Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس * - Sadržaj prijevodā


Prijevod značenja Sura: Sura el-Adijat   Ajet:

Surat Al-Aadiyat

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا
Mwenyezi Mungu Anaapa kwa farasi wenye kwenda shoti katika njia Yake kumkabili adui, wakitoa sauti kwa kasi ya kukimbia. Haifai kwa kiumbe kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni ushirikina.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا
Na wenye kutoa cheche za moto kwa kwato zao ngumu wanapokimbia kwa kasi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا
Wenye kushambulia maadui kipindi cha asubuhi.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا
Wakarusha vumbi kwa mbio zao.
Tefsiri na arapskom jeziku:
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا
Wakautia kati, kwa kuuzunguka kwa vipando vyao, mkusanyiko wa maadui.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ
Hakika binadamu ni mkanushaji sana neema za Mola wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ
Na yeye anakubali ukanushaji wake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ
Na yeye ana pupa sana la mali.
Tefsiri na arapskom jeziku:
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani binadamu hajui linalomngojea mbele yake, pindi Mwenyezi Mungu Atakapowatoa wafu makaburini waende kuhesabiwa na kulipwa?
Tefsiri na arapskom jeziku:
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na (kwani yeye hajui) yakatolewa yaliyo ndani ya vifua: mema au maovu?.
Tefsiri na arapskom jeziku:
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Hakika Mola wao kwao na kwa amali zao, Siku Hiyo, ni Mtambuzi; hakuna chenye kufichamana Kwake.
Tefsiri na arapskom jeziku:
 
Prijevod značenja Sura: Sura el-Adijat
Indeks sura Broj stranice
 
Prijevod značenja časnog Kur'ana - الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس - Sadržaj prijevodā

ترجمة معاني القرآن الكريم إلى اللغة السواحلية، ترجمها الدكتور عبد الله محمد أبو بكر والشيخ ناصر خميس.

Zatvaranje