwa Waislamu waliotakaswa, watu wa upande wa kulia waliojikomboa shingo zao kwa utiifu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فِي جَنَّٰتٖ يَتَسَآءَلُونَ
Wao watakuwa kwenye mabustani ya Peponi ambayo sifa zake hazifikiwi ukomo. Watakuwa wakiulizana wao kwa wao
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
عَنِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ
kuhusu makafiri waliojikosea nafsi zao,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
مَا سَلَكَكُمۡ فِي سَقَرَ
«Ni lipi lililowaingiza kwenye moto wa Jahanamu na likawafanya
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
قَالُواْ لَمۡ نَكُ مِنَ ٱلۡمُصَلِّينَ
mlionje joto lake lililo kali sana?» Wahalifu waseme , «Hatukuwa ni miongoni mwa wanaoswali duniani,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَلَمۡ نَكُ نُطۡعِمُ ٱلۡمِسۡكِينَ
na hatukuwa tukitoa sadaka na kuwafanyia wema wahitaji na maskini,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ ٱلۡخَآئِضِينَ
na tulikuwa tukizungumza maneno ya ubatilifu na watu wa upotofu na upotevu,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
na tulikuwa tukiikanusha Siku ya kuhesabiwa na kulipwa,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ
mpaka kifo kikatujia na hali sisi tuko kwenye mambo hayo mabaya ya upotevu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّٰفِعِينَ
Basi hayatawafalia neno maombezi ya wenye kuombea wote, miongoni mwa Malaika, Manabii na wengineo, kwa kuwa aombewaye ni yule aliyechaguliwa na Mwenyezi Mungu na akamuidhinisha mwenye kumuombea.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ
Basi wana nini hawa washirikina wamejiepusha na Qur’ani na
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ
mawaidha yaliyomo ndani yake? Kama kwamba wao ni pundamilia wanaobabaika
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ
wanaomkimbia simba mshambulizi.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ
Lakini kila mmoja, miongoni mwa hawa washirikina, ana matumaini ateremshiwe kitabu kutoka mbinguni kilichokunjuliwa kama kile kilichoteremshiwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Mambo si hivyo kama wanavyodai. Ukweli ni kwamba wao hawaiogopi Akhera wala hawaamini kuwa kuna kufufuliwa na kulipwa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ
Ni kweli kwamba Qur’ani ni mawaidha yenye ufasaha, yanayotosha kuwafanya wao wawaidhike.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Anayetaka kuwaidhika, basi na awaidhike kwa yaliyomo ndani yake na anufaike na uongofu wake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ
Na hawawaidhiki kwayo isipokuwa iwapo Mwenyezi Mungu Amewatakia kuongoka. Yeye, kutakasika na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye Anayestahiki kuogopewa na kutiiwa, na Ndiye Anayestahiki kumsamehe anayemuamini Yeye na kumtii.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-Muddaththir
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Abdullah Muhammad và Nasir Khamis - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili, dịch thuật bởi tiến sĩ 'Abdalla Muhammad Abu Bakar và Nasir Khamis.

Đóng lại