Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis * - Përmbajtja e përkthimeve


Përkthimi i kuptimeve Surja: Suretu Et Tarik   Ajeti:

Surat At-Tariq

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa mbingu na nyota yenye kuchomoza usiku.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ
Na ni lipi lilokujulisha ni ukubwa gani wa nyota hiyo?
Tefsiret në gjuhën arabe:
ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ
Hiyo ni nyota ing’arao na kuzagaa.
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ
Hakuna nafsi yoyote isipokuwa amewakilishwa kwayo Malaika mwenye kuchunguza na kusjili amali zake ili ihesabiwe Siku ya Kiyama.
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Basi aangalie binadamu mwenye kukanusha kufufuliwa ameumbwa kwa kitu gani? Ili ajue kuwa kurudisha umbo lake mara ya pili si vigumu kama kuumbwa mara ya kwanza.
Tefsiret në gjuhën arabe:
خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ
Aliumbwa kwa manii yenye kupenyeza ndani ya uzao kwa haraka.
Tefsiret në gjuhën arabe:
يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yatokayo kwenye mgongo wa mwnamume na kifua cha mwanamke.
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ
Hakika yule Aliyemuumba binadamu kwa maji haya ni muweza wa kumrudisha kwenye uhai baada ya kufa.
Tefsiret në gjuhën arabe:
يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ
Siku zitakapofunuliwa wazi siri ziliofichwa na nafsi na kupambanuliwa njema na mbovu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ
Binadamu hatakuwa na nguvu ya kuitetea nafsi yake wala hatakuwa na mtetezi wa kumwepushia adhabu ya Mwenyezi Mungu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ
Na Anaapa kwa mbingu yenye mvua ya kukaririka.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَٱلۡأَرۡضِ ذَاتِ ٱلصَّدۡعِ
Na ardhi yenye pasuko za kufanya mimea ichipuke.
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِنَّهُۥ لَقَوۡلٞ فَصۡلٞ
Hakika Qur’ani ni neno lenye kupambanua baina ya haki na batili.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَمَا هُوَ بِٱلۡهَزۡلِ
Na si upuuzi. Haifai kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Akifanya hivyo atakuwa amemshirikisha Mwenyezi Mungu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
إِنَّهُمۡ يَكِيدُونَ كَيۡدٗا
Hakika wenye kumkanusha Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na Qur’ani wanafanya vitimbi na mipango ili kuipinga haki na kuitilia nguvu batili.
Tefsiret në gjuhën arabe:
وَأَكِيدُ كَيۡدٗا
Na Mimi nafanya vitimbi kuidhihirisha haki ingawa makafiri wanatukia.Usiwe na haraka nao, ewe Mtume, kutaka wateremshiwe adhabu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
فَمَهِّلِ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَمۡهِلۡهُمۡ رُوَيۡدَۢا
Wape muhula uwangojee muda mchache wala usiwafanyie haraka, utaona adhabu itakayowafikia, mateso na maangamivu.
Tefsiret në gjuhën arabe:
 
Përkthimi i kuptimeve Surja: Suretu Et Tarik
Përmbajtja e sureve Numri i faqes
 
Përkthimi i kuptimeve të Kuranit Fisnik - Përkthimi suahilisht - Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Përmbajtja e përkthimeve

Përkthimi i kuptimeve të Kuranit në suahilishte - Përkthyer nga Abdullah Muhammed dhe Nasir Khamis - Botuar nga Kompleksi Mbreti Fehd për Botimin e Mushafit Fisnik në Medinë. Viti i botimit: 1435 h.

Mbyll