Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani * - Mục lục các bản dịch

XML CSV Excel API
Please review the Terms and Policies

Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-Nazi-'at   Câu:

Surat An-Nazi'at

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu!
Ninaapa kwa kila kilicho pewa uwezo wa kuving'oa vitu kutokana na pahala pao kwa nguvu,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا
Na kwa wanao toa kwa upole!
Na kwa kila kilicho pewa uwezo wa kuvitoa vitu kwa utaratibu na ulaini,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا
Na wanao ogelea!
Na kwa kila kilicho pewa mbio za kutekeleza kazi yake kwa sahala na wepesi.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا
Wakishindana mbio!
Na kwa vinavyo shindania kutimiza waajibu ulio twikwa juu yao kushindania kwa juhudi,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا
Wakidabiri mambo.
Na vinavyo dabiri, kupanga, mambo na kuyaendesha kwa mujibu wa vilivyo khusishwa,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka!
Bila ya shaka Saa ya Kiyama itafika; hiyo siku ambayo mpulizo wa mwanzo wa barugumu utavitikisa viumbe vyote,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
Kifuate cha kufuatia.
Na mpulizo huo utafuatiwa na wa pili ambao ndio utakao kuwa wa kufufuliwa watu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga!
Siku hiyo nyoyo zitapapatika kwa khofu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ
Macho yatainama chini!
Macho ya watu yatakuwa na huzuni, manyonge.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
Watu hawa husema duniani kwa kukanya kufufuliwa: Ati tutarudishwa sisi baada ya kwisha kufa, tuumbwe tena kama tulivyo kuwa?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
Tukisha kuwa mafupa yaliyo chakaa, ati tutarejeshwa tufufuliwe upya?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
Wanasema, kwa kukanya na kejeli: Kurejea huko kama kukitokea basi ni marejeo ya khasara, na sisi si watu wa kukhasiri.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
Msidhani kurejea huko ni kuzito. Kwani hayo ni ukelele mmoja tu,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
Mara maiti wote watahudhurishwa kwenye ardhi ya mkusanyiko!
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
Ewe Muhammad! Imekufikilia hadithi ya Musa,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
Alipo mwita Mola wake Mlezi katika bonde lilio takaswa, linalo itwa "T'uwa"?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri
Akaambiwa: Nenda kwa Firauni aliye pindukia mpaka katika udhalimu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
Umwambie: Je! Huelekei kut'ahirika?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
Na mimi nikuongoze upate kumjua Mola wako Mlezi, umwogope.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
Musa akamwonyesha Firauni miujiza mikubwa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
Lakini Firauni alimkadhibisha Musa kwa aliyo kuja nayo, na akamuasi kwa aliyo mwitia.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
Kisha akamgeuzia mgongo, akenda kujitahidi kumpinga.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Akakusanya watu akanadi.
Akawakusanya wachawi, na akawaita watu,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
Mwenyezi Mungu akampa adhabu kwa kauli yake ya mwisho, nayo ni vile kusema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa. Na akampa adhabu kwa kauli yake ya mwanzo, nayo ni kumkadhibisha Musa a.s.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
Hakika katika hadithi hiyo yapo mawaidha kwa mwenye kumkhofu Mwenyezi Mungu.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
Enyi mnao kanya kufufuliwa! Kukuumbeni nyinyi ni taabu zaidi au kuziumba mbingu, kuzikusanya sehemu zake zilio tawanyika mbali mbali,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
Na kunyanyua kimo chake, na zikakaa sawa hazina tafauti wala ila?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake
Na akatia kiza katika usiku wake, na akautokeza mchana wake ukawa na mwangaza?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
Na ardhi baada ya hayo akaikunjua, na akaisawazisha, ikasilihi kukaliwa na watu wake?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
Akatoa ndani yake maji yake yanayo tibuka katika chemchem zake, na ikamiminika mito yake, na ikawa na mimea yake ya chakula kwa ajili ya watu na wanyama;
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا
Na milima akaisimamisha,
Na milima akaithibitisha imara
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
Kwa ajili ya manufaa yenu na wanyama wenu mnao wafuga!
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
Kitakapo fika Kiyama ambacho vitisho vyake vitaenea kote,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
Siku atakapo kumbuka mtu vitendo vyake vya kheri au shari,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
Na Jahannamu ikadhihirishwa wazi, akaiona kila mwenye macho kuwa ndio malipo,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
Basi ama mwenye kupita mpaka kwa maasi yake,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Na akakhiari maisha ya dunia,
Na akajichagulia nafsi yake maisha yanayo pita njia,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
Basi Moto wa Jahannamu unao babua upepo wake ndio makaazi yake wala hana mengineyo.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
Na ama mwenye kukhofu ukubwa na utukufu wa Mola wake Mlezi, na akaizuia nafsi yake na matamanio ya kumpumbaza,
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
Basi huyo nyumba ya neema ya Peponi ndio makaazi yake, wala hana penginepo.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
Ewe Muhammad! Wanakuuliza, ati, khabari za Saa ya Kiyama, itakuwa lini?
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ
Una nini wewe hata uitaje?
Ujuzi wa hayo hauko kwako hata uwatajie.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
Ujuzi wa hayo uko kwa Mola wako Mlezi tu, si kwa mwenginewe. (Nabii Isa a.s. ambaye Wakristo wanasema ni Mwana wa Mungu, au ndiye Mungu, pia anasimuliwa katika Biblia kuwa hakuijua Saa na Siku ya Kiyama. Injili ya Mathayo inanukulu maneno ya Yesu: "Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.")
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
Kwani waajibu wako ni kuwaonya wanao khofu si kuwatangazia wakati wake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
Na wao siku watakayo iona hiyo Saa ya Kiyama ni kama kwamba hawakuishi duniani zaidi kuliko jioni moja tu, au mchana wake.
Các Tafsir tiếng Ả-rập:
 
Ý nghĩa nội dung Chương: Chương Al-Nazi-'at
Mục lục các chương Kinh Số trang
 
Bản dịch ý nghĩa nội dung Qur'an - Dịch thuật tiếng Swahili - 'Ali Muhsin Al-Barwani - Mục lục các bản dịch

Bản dịch ý nghĩa nội dung Kinh Qur'an bằng tiếng Swahili do 'Ali Muhsin Al-Barwani dịch thuật

Đóng lại