Check out the new design

《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 * - 译解目录


含义的翻译 章: 奈扎尔提   段:

An-Nazi'at

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا
Ninaapa kwa wanaokomoa kwa nguvu.
阿拉伯语经注:
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا
Na kwa wanaotoa kwa upole.
阿拉伯语经注:
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا
Na wanaoogelea sawasawa.
阿拉伯语经注:
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا
Wakishindana mbio kweli kweli.
阿拉伯语经注:
فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا
Wakidabiri mambo.
阿拉伯语经注:
يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ
Siku kitakapotetemeka cha kutetemeka.
阿拉伯语经注:
تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ
Kifuate cha kufuatia.
阿拉伯语经注:
قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ
Siku hiyo nyoyo zitapigapiga.
阿拉伯语经注:
أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ
Macho yatainama chini.
阿拉伯语经注:
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
阿拉伯语经注:
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ
Hata tukiwa mifupa iliyobunguliwa?
阿拉伯语经注:
قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye hasara!
阿拉伯语经注:
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu.
阿拉伯语经注:
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
阿拉伯语经注:
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
阿拉伯语经注:
إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى
Mola wake Mlezi alipomwita katika bonde takatifu la Tuwaa, akamwambia:
阿拉伯语经注:
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
阿拉伯语经注:
فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
阿拉伯语经注:
وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
阿拉伯语经注:
فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
阿拉伯语经注:
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
Lakini alikadhibisha na akaasi.
阿拉伯语经注:
ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
阿拉伯语经注:
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
Akakusanya watu akanadi.
阿拉伯语经注:
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
阿拉伯语经注:
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
阿拉伯语经注:
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanaoogopa.
阿拉伯语经注:
ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا
Je, ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliyeijenga!
阿拉伯语经注:
رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
阿拉伯语经注:
وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
阿拉伯语经注:
وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
阿拉伯语经注:
أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake.
阿拉伯语经注:
وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا
Na milima akaisimamisha imara.
阿拉伯语经注:
مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Kwa manufaa yenu na mifugo yenu.
阿拉伯语经注:
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ
Basi itakapofika hiyo balaa kubwa,
阿拉伯语经注:
يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyoyafanya,
阿拉伯语经注:
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
阿拉伯语经注:
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
Basi ama yule aliyezidi ujeuri,
阿拉伯语经注:
وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا
Na akakhiari maisha ya dunia,
阿拉伯语经注:
فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
阿拉伯语经注:
وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ
Na ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
阿拉伯语经注:
فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makazi yake!
阿拉伯语经注:
يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
阿拉伯语经注:
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ
Una nini wewe hata uitaje?
阿拉伯语经注:
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
阿拉伯语经注:
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuihofu.
阿拉伯语经注:
كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا
Ni kama kwamba wao siku watakapoiona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.
阿拉伯语经注:
 
含义的翻译 章: 奈扎尔提
章节目录 页码
 
《古兰经》译解 - 斯瓦希里语翻译 - 拉瓦德翻译中心。 - 译解目录

由拉瓦德翻译中心团队与拉布瓦 الدعوة协会和伊斯兰内容服务协会合作翻译。

关闭