কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ ও নাসির খামীস * - অনুবাদসমূহের সূচী


অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: সূরা আত-তারেক   আয়াত:

Surat At-Tariq

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu na nyota yenye kuchomoza usiku.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ
Na ni lipi lilokujulisha ni ukubwa gani wa nyota hiyo?
আরবি তাফসীরসমূহ:
ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ
Hiyo ni nyota ing’arao na kuzagaa.
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ
Hakuna nafsi yoyote isipokuwa amewakilishwa kwayo Malaika mwenye kuchunguza na kusjili amali zake ili ihesabiwe Siku ya Kiyama.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Basi aangalie binadamu mwenye kukanusha kufufuliwa ameumbwa kwa kitu gani? Ili ajue kuwa kurudisha umbo lake mara ya pili si vigumu kama kuumbwa mara ya kwanza.
আরবি তাফসীরসমূহ:
خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ
Aliumbwa kwa manii yenye kupenyeza ndani ya uzao kwa haraka.
আরবি তাফসীরসমূহ:
يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yatokayo kwenye mgongo wa mwnamume na kifua cha mwanamke.
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ
Hakika yule Aliyemuumba binadamu kwa maji haya ni muweza wa kumrudisha kwenye uhai baada ya kufa.
আরবি তাফসীরসমূহ:
يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ
Siku zitakapofunuliwa wazi siri ziliofichwa na nafsi na kupambanuliwa njema na mbovu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ
Binadamu hatakuwa na nguvu ya kuitetea nafsi yake wala hatakuwa na mtetezi wa kumwepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ
Na Anaapa kwa mbingu yenye mvua ya kukaririka.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَٱلۡأَرۡضِ ذَاتِ ٱلصَّدۡعِ
Na ardhi yenye pasuko za kufanya mimea ichipuke.
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلٞ فَصۡلٞ
Hakika Qur’ani ni neno lenye kupambanua baina ya haki na batili.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَمَا هُوَ بِٱلۡهَزۡلِ
Na si upuuzi. Haifai kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Akifanya hivyo atakuwa amemshirikisha Mwenyezi Mungu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
إِنَّهُمۡ يَكِيدُونَ كَيۡدٗا
Hakika wenye kumkanusha Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani wanafanya vitimbi na mipango ili kuipinga haki na kuitilia nguvu batili.
আরবি তাফসীরসমূহ:
وَأَكِيدُ كَيۡدٗا
Na Mimi nafanya vitimbi kuidhihirisha haki ingawa makafiri wanatukia.Usiwe na haraka nao, ewe Mtume, kutaka wateremshiwe adhabu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
فَمَهِّلِ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَمۡهِلۡهُمۡ رُوَيۡدَۢا
Wape muhula uwangojee muda mchache wala usiwafanyie haraka, utaona adhabu itakayowafikia, mateso na maangamivu.
আরবি তাফসীরসমূহ:
 
অর্থসমূহের অনুবাদ সূরা: সূরা আত-তারেক
সূরাসমূহের সূচী পৃষ্ঠার নাম্বার
 
কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ - সোয়াহিলি ভাষায় অনুবাদ- আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ ও নাসির খামীস - অনুবাদসমূহের সূচী

সোয়াহিলি ভাষায় আল-কুরআনুল কারীমের অর্থসমূহের অনুবাদ। ড. আব্দুল্লাহ মুহাম্মদ আবূ বকর এবং শায়েখ নাসির খামীস অনূদিত।

বন্ধ